Ipo hivi tajiri; binafsi ni ngumu kueleza huo uhusiano wa elimu na kujiajiri/kufanya biashara.
Biashara/kujiajiri au vyovyote unavyoita, binafsi naona ni kiu ya mtu, na itoke ndani kabisa ya moyo wake. Kama unavyoona madogo wanakiu ya muziki, soka, siasa au carrier flani, basi na kujiajiri hivyo hivyo. Usifanye kujiajiri kama kuganga njaa wakati unasubiria kupata kazi. 😁
Mtu aone kujiajiri ni maisha yake, aone anapaswa kujiajiri ili aishi hivyo. Huyo atafanikiwa, atapata mtaji na ataajiri wengine.
Sio ujiajiri huku huku moyo wako unataka uajiriwe. 😁 Hutamwajiri yeyote na hukofika popote hata kama una elimu.
Biashara ni tabia, unapaswa kujenga tabia ya biashara, na yenyewe itakujenga.
Ushauri: Jenga tabia ya kufanya biashara, ishi biashara, fikiria biashara kila muda kila wakati, jifunze kuhusu biashara, kosea na jisahihishe katika biashara, kua na ishi biashara, biashara ikulaze macho, biashara ikuamshe alfajiri 5Am, biashara ikustue mapigo ya moyo. Ikiwa hivyo na biashara hiyo isipokupa utajiri na maisha bora, njoo unipige mawe. 😁