Edward Lowassa special thread

Edward Lowassa special thread

Baada ya hasimu wake wa kisiasa kupenyeza 5 ni wazi kuwa huyu ndie next president..tutarajie kushuhudia lowasa nae akipelekwa segedansi.
 
Ni kweli kabisa mkuu, haya ndio yashatokea watu wajipange waanze maisha ya kukubaliana na hali halisi. Maana si kila unaloliota au liwaza lazima litimie, nyingine ni ndoto tu ambazo huja na kufutika. Sioni sababu ya kuwekeana chuki na visasi, maana nafasi yenyewe ni moja na wagombea 38 hivyo ni lazima wengine wakatwe ili apatikane huyo mmoja. Maana huwezi sema mimi ni zaidi ya yule, kila mtu ana nafasi sawa na hayo ndio matokei. Walioshindwa walende maendelea kwa namna nyingine sio lazima iwe Ikulu.
 
Kama ningekua ni mimi ningemsamehe tu maana hii torture ya kisaikolojia anayokutana nayo ni sawa na adhabu ya kifungo cha maisha jela
 

PASCO amdjishushia hadhi yake kama Kingunge,alitumia kipaji na akili nyingi kutaka kuwaaminisha wanajamvi khs mafuriko ya fisadi Lowassa,wamemfananisha na Yesu, wengine wakamfananisha na Mtume Muhammad lakini Mungu wetu mwema amejibu,nasubiri kumsikia The President
 
Last edited by a moderator:
Hii nchi bwana. Sasa hao vilaza watalipeleka wapi taifa wakipewa idhini and watz!?
 
Kumnyofoa Mamvi sawa ha ilikuwa lazima lol Ila hili la waliobaki mm sioni mwanga SISIEMU wanakoelekea, another KANU on the making
 
Mhs Mbunge Hamisi Kigwangwala roho kwatu, nadhani ametulia sasa, maana Bashe ataingia mitini!!
Tanzania hoeeeeeeeeeeee!!
Lowasa ziiiiiiiiii!!
 
Membe na Lowasa ilitakiwa wafutwe kabisa kwenye mzunguko wa kwanza. Kikwete na familia yake wana mkono katika hili jambo na hakuna asiyeliona.
Kwa kweli ilibidi wote wawili Membe na Lowasa watolewe kwani toka mwanzo kulikuwa na dalili ya uadui kimkakati.
 
Kumtoa kwenu lowasa mmfanya vema ukawa tuwamalize kabisa maana jamaa aliwabeba hadi ukawa yule
 
Taarifa kwamba Ngoyai kakatwa umezipata wapi.Au unamuandaa kisaikolojia kwa lolote.Tusubiri saa nne na nusu leo kwa taarifa kamilli.
Maamuzi yameshatolewa ndo hayo kubaliana nayo tu hata kama hukujiandaa kisaikolojia. Japo ulijiapiza kuwa huwezi kukatwa kwa vile eti upo CCM tangu kuanzishwa kwake lakini ndo hivyo tena yamekuwa hata wenzako pia walikuwemo vile vile.

Ulizua misemo mingi kipindi hiki kama vile HAKATWI MTU, PATACHIMBIKA, HUWEZI KUZUIA MAFURIKO, yote hiyo ilikuwa ni mikwara yako ambayo labda kwa namna moja ama nyingine imekuponza kwa vile ulikuwa kama unaitishia CCM na ngazi zote za juu za maamuzi na uteuzi.

Najua imekuuma sana kutokana na jinsi ulivyokuwa umeikamia nafasi hiyo ya juu kabisa kitaifa lakini kumbuka asiyekubali kushindwa si mshindani. Siasa ndo zilivyo hata wewe unazijua.

Kwa heri mzee wa safari ya matumaini amini tu kuwa umeshakatwa na hakuna rufaa.
Pole sana pia wapambe na wafuasi wake wote.

Bado unayo nafasi ya kuondoa umasikini katika nchi kwa vile ulisema unakerwa nao.

Ni mimi mpiga kura wa kawaida nisiyefungamana na chama chochote. Nasubiri October nimkate mmojawapo kati ya CCM au UKAWA.
 
Kumuondoa Lowasa na Kumwacha Membe imetoa Tafrisi mbaya kwa Mkulu WA Kaya
Ubaguzi wa kiukanda walishatamka RAIS hatatoka KASKAZIN.tatizo la Lowasa ni wa kaskazini.membe ni jirani tena nasikia ni familia ya mwenyekiti.
 
Back
Top Bottom