Edward Lowassa hatoruhisiwa kugombea Urais!

Edward Lowassa hatoruhisiwa kugombea Urais!

Ni kweli tume inaweza kumzuia lowasa kugombea akiwekewa pingamizi na ccm au hata wanachama wa chadema ambao wanaona wameletewa mtu asiye na maadili kwenye chama chao. Ccm wameeleza kwa nini walikata jina lake! Amekidhi lini viwango baada ya kuenguliwa au ni hizo fedha zake tunazitaka?
 
baada ya lowasa kukatwa ccm nilikuwa nawaza sana jinc ya kumpa kura magufuli ila kwa sasa nawashukuru UKAWA wamenirahishia kazi hata kama UKAWA wakiweka MBWA ntampa kura MBWA TU lakini sio CCM...
 
Nendendeni mkawafanyie CCM umbea mliokuwa mnatufanyia sisi hatusikii hatuelewwi mtaji wa kura ni watu na watu wenyewe ni ndiyo hawa wanaokuja sasa mungu akupe nini usiseme Lowasa tu mseme Lembeli, Bulaya, Ole Medei na wengine kifupi hatutaki ushauri wenu kawashaurini ACT labda watawasikia sisi mtukome tena mkomeke
 
Nendendeni mkawafanyie CCM umbea mliokuwa mnatufanyia sisi hatusikii hatuelewwi mtaji wa kura ni watu na watu wenyewe ni ndiyo hawa wanaokuja sasa mungu akupe nini usiseme Lowasa tu mseme Lembeli, Bulaya, Ole Medei na wengine kifupi hatutaki ushauri wenu kawashaurini ACT labda watawasikia sisi mtukome tena mkomeke

umenifurahisha sana! ukweli mweupe! kama theluji. upewe nini?.... Likes elfu moja
 
kama tukimkataa Lowasa kwa sababu ni mchafu basi hata akitubu Mungu hatamkubali,hakuna njia nyingine ya kuondoa hawa majambazi madarakani tusipomkubali Lowasa,nawahakikishia ccm itashinda uchaguzi mkuu kama kawaida na itatawala tena miaka kumi na Magufuli atafanya kazi na walewale maana hawana jipya,Lowasa atatusaidia kuiondoa ccm halafu tugeukiane baada ya ccm kuzikwa,hapo ndiyo tutaona njia

kwani Lowasa katubu? tutamsemehe vipi kama haoni makosa yake?
 
Kwa taarifa yako ni mwanachama na mfadhili wa wagombea wa cdm ila sijafurahi lowasa kufanywa mgombea wa ukawa. Kubwa ya sababu ni kuwa viongozi wa Ukawa wamekubali kumpokea mtu ambaye hana maadili na marafiki wake ni wa aina hiyo. Waadilifu wengi tumekata tamaa.


Kuna kundi limeibuka ghafla wakijifanya kuwa na uchungu sana na CHADEMA kumbe ni wanafiki, moyoni wako CCM. Wakati Magufuli anatangazwa kundi hilo hilo liliibuka na kuwashauri CHADEMA wakomae na ubunge. Ujio wa Lowassa umeonyesha rangi za baadhi ya watu. Sasa ni kama wamechanganyikiwa na kujifanya washauri wa CHADEMA.

Mimi nilikuwa mmoja wa watu niliyempinga Lowassa na kumuita mwizi wakati wa mchakato wa kura za maoni CCM ili asipitishwe sababu kubwa niliona upepo wake ulikumba hata wasiokuwemo. Nilijua wakimpitisha tu wapenda mageuzi tumekwisha kwani upepo wake ungepiga hadi kwenye majimbo ya upinzani, na badala ya kuongezeka yangepungua. Kuna wabunge wengi wa CCM walitegemea sana upepo wa Lowassa uwapitie. Sasa hivi wamechanganyikiwa wanaomba bora wangejitoa CCM mapema kabla kura za maoni CHADEMA hazijafanyika.

Ndugu zangu upepo wa wanasiasa ni mbaya sana kuna wabunge CHADEMA upepo wa Dr.Slaa uliwapitia hadi leo hawaamini kama wapo mjengoni. Lowassa upepo wake ni mbaya sana. Dr.Slaa angemsumbua Dr.Magufuli lakini asingemshinda. Vile vile kwenye UKAWA ujio wa Lowassa umeleta mshikamano zaidi. Ninaamini kuna wana CUF na NCCR wasingeweza kumpigia kura Dr.Slaa zaidi ya wabunge wao. Lakini Lowassa ni kama amekuja kuwaunganisha UKAWA. Zitabebwa kura nyingi sana hapa.

Hawo wasiomtaka Lowassa ni wale waliotaka wapinzani wawe wapinzani milele. Ndio wale utawaskia Urais CCM, Ubunge upinzani. Huo ni unafiki mkubwa. Tunahitaji CCM itoke kabisa. Sasa ujio wa Lowassa ni kama umewachanganya sana wamebaki kujifanya wanakishauri chama kumbe wanafki wakubwa. Lengo kuu la chama ni kushika dola kama kuna upenyo umetokea wa kukupeleka huko utumie ipasavyo. Muda ndio huu ukipita CCM itatawala milele.
 
Mimi kinachonishangaza jamani ni hivi; kwanini baada tu ya Mh.ENL kutangaza kuhamia upinzani
kwa kutumia demokrasia na haki yake kisiasa, ghafla wana CCM wameibuka na
kuanza kuibua vioja vya kila aina?
Lowasa mwenyewe ameshasema, aliye na ushahidi wa tuhuma dhidi yake,
aende mahakamani. Zaidi ya hapo,wana ccm acheni porojo! Period!!
 
Najua wanajamvi wengine hawatanielewa,ila nachokisema ni kwamba,lowassa ajiandae kisaikolojia maana mpaka sasa hivi ccm wamekaa kimya wakipanga first eleven,CCM ni bingwa mzoefu,CCM ni watu wa offside,CCM ni watu wa fitina,najaribu kutafakari kwa kina kwamba,Lowassa akitangazwa ameshindwa,je atakubali kushindwa au ndio vurugu zitaanzia hapo?

Je, vurugu hizo zitakuwa na tija kwetu?

Ndio maana nasema Lowassa jiandae kisaikolojia kwani utafungwa kwa gori la offside kwasababu marefarii wasaidizi ni wa kwao na refa wa kati ni wa kwao.siongei kiushabiki maana ushindi hauanzii ndani bali na nje!

Kwa upande wa pili CCM na nyie mjiandae kisaikolojia maana ukawa wanacheza sana na akili za watu na kutafuta majority hivyo endapo wananchi watajitokeza kwa wingi kupiga kura kama walivyojitokeza kujiandikisha basi kuna uwezekano mkubwa UKAWA kushinda.

Jambo jingine nawaasa wanasiasa kwamba tuache siasa za kupakana matope kwani wananchi bado tunahoji?

Tumeupenda upinzani kwa kuikosoa serkali na kuwaumbua wala rushwa wakubwa nchini akiwemo mh. Lowassa.

kwa pamoja bunge liliadhimia kumuondoa waziri mkuu kwa kuitumia vibaya ofisi....je nyie wapinzani mtatueleza nini watanzania ili tuwaelewe?

Leo Lowassa msafi,kesho Chenge msafi,kesho kutwa akina Muhongo na akina Kalamagi watakuwa wasafi endapo watapata fursa kuhamia CHADEMA.

Je, mnapozunguka mtaani kutueleza kwamba Magufuli ameuza nyumba mna ushahidi? Na kama mna ushahidi si mpeleke mahakamani?

Acheni siasa taka wananchi tunaelewa!

 
CCM tulieni dawa iwaingie au mnataka sindano ikatikie kwenye tako?

ImageUploadedByJamiiForums1438329409.124488.jpg
 
mkuu umeandika huku ukiwa umejawa hofu hukutegemea na hakuna aliyetegemea kuwa mh.Lowasa angetoka Ccm .kipindi hiki Ccm ipo gonjwa wasiwasi ni mwingi na hofu Kwa sababu hamjatambua nani atafuata .ni uamuzi mzito rejea hotuba ya mwenyekiti WA chadema wakati wanamtambulisha mh.Lowasa imejitosheleza.hiki si kipindi cha vitisho kubali mabadiliko.
 
Seconds into the 1st half mbowe, who was wrongly thought to be the pillar of chademas' defence, has two own goals to his tally.
 
Back
Top Bottom