Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,933
Hii sredi imenifungua sasa. Nimegundua changamoto zifuatazo:
1. Kuna matatizo ya kiufundi na elimu duni kwa watumiaji -Nadhani hoja ya msingi hapa iwe ni kuboresha na kuimarisha utoaji elimu, maana hakuna teknolojia isiyokuwa na changamoto zake
2. Kuna tatizo la gharama za mashine kwa kuwa TRA imetoa exclusive rights kwa wakala maalum. Pengine dhamira ya hili inaweza kuwa ni nzuri (kudhibiti uchakachuzi) lakini hili linahitaji kuangaliwa upya. Udhibiti wa bei ni jambo la msingi.
3. Inaonekana mashine hizi zinawabana wafanya biashara kutokwepa kodi. Kama tatizo ni kwamba kodi imekuwa kali nadhani ni bora waweke bayana, badala ya kupindisha hoja. Maana kukwepa kodi si jambo la kizalendo hata kidogo!.
Najaribu kutafakari ukubwa wa laki saba (mara moja kwa miaka) kwa hawa wafanyabiashara wa Kariakoo..
Waungwana tulipe kodi tujenge nchi. Hao wanaoibomoa kwa kutafuna kodi zetu dawa yao ipo jikoni!
$99.99 EachEach[h=1]Sharp XE-A107 Business Cash Register[/h]Item: 117579 Model: XE-A107
- 8 Pre-Programmed Departments - Easily separate product types
- 80 Price Look-ups - For fast print speed and quiet operation
- Clear Removeable Keytops - convenient and easy-to-clean
Cash Register huanzia na bei ya $ 99.00. Za bai mbaya ni zile zinazotumika kwa malipo pia ya electronic money transfer kama bank card, credit card, zinazotumika kwenye vituo vya mafuta ambazo zimeunganishwa na control ya pump za mafuta, nk ambazo huanzia na bei ya $250 and up.
Hizi walizoleta TRA hakuna tofauti na calculator zitumikazo kwa wanafunzi katika masomo ya sayansi, ingekuwa labda $50 hivi na bei halali isingezidi laki moja na nusu. Kinachoendelea ni wizi mtupu na pengine ni miradi ya vizito kuwanyonya wafanya biashara.