Edward Lowassa on ITV!-Dakika 45 Part II!.


we pasco unavyonikunaaa, we acha tu. Ngoyayi go
 

PASCO,
Ukimya wa EL bungeni una sababu nyingi ila kubwa kuliko zote ni kwamba chochote atakachoongea EL popote pale iwe bungeni, kanisani, kwenye harambee, tv n.k kinapitishwa kwenye 'intensive scrutiny' yaani kinachambuliwa katika angle zote na priority itapewa kwenye angle ambayo wabaya wake wataipenda waitumie kama propaganda ya kumbomoa, si unakumbuka akina mkama walivyomjibu wakati ule alivyoongea bungeni wakamwambia kama ana maoni ayawasilishe kwenye vikao halali vya chama na sio kuongelea bungeni.

NGOYAYI FOREVER
 

welcome bro'
EL ni kiongozi pekee aliyeko CCM ambaye anaweza kusimamia kile anachokiamini bila kuyumbishwa na upepo wa kisiasa.
Unlike huyu Pinda ambaye ni kigeugeu wakati wa Jairo alisema yeye siyo mamlaka ya nidhamu hawezi kumchukulia hatua ila ilipofika kwa Brandina Nyoni (katibu mkuu wizara ya afya) alimsimamisha kazi mara moja. haeleweki pinda ni mnyama au ndege, labda POPO.
 
Akina Nape, Sitta, Mwakyembe,..., wanakuelewa kweli? Nitamshangaa sana JK na CC yake atakayounda mwaka huu wakimwachia mtu huyu akapenya hadi kwenye ballot boxes za 2015. Hebu tuangaze macho na akili zetu nje ya CCM pia.
Historia ya NCHI hii haimpi nafasi Lowasa kuwa Rais wetu ajae. Hakuna WAZIRI MKUU amepata kuwa RAIS isipokuwa Mwalimu pekee.
[/QUOTE]

mkuu tatizo nikuwa nani ndani ya ccm wakumshikia bango Edo, kumbuka jamaa anamtandao mkubwa serikalini kuliko hata dagama, yeye alipokuwa anazurula mwenzake alipanga safu yoote kuanzia usalama wakuu wa mikoa,wilaya na vitongoji! udhaifu wa dhaifu ndo umempa nguvu huyu fisadi!
 
Henge,
Mtandao wa Lowasa serikalini ni kama vile umemalizika sasa baada mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri, maRC na hivi karibuni maDC. Tatizo limebaki BUNGENI tu ambako wakati uchaguzi linavunjwa na kila mbunge kulilia nafsi yake zaidi baada ya hapo.
Kwenye CCM nako huu utaratibu mpya wa kuwapata wajumbe wa NEC toka ngazi ya wilaya nako kumeharibu sana mitandao sugu ya akina Lowasa. Wagombea wa NEC-CCM wametakiwa kikanuni wasiwe wanashikilia nafasi nyingine za kudumu kama UBUNGE.
Sekretarieti ya akina Mukama, Nape, January, Mwigulu,..., nayo haitabiriki na kuingilika kirahisi kama ile ya Mzee Makamba.Nguvu kubwa aloobaki nayo Lowasa na washirika wake ni PESA ambayo watapata taabu sana kuitumia kwa taratibu na kanuni za sasa ndani ya chaguzi za CCM zinazoendelea sasa.
 
Ndugu yangu Lowasa hata ukioga na omo na maji ya jik, ili mradi ww ni wa magamba kwangu ni kazi bure nawajua ninyi na nyinyiemu yenu, ni wataalam wa kuongea km wale wanao aproach wanawake[hasa mke wa mtu] mpaka wanasahau kama wana ndoa zao, halafu wakishatendwa ndiyo wanakumbuka, binafsi mpaka hapa inatosha sidanganyiki tena.
 
Mkuu MGAYI TAWA, karibu, jf, mtu aliyechafuka kwa kujichafua, ndio mwenye jukumu la kujisafisha, lakini mtu aliyechafuliwa tuu na kuonekana mchafu, ule uchafu aliochafuliwa nao ukondolewa, atakayebaki ni msafi na asiye na mawaa!. Subiria safisha safisha ianze, nakuhakikishia atang'aa kama mbalamwezi na kumeremeta kama nyota!.
 
Rais wangu 2015 ni Shamsi Vuai Nahodha kama tutalazimika kuendelea na CCM. Amekuwa WaziriKiongozi SMZ; akawa waziri wa Mambo ya Ndani na sasa ni Waziri wa Ulinzi na JKT. Atapata mtu kama Dr Asha Rose Migiro kumsaidia kama Makamu wa Rais au Waziri wa Mambo ya Nje
 
Anasema Angekuwa Rais angechukua mamia ya wanajeshi apande mahecta ya michikichi tungepata mafuta mengi tungejenga kiwanda Iyo ni mbinu moja na anazo Mia moja

Kaka kusema tuu ni rahisi sana, je sera za chama chake zinasemaje.....? kwasababu hawezi kusimamia maamuzi yake binafsi labda awe mgombea binafsi..............., lakini je ameshatakata ktk tuhuma a richmund?
 
ELK hakubaliani na Kilimo Kwanza, amesema hapingi sera, bali "Elimu Kabla Kilimo Kwanza", elimu ndio msingi wa maendeleo, tuwekeze kwanza katika elimu ndipo tuje kwenye mapinduzi ya kilimo, viwanda etc!.

hapa point nakubaliana naye.....
 
Mkuu Ndahani, hana kiharusi, kule kutetema na uso kuchoka, kunatokana na Black Label!, akiacha kutaacha!.

I let myself believe what you say is the fact....otherwise urais bado ngoma mbichi.
 
Uchambuzi umeeelekezwa kwenye tuhuma za ufisadi ambao kimsingi ni karibu miaka mitano sasa hakuna ambaye ameweza kuleta ushahidi usiokuwa na mashaka juu ya hilo.

Hoja kubwa alizozitoa ni nyingi, mfano Gavana atueleze kunanini mbona inflation haishuki? hili ni la msingi na pengine tungeelekeza uchambuzi wetu huku, tungefaidika zaidi kama taifa. Yako mengi ya kujadili katika hoja zake.

Umefika wakati wa kuacha kujadili hoja kwa mkondo wa chuki na fitina hapa JF.
 
Lowasa akasahau kwamba hata yeye na familia yake wanachangia pakubwa kwenye hii inflation kwa kuhamisha fedha kwenda nje ya nchi! Huyu baba msanii sana.
 

Mkuu Pasco.. Inasemekana tatizo kubwa lililotokea ni baada ya Nyerere kugundua pamoja na Jengo kupangishwa lakini Landlord wake (Lowassa) hakuwa akilipa kodi serikalini..! Anaetaka kuwa Raisi wetu anakwepa kulipa kodi..! Uliwahi kuicikia hii..? Ina ukweli wowote..?
 
Mkuu Hekima Ufunuo, usemayo ni kweli, mwanzo nilipojiunga jf, nilidhania huu kiukweli ni ukumbi wa ma great thinkers, baada ya kudumu humu kwa kipindi kifupi, nikagundua ma great thinkers humu ndani ni wachache sana tena wanahesabika!. Wengi wanajadili kiushabiki zaidi, wengine kwa chuki binafsi na wengine hujadili ki fitna zaidi, zengwe au kimajungu majungu!, badala ya kujadili hoja alizotoa, watu wanaacha kujadili hoja, wanajadili mtu/watu!.
 
Mkuu Soso, hii itakuwa ni kweli, property tax imekuwa introduced juzi juzi tuu, kwani ma landlord wengi unadhani wanalipa kodi?. Tanzania tunapoteza mabilioni ya kodi kwenye capital gains na trasfer za shares, mfano TTCL imegeuka Celtel,imegeuka Zain, sasa imegeuka Aortel, huko kote ni changing hands, kuna kodi kibao ya capital gain imepotea huku tuking'aang'aa macho tuu!. Nyerere alikuwa mjamaa wa kweli na aliumizwa na mapebari na makabaila, kwa taarifa tuu, hao waliopo mnaowadhania ndio wasafi, basi ndio wachafu kunuka hadi uchafu wa EL kuonekana ni cologne, au eu de toilette!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…