DW: Zitto Kabwe ametorokea nchi jirani

DW: Zitto Kabwe ametorokea nchi jirani

Enzi nachunga ng'ombe nilipenda sana michezo ya kuchonganisha madume ya ng'ombe kupigana.
Hali hiyo imeniathiri sana hata katika maisha yangu mengine.
Kwamfano, mchezo unaochezwa sasa kati ya wanasiasa "miamba" kwa upande mmoja na serikali ya Magufuli kwa upande mwingine mimi ninafurahia sana.
Ukiangalia hawa wanasiasa wanaotimuliana vumbi na serikali awamu hii ni "muvi" ya kustarehesha sana. Watu wanaoongea hadi nyasi zinatetema! Lakini kukicha mtu "ndani" Mh! Unaanza kujiuliza huyu bingwa wa jukwaa kageukaje mfungwa? Tulidhani anasema siasa kumbe alikuwa anaropoka! Kwanini msomi asichuje mbichi na mbivu?
Kwa awamu iliyopita nani angeweza kuona Lema yupo rumande?
Nani angeona Zitto anaisepa kama tumbili, arrest "tukufu" iliyoandaliwa kwa ajili yake?
Ninaegemea upande mmoja, upande wa mshindi. Kwangu mimi mshindi ndiyo mpango mzima maana wanasiasa wa Afrika ni sawa na timu zetu za soka nchini. Ukiwekeza ushabiki wako katika timu flani, unaweza ukafa kwa presha itokanayo na ushabiki. Nimebaki kumshangilia anayeshinda, bila kujali ni,wa upande gani.
Hii ndio nchi inayochagulia wanasiasa nini cha kusema halafu hapo hapo mnataka washindane sawasawa jambo ambalo haliwezekani
 
Fisadi mkubwa. Ameuza nyumba zetu. Amenunua kivuko kibovu, ameliingizia taifa hasara ktk samaki etc
Prove basi by documentation Ili na sisi tujue nyumba yako ipi iliyouzwa mkuu?
 
Yaani gari yangu ikiwa haina vibali naweza kutoroka nchi? Just use a little bit of common sense.
 
Yaani gari yangu ikiwa haina vibali naweza kutoroka nchi? Just use a little bit of common sense.
Ndio ujue kuna watu wanatumika kuvuruga amani ya nchi who knows huko alikokimbilia ndiko wanakomtumia!
 
Ndio ujue kuna watu wanatumika kuvuruga amani ya nchi who knows huko alikokimbilia ndiko wanakomtumia!

Mimi si muumini wa hicho ulichokisema. Hakuna mtu yeyote anayetumika kuvuruga amani ya nchi hii. Haya ni maneno wanayoyatumia zaidi wanasiasa kutia hofu watu huku wakiwa na ajenda zao za siri.
 
Mr. Mark are you serious? Utendaji makini au utishaji na utesaji uliokubuhu?
 
Prove basi by documentation Ili na sisi tujue nyumba yako ipi iliyouzwa mkuu?
Mzee ofisadi ni sawa na moshi huwezi kuufuta.
Nyumba za shirika letu LA NHC ziliuzwa kwa bei ya kutupwa na mbaya zaidi ziligawiwa kwa upendeleo hadi vimada na watoto wa mtukufu wakapewa
Kama nalo unalikataa hilo basi hebu Fanya utafiti wako kimyakimya
 
Anakimbia ana kosa gani? Hilihili kosa la gari yake kutokuwa na documents muhimu?
 
Ameiba nini au ni mfuasi wa Yahaya?? Nchi hii ina amani tele, vyakula tele, maji tele kama ni mvua ni kwa wote. Yeye sio waziri wa Mali asili useme alitoa amri wafugaji wauliwe. Wala hajalima kwenye vyanzo vya maji ka yule mbunge mwenzake. Unakimbia nini Tz hii?? Nawaza tu
Haha hahah haaaa! "Vyakula tele"!!!
 
Haha hahah haaaa! "Vyakula tele"!!!

Tewe;
Inamaana nimeandika maajabu?? Mbona twaviona huko masokoni na kwenye magulio kule dodoma soko la mahindi?? We upo wapi mkuu tukuletee aina unayotaka? Hata mtori kwa wagonjwa upo ni weye tu
 
Dw- Swahili imekuwa kama Uhuru na Tanzania Daima tu, ni mwendo wa propaganda tu.
Nani anapropagate hapa kati yako na DW?
Wao wana source ya information wanayotulisha, wewe unayo au unasubiri humu ndio ujiongeze na kujionyesha kuwa upo current? Learn to read between lines ili update dhima ya kikixhokusudiwa na yafaa udigest before erupting like volcano here.
Kisha acha dharau za kitoto. Unayoyaita magazeti ya udaku na huwezi kumiliki hata kijarida cha page tatu ni upungufu wa akili.
Au wewe ni salesman wa Uhuru na mzalendo na ili uishi lazima uiponde product ya mwingine? Sijui mnasomeaga wapi ujinga huu! Pathetic!
 
Ameshakata tamaa na kachama kake ka ACT hakawezi toka tena kwa aina hii ya utendaji mzuri wa JPM. Kama cdm wanahaso vipi kwa ACT

Wabongo mnaridhika mapema ndo maana mnaishia kuwa maskini
 
Karibuni Nita Update hapa

Nimerekodi Audio imeshindikana Ku Upload hapa

-Dada aliyekua anahojiwa kakataa kukimbia kwa zitto Kabwe na wala hajakubali kuwa yupo Nchini amesema mpaka Kikao cha Chama kikae ndiyo wataongelea hilo.

-Zitto Kabwe yupo na ni mzima wa Afya ila haja sema yupo wapi ila anasema wanamawasiliano naye.



Labda anakimbia lile deni la mill 300 .
 
Tewe;
Inamaana nimeandika maajabu?? Mbona twaviona huko masokoni na kwenye magulio kule dodoma soko la mahindi?? We upo wapi mkuu tukuletee aina unayotaka? Hata mtori kwa wagonjwa upo ni weye tu
Inawezekana unaishi kuzimu Mimi sili vyakula Vya huko
 
Kwani rais hapati mshahara hadi useme anakula bure dhihaka kwa watawala siyo nzuri. Pia ni kosa kisheria.
Ushawahi muona rais gani sokoni, Haruna zihaka mkuu wa nchi huandaliwa kila kitu pamoja n'a chakula ni sehemu y'a gharama za office n'a ndiomaana anaishi offisini. Hii yote ni kumfanya mkuu afikirie jambo moja ustawi wa nchi n'a wananchi wake kwa maslahi y'a wananchi.
Huwezi kumfsnya mkuu afikirie chakula n'a mavazi
 
Back
Top Bottom