Bonheur Travels Tanzania
JF-Expert Member
- Dec 29, 2020
- 252
- 499
Ndugu WanaJF,
Kwa mara nyingine tena tunakuja na uzi mahsusi kwa wote wanaofanya safari kwa njia ya anga. Huu ukiwa ni mwendelezo wa mtiririko wa threads zetu za Elimu kwa Umma ambapo tunakusudia kuelimisha wasafiri na wanaotarajia kusafiri kuhusu mambo mbalimbali ili safari zao ziwe salama na zenye mafanikio bila kupata hasara wala kuharibu ratiba zao.
Leo tungependa kushauri juu ya umuhimu wa kutumia Wakala (Travel Agency) pale unapopanga safari yako iwe ni mapumziko, kutalii au kujifunza. Tutaambatanisha na huduma ya booking kwa ajili ya hoteli au sehemu za kupumzikia hasa ugenini.
Swali ambalo mara nyingi watu huuliza ni; kwanini nitumie Wakala badala ya kwenda "direct" mtandaoni au kwenye kampuni husika (mfano shirika la ndege) kukata tiketi au ku-book hoteli?
Ni kweli. Kufanya huduma moja kwa moja kwenye kampuni au shirika husika inaaminika kuwa ni njia salama na yenye mantiki kwa kila anayetumia huduma. Pia kuhusu gharama, inaaminika kuwa kukata tiketi moja kwa moja na kukata tiketi kupitia kwa wakala huenda kukawa na tofauti za bei na kadhalika, jambo ambalo sio kweli.
Hata hivyo, kuna faida kubwa zaidi kwa mteja kutumia Wakala badala ya kwenda kufanya huduma moja kwa moja kwenye wavuti au ofisi za shirika la ndege / hoteli husika. Kwa uchache, faida atazozipata ni pamoja na:
1. Wakala humsaidia mteja kuhusu mchakato mzima wa ukataji tiketi au ku-book hoteli kabla, wakati na baada ya safari/likizo husika. Hapa ni pamoja na kumsaidia kuahirisha safari wakati wa dharura, kumshauri na kumsisitiza kuhusu muda wa safari, ratiba za safari na taratibu nyingine zote ambazo mara nyingi abiria hujisahau na kujikuta wanapata hasara au wanaharibu ratiba zao.
2. Wakala humsaidia mteja kuchagua ndege au hoteli bora kulingana na bajeti yake. Mara nyingi hutokea abiria kulazimika kulipa gharama za ziada tofauti na bajeti yake ya awali pale anapofanya booking moja kwa moja bila kujua kama kuna options nyingine. Faida hii anaipata kwa wakala pekee.
3. Wakala humpa ushauri wa kweli (honest) mteja kuhusu sehemu ambazo anaweza kwenda kufurahia huduma kwa gharama rafiki kupitia machaguo ambayo wakala anayo kwenye orodha yake.
4. Uhusiano baina ya Wakala na Mashirika au Hoteli mbalimbali hurahisisha kupewa kipaumbele anapofanya booking. Hii ni kutokana na kufanya nayo kazi mara kwa mara. Ni rahisi zaidi kwa wakala kuwasiliana moja kwa moja na watoa huduma kama kuna mapendekezo anayotaka kufanyiwa kwa niaba ya mteja.
5. Wakala humpatia namba ya simu mteja ambayo watakuwa wakipigiana simu muda wowote ikiwa kuna kitu mteja anahitaji. Hilo mteja hawezi kulipata kutoka kwenye tovuti za booking au kampuni husika.
Na mengine mengi tu.
Kuhusu hofu ya gharama; mara nyingi kama sio zote mteja hulipia gharama ile ile ambayo angechajiwa na shirika la ndege/hoteli au pengine chini yake kutokana na mapendekezo ya Wakala au "ofa" ambazo wakala anapatiwa na mashirika/hoteli hayo.
Hizo ni faida na ushauri wa kitaalamu ambao tumeona tuwapatie kutokana na uzoefu tulionao kwenye industry hii. Sio shurti kufanya hivyo. Mwisho wa siku muamuzi wa mwisho ni mtu mwenyewe.
Karibuni kwa maoni na maswali kama yapo turahisishe maisha!
Kwa mara nyingine tena tunakuja na uzi mahsusi kwa wote wanaofanya safari kwa njia ya anga. Huu ukiwa ni mwendelezo wa mtiririko wa threads zetu za Elimu kwa Umma ambapo tunakusudia kuelimisha wasafiri na wanaotarajia kusafiri kuhusu mambo mbalimbali ili safari zao ziwe salama na zenye mafanikio bila kupata hasara wala kuharibu ratiba zao.
Leo tungependa kushauri juu ya umuhimu wa kutumia Wakala (Travel Agency) pale unapopanga safari yako iwe ni mapumziko, kutalii au kujifunza. Tutaambatanisha na huduma ya booking kwa ajili ya hoteli au sehemu za kupumzikia hasa ugenini.
Swali ambalo mara nyingi watu huuliza ni; kwanini nitumie Wakala badala ya kwenda "direct" mtandaoni au kwenye kampuni husika (mfano shirika la ndege) kukata tiketi au ku-book hoteli?
Ni kweli. Kufanya huduma moja kwa moja kwenye kampuni au shirika husika inaaminika kuwa ni njia salama na yenye mantiki kwa kila anayetumia huduma. Pia kuhusu gharama, inaaminika kuwa kukata tiketi moja kwa moja na kukata tiketi kupitia kwa wakala huenda kukawa na tofauti za bei na kadhalika, jambo ambalo sio kweli.
Hata hivyo, kuna faida kubwa zaidi kwa mteja kutumia Wakala badala ya kwenda kufanya huduma moja kwa moja kwenye wavuti au ofisi za shirika la ndege / hoteli husika. Kwa uchache, faida atazozipata ni pamoja na:
1. Wakala humsaidia mteja kuhusu mchakato mzima wa ukataji tiketi au ku-book hoteli kabla, wakati na baada ya safari/likizo husika. Hapa ni pamoja na kumsaidia kuahirisha safari wakati wa dharura, kumshauri na kumsisitiza kuhusu muda wa safari, ratiba za safari na taratibu nyingine zote ambazo mara nyingi abiria hujisahau na kujikuta wanapata hasara au wanaharibu ratiba zao.
2. Wakala humsaidia mteja kuchagua ndege au hoteli bora kulingana na bajeti yake. Mara nyingi hutokea abiria kulazimika kulipa gharama za ziada tofauti na bajeti yake ya awali pale anapofanya booking moja kwa moja bila kujua kama kuna options nyingine. Faida hii anaipata kwa wakala pekee.
3. Wakala humpa ushauri wa kweli (honest) mteja kuhusu sehemu ambazo anaweza kwenda kufurahia huduma kwa gharama rafiki kupitia machaguo ambayo wakala anayo kwenye orodha yake.
4. Uhusiano baina ya Wakala na Mashirika au Hoteli mbalimbali hurahisisha kupewa kipaumbele anapofanya booking. Hii ni kutokana na kufanya nayo kazi mara kwa mara. Ni rahisi zaidi kwa wakala kuwasiliana moja kwa moja na watoa huduma kama kuna mapendekezo anayotaka kufanyiwa kwa niaba ya mteja.
5. Wakala humpatia namba ya simu mteja ambayo watakuwa wakipigiana simu muda wowote ikiwa kuna kitu mteja anahitaji. Hilo mteja hawezi kulipata kutoka kwenye tovuti za booking au kampuni husika.
Na mengine mengi tu.
Kuhusu hofu ya gharama; mara nyingi kama sio zote mteja hulipia gharama ile ile ambayo angechajiwa na shirika la ndege/hoteli au pengine chini yake kutokana na mapendekezo ya Wakala au "ofa" ambazo wakala anapatiwa na mashirika/hoteli hayo.
Hizo ni faida na ushauri wa kitaalamu ambao tumeona tuwapatie kutokana na uzoefu tulionao kwenye industry hii. Sio shurti kufanya hivyo. Mwisho wa siku muamuzi wa mwisho ni mtu mwenyewe.
Karibuni kwa maoni na maswali kama yapo turahisishe maisha!