Nakubaliana na wewe kwa sehemu lakini kosa mnalofanya ni kutenganisha maagizo ya Kanisa na ya Mungu. Hili mnahitaji shule kwelikweli.
Kwa mfano ni wapi Mungu anasema wanadamu wawe na Biblia yenye vitabu fulani tu? Kanisa kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu likafanya hilo. Kama umekubali agizo la Kanisa kuwa Biblia unayotumia ndio sahihi kwanini upinge maagizo mengine?
Ukusoma matendo ya Mitume utaona mitume waliagiza waamini wauze kila walichonacho wagawane kwa usawa na kuishi kishirika. Watu waliuza na yule mtu na mke wake walipodanganya kiasi walichopata walipata mauti kwa kukaidi lile agizo. Je ingekuwa wewe si ungesema ni agizo la wanadamu na si Mungu? au imendikwa wapi tuuze kila kitu na kugawana sawa? Leo ambao hatufanyi hayo makanisa yote tunakosea? Nani alisitisha hili?
Ijumaa kuu tumeagizwa kutokula nyama na Kanisa likatoa sababu ili dunia nzima tusichinje au kumwaga damu kama ilivyokuwa desturi zamani ya kumwaga damu za wanyama ili kuondolewa dhambi.
Ijumaa kuu hatumwagi damu za wanyama maana damu yenye thamani imemwagwa pale msalabani. Ni njia tu ya kuinjilisha na kutukumbusha ukomo wa kutumia damu za wanyama kuondoa dhambi!
Hakika Wakatoliki hatutokula nyama (maana yake msimwage damu siku hiyo) na siku hiyo idadi ya ngombe, kuku, nguruwe n.k itayochinjwa itakuwa ndogo tofauti na siku nyingine hivyo automatically kule kutii kutomwaga damu siku hiyo ni utii wa kutambua iko damu yenye thamani pale msalabani!! Zipo namna nyingi za tafakari ya neno la Mungu na utii kwa Kanisa si shauri ni lazima kama wewe ni Mkristo.
Mkuu unajua shida yangu mimi najua sana jinsi imani ilivyo na nguvu ,hivyo nikwa namwelimisha mtu wa imani tofauti na mimi huwa nakuwa makini sana na muda mwingine kuna vitu sitaji.
Angalia hapo juu nilpohighlight red,issue ya Ijumaa kuu kutokula nyama mimi nilifuata kama maagizo ya kanisa langu la zamani RC,kwa sasa siko huko.Sasa tukiwa tunataja majina kila wakati wengine tunaogopa kuwakwaza watu,nilitegemea ungegundua niliposema ni maagizo ya kanisa nilimanisha kanisa la RC na hivyo ambaye si wa kanisa hilo hafungwi na sheria za kanisa hilo.
Mimi si mshabiki wa dini,napenda watu wamjue Mungu wa kweli suala lako la biblia za aina nyingi nyinge sitazungumzia kwa sasa lakini najua kuna thread ilielezea vizuri hilo suala.
Sitaki nilete mada zingine ndani ya mada.Ni kweli umesema tunahitaji kuelimishwa lakini na wewe unahitaji kuelimishwa zaidi.Hakuna dini iliyo kamilika machoni pa wanadamu,Mungu akilijua hilo ndiyo maana hakusema watu wa dini fulani ndiyo wataingia mbinguni,mbinguni wataingia walio watakatifu tu kwa vipimo vya Mungu na si wanadamu.
Ebrania 12:14:"Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote,
na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao".
Kwa hiyo kama kuna mtu yeyote anataka kwenda mbinguni jibu liko hapo juu,dini hazitaisha,tofauti hazitaisha lakini neno la Mungu litasimama.
Kwa hiyo nirudie tena kutokula nyama siku ya ijumaa kuu ni mapokeo ya wanadamu,si agizo la Mungu ingawa kama watu hao wamekubaliana wasile nyama siku hiyo,Mungu anaheshimu makubaliano.Huku ninakoabudu tumekubaliana kula nyama until further notice.
Nye mmekubaliana msile,well and good.Wewe uliyeambiwa usile,ukila utakuwa umekosea kwani umeagizwa hivyo.
Mbinguni hatutaingia kwa sababu tulisoma biblia yenye idadi fulani ya vitabu.