Ebu umiza kichwa kidogo?

Ebu umiza kichwa kidogo?

Uko sahihi mkuu, unaweza ukawa na Elimu na usitoboe maisha, kuliona Jicho la tatu kwenye biashara duu, kama muda mwingi ulikuwa shule na biashara umeiaza ukubwani ukiwa na majukumu, una familia, una madeni, stress za wana uliokuwa unawaona vilaza saizi wana push lc300 lanzima kichwa kiwake moto.
Acha tu classmates wa primary wanashusha contena za kutosha na wanapost status😨
 
Mm sio Mzee. Ila kuna namna naisifu Elimu ya Mkoloni.

Kulikuwa na watu wa fani mbalimbali (ufundi stadi) na watu wa taaluma white collar Job.

Sasa hapa katikat kama taifa hawakuipa kipaumbele Taaluma ya fani mbalimbali na wakaona fani sio mwelekeo sahihi. Wakaelekeza kwenywe wasomi na kutengeneza watu weng wa white collar job ambao pia kazi hazipo za kuwasitiri wote.

Kuna mtu anamaliza SUA.
Ila anasubiria aajiriwe.
Wakat mfano kama amesomea Livestock alitakiwa
Awezeshwe afuge na aelimishe jamii inayomzunguka maana anajua mifugo kwa undan . Na ataleta tija kwa jamii na taifa.

Ila sasa mtu kama huyo anataka aajiriwe. Inafikirisha.
Ila ni kwasababu ametaarishwa hivyo.

You are missing the point mkuu.

Ina maana mtu akisomea Utaalamu wa kutibu Mifugo, wewe unataka afuge ili aitibu mifugo yake?

Kwa kukwambia tu, Mfumo wa elimu hasa chuo ni Universal kwa vitu vingi ukiacha vichache vinavo kuja sasa(New tech ) ndo inachelewa kuja Africa.

Shida ya nchi za kiafrica ni uongozi, sera na uratibu.

Elimu tunaisingizia tu, Kuna vijana wengi sana hawajasoma bongo, wameaoma nje ya bongo lkn hata wakija hapa hawawezi kufanya maajabu.

Embu chukulia mfano, Mfugaji wa Ng'ombe morogoro anakosa soko la maziwa, lkn Nchi inaagiza maziwa kutoka nje. Hapo utasema nchi inaviongozi au Vichaa
 
Elimu pia ifupishwe.
Elimu ya Sekondar iwe miaka 4.
Mtoto akimaliza aingie kwenye fani na taaluma anayoipenda.
Kwa miaka 2 , 3 au 4 na akitoka hapo akiwa ana miaka 18+ awe anafanya kazi.

Kule kwao mtoto ana miaka 16 ana degree. Huku hadi 21+.

Mkuu kwa sasa hvi mtoto anaweza kuchagua, aende kusomea fani au White collar jobs after form 4.

Ni wajibu wa mzazi kumuelimisha vzuri mtoto faida na hasara za kila njia.

Japo tukitazama zaidi, walio somea fani ano ni choka mbaya tu, wana hela za kubadirisha mboga tu.
 
Back
Top Bottom