Edward Lowassa special thread

Edward Lowassa special thread

Lowasa akihamia ukawa na kupewa nafasi ya kuugombea urais tugomeni wote wana ukawa kufanya uchaguzi
 
MIMI NI MWL IDARA MSINGI NIPO GAIRO KWA ALIYE MVOMERO NA ANATAKA KUJA GAIRO TUWASILIANE 0687435031 au 0767201359
 
Mkuu,
Angalizo lako linaweza kuwa ni kweli hasa ikichukuliwa Rais Kikwete ni kiongozi asiyeeleweka katika misimimo mingi.

Rais Kikwete hupenda kusema ''akili ya kuambiwa changanya naya kwako''.

Kuna kitua ambacho hatukifahamu lakini ninachofahamu Lowassa hawezi kuondoka CCM kama bado anaamini CCM bado inachagulika katika kiti cha Urais wa Tanzania.

...Lowasa atabakia CCM ili kuhakikisha anakiua chama from within na si kwa sababu nyingine yoyote. hakuna Masai anayependa na kukubali kudhalilishwa na mtu awaye yote!

hapa CCM mnalo!
 
Wanajukwaa!!!
Macho na masikio ya watanzania walio wengi yameelekezwa Dodoma ambapo CCM, Chama kikubwa na kikongwe kabisa hapa nchini na Afrika kwa ujumla kipo katika mchakato wa kumpata mtu wa kupeperusha bendera katika kumrithi Mhe Jakaya Kikwete.

Chambuzi nyingi za siasa kuelekea Magogoni 2015 zimekuwa zikiangaza nani atapitishwa na Chama, uimara wake na udhaifu wake.

Wapo wanaochambua kwa mapenzi, chuki, kutokujua na wengine kwa utaalamu wa hali ya juu.

Mimi kama mchambuzi wa siasa hesabu zangu zinanielekeza kuwa Mhe Edward Lowassa ana nafasi kubwa ya kuibuka mshindi akiwa ndani ya CCM na hata akiwa nje ya CCM.

Matokeo ya uchambuzi wangu hadi kufikia hitimisho kuwa Lowassa ana nafasi kubwa ni baada ya tafakuri ya kina ya mwenendo wa kisiasa tangu mwaka 2005 hadi sasa.

Mwaka 2005, Mhe Kikwete wa CCM alipata zaidi ya 80% ya kura zote na hivyo kuonesha namna gani wananchi walivyokuwa na kiu na imani kubwa kwa Kikwete binafsi na hata CCM kwa ujumla.

Miaka mitano (05) baadaye Mhe Kikwete aliporomoka kwa karibu 20% na hivyo kuambulia kura 5,276,827 sasa na 61.17% ya kura zote. Wapinzani kwa upande wao tunaona Chadema walipata kura 2,271,941; CUF kura 695,667 na NCCR kura 26,388 (hawa ndio UKAWA)

Sasa, tuangalie hesabu za Sayansi ya Siasa vipi zinambeba Lowassa ikiwa atakatwa jina lake na kuamua kuhamia katika mwamvuli wa UKAWA na wenye UKAWA wakampokea??

Kwanza, wakati wakiwa katika zoezi la kutafuta wadhamini Lowassa alijipatia jumla ya wadhamini 874,297 ambao tunaamini kuwa wapo tayari kumpigia kura popote atakapokuwa. Na iwapo kila mdhamini atashawishi watu watatu (03) ni kwamba Lowassa atakuwa na mtaji wa watu 2,532,891.

Sasa (wadhamini x 3)+(mtaji wa UKAWA 2010) =Kura kibindoni

2,532,297 + 2,993,996 = 5,526,293

Kwa hiyo, kama ataingia na mtaji huo katika uchaguzi mkuu atakuwa amebakiza kazi ndogo tu ya kushawishi undecided group na kwa kuzingatia kundi kubwa la vijana ambao hawakuweza kupiga kura 2010 kutokana na kuwa na umri chini ya miaka 18, ambao hakuna ubishi kuwa wengi ni wafuasi wa vyama vya upinzani na hivyo watampa kura mgombea wa Upinzani, ni dhahiri kuwa Lowassa ana nafasi kubwa ya kushinda ikiwa atagombea kupitia CCM au atapitia Muungano wa UKAWA.

Hizo ni hesabu zangu nikiwa mchambuzi huru.

Ni mwaka wa Ukawa toa hapa ccm kama KANU. Kenya wameweza why not us.
 
Kwa wale wasoma maandiko ni matumaini yangu haya maandiko sio mageni, ni mlio wa sauti ya mwisho kabla ya kukuta roho, Hakika CCM inakata roho pale tu watakapo mkata huyu ndugu Lowassa, nadhani waliosema sikio la kufa halisikii dawa hawakukosea, waliosema aonywae mara nyingi na kushupaza shingo ......, lakini adharauie mwiba mguu huota tende.

Wahenga wetu hutuonya pasipo kukoma siku zote, yumkini hatusikii lakini katika hili CCM wenzangu tunaenda vibaya, nani anataka kumchagua JAJI AGUSTINO na wakati tunajua kabisa kanisa lake ambalo naye ni kiongozi wameshakubali ushoga, tunataka kiongozi atakaye tuvukisha salama wakati huu wa USHOGA ambao unaonekana kuwa agenda kuu ya dunia, kiongozi mwenye maamuzi sahihi na magumu.

Hatutaki kiongozi atakaye lia lia wakati anatakiwa kuwajibika, wala hatutaki kiongozi atakaye kuwa anahonga wanafunzi nyumba za uma kwa kubadilishana na mapenzi, hatutaki kiongozi ambaye atasafiria nyota ya marehemu baba yake ili hali hata ubunge wa nyumbani hana.

Mwaka 2015 ni ama LOWASSA au DR SLAA, kupanga ni kuchagua na ndio tumeshapanga,
 
Hesabu zingine hizi hapa:-

Lowassa,Lowassa hadi kero Kila kukicha Lowassa, Lowassa, oooo mtu mawazo yake binafsi tu anakuja na kusema ametumwa na wanainchi katika eneo lake mfano mkoa au kanda amshauri lowassa agombee Urais.

Lowassa jamani hafai, mtu anayejitajirisha kwa kutumia wadhifa wake katika utumishi wa umma hafai kuwa kiongozi kwa sababu siyo mfano wa kuigwa, yaani kuiba mali za umma siyo sifa ambayo inafaa mtu mwingine aige.

Lowassa kuwa kiongozi wa ofisi ya juu kutavutia wezi wenzie kuinajisi ofisi hiyo, yaani kama ukifuga fisi tegemea fisi wenzie kumtembelea fisi mwenzao hawezi kutembelewa na swala.Jamani Lowassa hafaiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.

Kikwete, Mangula hebu mwambieni huyo mtu kwamba hana sifa za kiti cha urais, anaweza mambo mengine na siyo urais, ni nyie mnamlealea mnamchelewesha mpeni makavu ya moja kwa moja na wala siyo mafumbo mafumbo

CC. 1. Jajaya Mrisho Kikwete
2. Jack Zoka
3. Philip Mangula
4. Abdrahiman Kinana
5. Benjamin Mkapa- Uliwakemea maaskofu ukasema na majoho yao haiwezekani serikali tatu kwa sababu baba wa taifa alikataza mbona Lowassa humkemei? Mnafiki mkubwa wee.
6. Ali Hassan Mwinyi
7. Nape Nnawiye
8. Delvis Adolf Mwamunyange
9. Ernest Hamis Mangu
10. John Komba-na unafiki wako, kama Lulu Michael kakukomba mali zote usitegemee uibukie katika kumpigia dabe fisadi Lowassa, kufa na lywako
11. Rostam Azizi –ikulu siyo pango la walanguzi unatumia mapesa yako ya wizi ili umweke Lowasaa ikulu ili uwe ndio uchochoro wako

Rostam anakuhusu nini kaiba una ushahidi? acheni kuingizia watu wasiowahusu humu pumbavu mkubwa
 
"........nawaomba maaskofu wote,masheikh wote,na vijana wote.......wanaotaka fedha za haraka haraka........wamfuate EDWARD NGOYAI LOWASA atawapatia! Lakini hana sifa ya kuwa RAIS.............." -Dc Makonda.

1,sifa hana 2.hawezi kuwa mwenyekiti wa chama kwakuwa katiba ya chama inasema hurusiwi kutoa rushwa wala kupokea rushwa .......asanteni kwa kuniskiliza paul makonda kabla hajawa DC kinondoni
 
Lowassa ndio rais ajaye... anzeni kujiandaa kumpokea Rais wa maendeleo sio longolongo...!!!
 
lowasa akikatwa na cc ya ccm patachimbika by kingunge. nasubiri pachimbike hapo dodoma.
Hizi hoja zinazosema patachimbika asipoteuliwa Edward Lowassa ni dharau kwa Kamati kuu ya CCM!

Mwaka 2012, Mbunge Nimrod Mkono aliwahi kudai hapatatosha kama jina lake litakatwa kwenye ugombea uenyekiti wa Wazazi. Jina lake likakatwa, nini kilitokea...

Prof. Muhongo kwenye sakata la Tegeta Escrow account alidai pia patachimbika. Nini kilitokea baadaye...

Prof. Tibaijuka naye yalitokea yaleyale...
 
Kwa habari zi sizo rasimi M/kiti ameonekana mkingia kifua Edward Lowassa wale waliokuwa wakisema kwa dhiaka juu ya EL nasikia wameufyata!hili hali M/kiti akiwa mbogo kwa kila mtu!
Waliotegemea kumchekea waishia kununa!
 
Kwa habari zi sizo rasimi M/kiti ameonekana mkingia kifua Edward Lowassa wale waliokuwa wakisema kwa dhiaka juu ya EL nasikia wameufyata!hili hali M/kiti akiwa mbogo kwa kila mtu!
Waliotegemea kumchekea waishia kununa!

Akifanya hivyo CCM itamfia, sijui ataficha wapi USO wake
 
Back
Top Bottom