Electrical Engineers kujadili tatizo la Umeme

Nikupateje

JF-Expert Member
Dec 22, 2009
1,334
988
Wataalamu wa umeme nchini (Electical Engineers), na wadau wengine watakutana kujadili ufumbuzi wa kitaalamu wa matatizo ya umeme nchini.

Barua ya mwaliko huo inasambaa kwenye internet na mimi nimeipata kuiweka humu inaonyesha kwamba kikao hicho kitafanyika kwenye ukumbbi wa Karimjee Hall, siku ya Jumamosi, July 30, 2011 kuanzia saa 04:00 hadi saa 06:00 mchana.

Barua inaonyesha kikao hicho kinaratibiwa na Taasisi ya Wahandisi hapa nchini yaani Institute of Engineers Tanzania.

Watoa mada watakuwa ni Dr. Maingu, Dr. Kyaruzi na Eng. Mgaya.

Dr. Kyaruzi ni yule aliyemaliza hoja ya kitaalamu kwamba umeme unaopita juu ya Kanisa la Kakobe hauna madhara.

Hivyo wale wenye kutaka kujua wataalamu wa umeme wanasema nini kuhusu hali ya sasa hii ni fursa yao.

*****
Barua ya mwaliko inasema hivi hapa chini na vilevile unaweza kui-download kwenye attachment:
*****
View attachment ADVERT - MATATIZO YA UMEME.doc
*****



THE INSTITUTION OF ENGINEERS TANZANIA


MKUTANO WA KUJADILI TATIZO LA UMEME NCHINI TANZANIA:


MAHALI: KARIMJEE HALL

SIKU/TAREHE: JUMAMOSI, 30/07/2011

MUDA: SAA 4 ASUBUHI – SAA 6 MCHANA


MADA: UFUMBUZI WA KIHANDISI WA KUTATUA TATIZO LA UMEME NCHINI TANZANIA


WATOA MADA: (1) ENG. DR. M.I. MAINGU
(2) ENG. S. M. MGAYA
(3) ENG. DR. A. L. KYARUZI


WADAU NA WANANCHI MNAKARIBISHWA


RAIS
21/07/2011
*******
Maswali zaidi wasiliana na anuani ifuatayo:

*****
Eng. S.N.A. Kassera
Executive Secretary,
The Institution of Engineers Tanzania,
Pamba Road, Opp. Former Hotel Agig
P.O. Box 2938,Dar es Salaam, Tanzania,
Tel: +255 22 2124265/2122836,
Mob: +255 717 110411/0784 909060,

*****
 
Msisahau kumkaribisha Engineer, Ambassador, M.P, Dr., Rev. Prof. Captain Rwegasira Esq.
Mlikuwa wapi nyie mainjinia siku zote? Hili tatizo limeanza toka 1990's?
Hata mkiweka huo mkutano na mkija na hoja zenu za kutatua hili tatizo, can't you see ni yaleyale kama mapendekezo ya tume ya Warioba na majina ya wauza madawa kapelekewa report raisi na kaziweka reports kwenye kabati?
Ni vema mkafanya huo mkutano wenu but I think it's a waste of time and resources sababu JK ameshasema eti tatizo la umeme ni ukame na yeye hana uweza wa kuleta mvua. Solution ameshanena kuwa ni hadi mvua zinyeshe. Msipoteze muda wenu labda mkutane tu for a get together
 
Wanaokutana ni Members wa Institute of Engineers Tanzania siyo Electrical engineers kwa mujibu wa vyanzo vyangu vya habari.

By the way ina maana wizara ya Nishati haina Electricla Engineers? Ahaa usanii huu alafu Karimjee!
 
msisahau kutupa feedback..., alafu please tumeongea sana sisitizeni action sababu kama ni kuongea walishaonge, tumeongea na wataendelea kuongea sana...
 
Wataalamu wa umeme nchini (Electical Engineers), na wengine wa fani hiyo wameitisha kikao kujadili ufumbuzi wa kitaalamu wa matatizo ya umeme nchini.

Barua ya mwaliko huo inasambaa kwenye internet na mimi nimeipata kuiweka humu inaonyesha kwamba kikao hicho kitafanyika kwenye ukumbbi wa Karimjee Hall, siku ya Jumamosi, July 30, 2011 kuanzia saa 04:00 hadi saa 06:00 mchana.

Barua inaonyesha kikao hicho kinaratibiwa na Taasisi ya Wahandisi hapa nchini yaani Institute of Engineers Tanzania.

Watoa mada watakuwa ni Dr. Maingu, Dr. Kyaruzi na Eng. Mgaya.

Dr. Kyaruzi ni yule aliyemaliza hoja ya kitaalamu kwamba umeme unaopita juu ya Kanisa la Kakobe hauna madhara.

Hivyo wale wenye kutaka kujua wataalamu wa umeme wanasema nini kuhusu hali ya sasa hii ni fursa yao.

*****
Barua ya mwaliko inasema hivi hapa chini na vilevile unaweza kui-download kwenye attachment:
*****
View attachment 34395
*****



THE INSTITUTION OF ENGINEERS TANZANIA


MKUTANO WA KUJADILI TATIZO LA UMEME NCHINI TANZANIA:


MAHALI: KARIMJEE HALL

SIKU/TAREHE: JUMAMOSI, 30/07/2011

MUDA: SAA 4 ASUBUHI – SAA 6 MCHANA


MADA: UFUMBUZI WA KIHANDISI WA KUTATUA TATIZO LA UMEME NCHINI TANZANIA


WATOA MADA: (1) ENG. DR. M.I. MAINGU
(2) ENG. S. M. MGAYA
(3) ENG. DR. A. L. KYARUZI


WADAU NA WANANCHI MNAKARIBISHWA


RAIS
21/07/2011
*******
Maswali zaidi wasiliana na anuani ifuatayo:

*****
Eng. S.N.A. Kassera
Executive Secretary,
The Institution of Engineers Tanzania,
Pamba Road, Opp. Former Hotel Agig
P.O. Box 2938,Dar es Salaam, Tanzania,
Tel: +255 22 2124265/2122836,
Mob: +255 717 110411/0784 909060,

*****
Academic and technical solutions of electricity are well known but at the moment we need political solution. Makongamano na midahalo ya nini? Kipya gani ambacho watazungumza hawa watu?
 
Wanaokutana ni Members wa Institute of Engineers Tanzania siyo Electrical engineers kwa mujibu wa vyanzo vyangu vya habari.

By the way ina maana wizara ya Nishati haina Electricla Engineers? Ahaa usanii huu alafu Karimjee!

Sorry mkuu,

Ni kweli mwaliko ni kwa ma-engineer japo kwa tatizo la umeme na haraka ya ku-post nikajikuta nakazia Electrical Engineers japo pia niliongezea neno na wengine wa fani hiyo.

Lakini kila kitu kingine kinabaki kama barua ilivyo.

Suala kwamba WIzara haina ma-engineer hilo ni juu yao. Kama na wenyewe watakuwepo mkutanoni basi itajulikana kwa nini kuna matatizo na wao wamo humo wizarani.

Suala ni kwamba hata usiwe engineer naamini unaweza kutoa na kusikia aoni yako. Vinginevyo hata hapa JF matatizo ya umeme yangekuwa anaongelewa na hao wa wizarani tu amba kila siku wanataja hesabu za Megawati.
 
Wataalamu wa umeme nchini (Electical Engineers), na wadau wengine watakutana kujadili ufumbuzi wa kitaalamu wa matatizo ya umeme nchini.Barua ya mwaliko huo inasambaa kwenye internet na mimi nimeipata kuiweka humu inaonyesha kwamba kikao hicho kitafanyika kwenye ukumbbi wa Karimjee Hall, siku ya Jumamosi, July 30, 2011 kuanzia saa 04:00 hadi saa 06:00 mchana.Barua inaonyesha kikao hicho kinaratibiwa na Taasisi ya Wahandisi hapa nchini yaani Institute of Engineers Tanzania.Watoa mada watakuwa ni Dr. Maingu, Dr. Kyaruzi na Eng. Mgaya.Dr. Kyaruzi ni yule aliyemaliza hoja ya kitaalamu kwamba umeme unaopita juu ya Kanisa la Kakobe hauna madhara.Hivyo wale wenye kutaka kujua wataalamu wa umeme wanasema nini kuhusu hali ya sasa hii ni fursa yao.*****Barua ya mwaliko inasema hivi hapa chini na vilevile unaweza kui-download kwenye attachment:*****View attachment 34395*****THE INSTITUTION OF ENGINEERS TANZANIAMKUTANO WA KUJADILI TATIZO LA UMEME NCHINI TANZANIA:MAHALI: KARIMJEE HALLSIKU/TAREHE: JUMAMOSI, 30/07/2011MUDA: SAA 4 ASUBUHI – SAA 6 MCHANAMADA: UFUMBUZI WA KIHANDISI WA KUTATUA TATIZO LA UMEME NCHINI TANZANIAWATOA MADA: (1) ENG. DR. M.I. MAINGU(2) ENG. S. M. MGAYA(3) ENG. DR. A. L. KYARUZIWADAU NA WANANCHI MNAKARIBISHWARAIS21/07/2011*******Maswali zaidi wasiliana na anuani ifuatayo:*****Eng. S.N.A. KasseraExecutive Secretary,The Institution of Engineers Tanzania,Pamba Road, Opp. Former Hotel AgigP.O. Box 2938,Dar es Salaam, Tanzania,Tel: +255 22 2124265/2122836,Mob: +255 717 110411/0784 909060,*****
Nashukuru kwa taarifa kiongozi!!
 
Msiwasahau wachumi tu kwani malengo hayatafikiwa. Engineers watatoa utaalamu wao wa kiufundi ila utaalamu wa kimipango ni kazi ya wachumi.
 
Na wiki 3 za Ngeleja ndo zinakaribia kwisha...!!ngoja tuone, Engg Nsiande nadhani atakuwepo!!
 
Msisahau kumkaribisha Engineer, Ambassador, M.P, Dr., Rev. Prof. Captain Rwegasira Esq.
Mlikuwa wapi nyie mainjinia siku zote? Hili tatizo limeanza toka 1990's?
Hata mkiweka huo mkutano na mkija na hoja zenu za kutatua hili tatizo, can't you see ni yaleyale kama mapendekezo ya tume ya Warioba na majina ya wauza madawa kapelekewa report raisi na kaziweka reports kwenye kabati?
Ni vema mkafanya huo mkutano wenu but I think it's a waste of time and resources sababu JK ameshasema eti tatizo la umeme ni ukame na yeye hana uweza wa kuleta mvua. Solution ameshanena kuwa ni hadi mvua zinyeshe. Msipoteze muda wenu labda mkutane tu for a get together

Ikiwa ni hivyo basi hata thread unazojadili hapa JF zifutwe kwa sababu JF hardly imeanza mwaka 2005 na matatizo kibao ya nchi hii yalikuwepo.

Je, ulipitia ile thread kwamba ilikuwa ni makosa kuweka 80MW pale Mtera? Je, unajua kwa nini ilikuwa ni makosa?
Ilikuwa ni makosa kwa sababu MasterPlan ya Mtera haikuwa kuzalisha umeme. Mtera iliwekwa kwa ajili ya kuisaidia Kidatu inapozidiwa, kwamba maji yakikauka Kidatu basi yaweze kuletwa yalioko Mtera.

Sijui ni nini kiliingia vichwani na kufanya pale Mtera waweke 80MW na iwe ni ile inayojitegemea.

HIvyo Mtera ilikuwa kama standby source. Sasa tume-utilize hadi standby na matatizo yenyewe ndiyo haya.

Wewe kwa upeo wako hulioni hilo na hutaki lijadiliwe.

Waache wajadili kama mnavyojadili humu JF.
 
Mbona sioni mtu kutoka wizarani au tanesco kama watoa mada
Jamani ni aibu hii,mhando ni engineer si aje tupa master plan yao tuidiscuss
 
Hawa wahandisi wa Kiafrika hawana lolote. Watakutana hapo na kunywa maji yao ya Kilimanjaro na tuvitafunio twao (vibajia, sambusa, ufuta, kashata, kachori, n.k.). Halafu watataoka hapo na makabrasha kibao. Hamna lolote la maana watakaloliongelea. Mgao utaendelea kuwepo. Na rhumba litazidi kuwa kali. Ndiyo wahandisi wa Kiafrika hao. Ingenuity sufuri kabisa. Miaka yote hii ya matatizo ya umeme leo ndiyo wanagutuka? Get outta here...
 
Mbona mimi Eng. Ngabu sijapata huu mwaliko?

Kwakuwa si member wa IET ama vinginevyo masuala ya umeme huyafahamu kwahiyo hawakuona umuhimu wako, ama vinginevyo hauko kwenye mtandao wao!!
Hapana shaka eng.stella manyanya atakuwepo kuwakilisha,...

Msisahau kumkaribisha Engineer, Ambassador, M.P, Dr., Rev. Prof. Captain Rwegasira Esq.
Mlikuwa wapi nyie mainjinia siku zote? Hili tatizo limeanza toka 1990's?
Hata mkiweka huo mkutano na mkija na hoja zenu za kutatua hili tatizo, can't you see ni yaleyale kama mapendekezo ya tume ya Warioba na majina ya wauza madawa kapelekewa report raisi na kaziweka reports kwenye kabati?
Ni vema mkafanya huo mkutano wenu but I think it's a waste of time and resources sababu JK ameshasema eti tatizo la umeme ni ukame na yeye hana uweza wa kuleta mvua. Solution ameshanena kuwa ni hadi mvua zinyeshe. Msipoteze muda wenu labda mkutane tu for a get together

Waswahili wana kamsemo kao kwamba "better late than never" kwahiyo waache wahandisi wakutane kisha tusikie watasema nini.

Wanaokutana ni Members wa Institute of Engineers Tanzania siyo Electrical engineers kwa mujibu wa vyanzo vyangu vya habari.

By the way ina maana wizara ya Nishati haina Electricla Engineers? Ahaa usanii huu alafu Karimjee!


Wapo ma engineer wa kutosha kabisa pale wizarani; kuanzia kwa naibu katibu mkuu eng.mwihava, eng.mushi, eng.kitonga kwa kutaja wachache wakiongozwa na ma profesa wao Dr. eng.ngeleja na Dr.eng.malima

Academic and technical solutions of electricity are well known but at the moment we need political solution. Makongamano na midahalo ya nini? Kipya gani ambacho watazungumza hawa watu?

Inabidin wakutane si unajua tena mambo ya sitting allowance mkuu, bila hivyo hiyo mil 460 iliyochangishwa na jairo itakosa justification!! Matatizo ya umeme ndani ya nchi hii hayawezi kumalizika kama ccm itaendelea kuiongoza nchi hii, iwe wameshinda kwa halali ama kwa haramu. Sasahivi wanatumia pesa nyingi kwa mamilioni kugawana posho kwa kisingizio cha kusherekea uhuru wakati nchi iko gizani, aibu kiasi gani kwa watanzania!!??

Msiwasahau wachumi tu kwani malengo hayatafikiwa. Engineers watatoa utaalamu wao wa kiufundi ila utaalamu wa kimipango ni kazi ya wachumi.

Wachumi wetu hawa hawa wanaotuhubiria kwamba uchumi wa nchi unakuwa kwa kiwango cha juu wakati mifukoni hatuna hata senti ya kununua maandazi?? Labda tupate wachumi wa kichina, hawa watanzania hawafai kabisa, hovyooooo!!!

Ikiwa ni hivyo basi hata thread unazojadili hapa JF zifutwe kwa sababu JF hardly imeanza mwaka 2005 na matatizo kibao ya nchi hii yalikuwepo.

Je, ulipitia ile thread kwamba ilikuwa ni makosa kuweka 80MW pale Mtera? Je, unajua kwa nini ilikuwa ni makosa?
Ilikuwa ni makosa kwa sababu MasterPlan ya Mtera haikuwa kuzalisha umeme. Mtera iliwekwa kwa ajili ya kuisaidia Kidatu inapozidiwa, kwamba maji yakikauka Kidatu basi yaweze kuletwa yalioko Mtera.

Sijui ni nini kiliingia vichwani na kufanya pale Mtera waweke 80MW na iwe ni ile inayojitegemea.

HIvyo Mtera ilikuwa kama standby source. Sasa tume-utilize hadi standby na matatizo yenyewe ndiyo haya.

Wewe kwa upeo wako hulioni hilo na hutaki lijadiliwe.

Waache wajadili kama mnavyojadili humu JF.

Punguza jabza mkuu, kila mmoja ana uhuru wa kutoa mawazo yake na hayo ndio mawazo yake kama na wewe unavyotoa yakwako.
Mwisho wa siku tutaangalia hoja ya msingi imetoka wapi na ni ipi kwa utekelezaji na manufaa ya wananchi.
 
Mbona sioni mtu kutoka wizarani au tanesco kama watoa mada
Jamani ni aibu hii,mhando ni engineer si aje tupa master plan yao tuidiscuss

mhando anauza umeme kwa hasara, ananunua umeme kwa bei ghali toka kwa songas na wengineo lakini anatuuzia kwa bei poa, ukichanganya na vishoka mitaani plus umeme unaopotea kutokana na uchakavu wa miundombinu, sidhani kama atathubutu kuwa msemaji siku hiyo, sana sana atakuja kama msikilizaji!!

Hawa wahandisi wa Kiafrika hawana lolote. Watakutana hapo na kunywa maji yao ya Kilimanjaro na tuvitafunio twao (vibajia, sambusa, ufuta, kashata, kachori, n.k.). Halafu watataoka hapo na makabrasha kibao. Hamna lolote la maana watakaloliongelea. Mgao utaendelea kuwepo. Na rhumba litazidi kuwa kali. Ndiyo wahandisi wa Kiafrika hao. Ingenuity sufuri kabisa. Miaka yote hii ya matatizo ya umeme leo ndiyo wanagutuka? Get outta here...

wanataka kuuza sura tu kwenye mikamera ili jioni yake tuwaone na tukiamka tukute wamejazana kurasa za mbele za magazeti.
 
haya mambo yanaendeshwa kisiasa jmani,labda washauri tu na ushauri wenye nchi wataweka kabatini
 
msisahau kutupa feedback..., alafu please tumeongea sana sisitizeni action sababu kama ni kuongea walishaonge, tumeongea na wataendelea kuongea sana...
hata wakitoa mapendekezo mazuri vp,serikali kiburi ya magamba itayaweka makabatini.nahis kichwa kupasuka nikiwafikiria politicians njaa wa nchi hii
 
Wakaongee na kujadiliana na maamuzi yafnywe kwa vitendo....Kenya wametengeneza mradi wa umeme kwa miaka 3....Uganda wanatengeneza bwana lingine la umeme.....hku kwetu watu wamekazania posho za vikao tu....na ufisadi
 
Kikubwa ni kwamba wameamua kukutana waziwazi na si kwa kujificha kama humu ambamo hata majina hatujuani.

Jambo lenyewe professionally ni rahisi sana. Peleka swali kwenye University yoyote duniani halafu uliza kifanyike nini kuondoa tatizo la umeme kwenye nchi yenye tatizo kama letu.

Sidhani kama hiyo thesis yako utataja jamaa anaitwa Kikwete, Pinda au Ngeleja.

Ukifanya hivyo nadhani huo Supervisor itabidi akupe negative max ili hata zeo usiipate! Umeambiwa kwamba kwa utaalamu tuliokufundisha kama engineer lete soultion halafu unatutajia majina ya wanasiasa!

Ni utoto kuanza kuwaza kwamba watapuuza kwani anayefikiri hivyo basi huenda ni mtoto wa juzi ambaye hajui kuwa hata mwanzilishi wa CCM yaani Nyerere ilifika mahala wakampuuza akiwa hai!
 
Back
Top Bottom