DV Lottery (green card) 2012

DV Lottery (green card) 2012

mkuu thanks sana, sasa nataka kutuma hii form je naweza kutumia posta yetu ya kawaida, je on average posta za kawaida hutumia muda gani kufikisha barua U.S, DHL naona ni ghali mno...je nikitumia posta sitapoteza muda sana?

Posta ya kawaida tu wiki inakuwa ishafika mkuu huna haja ya kuingia gharama kubwa mapema hivi wkt kazi ipo mbele!
 
mkuu nashukuru labda nifanunue kidogo, ile stage ya kutuma maombi online ilishapita sasa nimechaguliwa kwa ajili ya kwenda kufanyiwa interview na masuala mengine sasa ndio nilitaka kujua kama kuna mzoefu aliepata miaka ya karibuni anipe details, ni kipi hasa wanahitaji?

Kuna watu wawili pale Vodacom Dar wameshinda Greencard ya intake hiyohiyo unayoulizia. Fika ofisi za Voda headquarters ulizia suala hilo na omba kuonana na hao walioshinda kwani pale wanajulikana watakuelekeza nini cha kufanya.
 
vipi ulifanikiwa kushinda dv lottery?
habari za leo wanajamii, mashabiki wa man u poleni kwa kipigo toka imarati...

Kwa wadau wanaofuatilia dv lottery 2012 matokeo yameshatoka leo May1, nilitaka kuuliza kuna yeyote humu amepenya jamani?? Au kuna ambaye amewahi kupata dv lottery (nazungimzia ile yenyewe inayotolewa na state department sio phishy agents) hii anisaidie maujanja pamoja na docs za kuwa nazo ikiwa umechaguliwa??
 
Boss, wacha uongo zako mingi mingi mingi, hakuna makachero watakao tumwa kijijini kwa uchungizi, hakuna FBI watachunguza mienendo yako ukishinda green card, so, wacha kuweka watu uoga bure
Naomba nikupe tahadhali hivi karibuni nilikuwa bongo na mtu mmoja akapata email ya kitapeli ikimujulisha kuwa amewin green card, sasa angalia kuna matapeli. Forms hizo zitatumwa kwako kutoka state dept zina (bar code).

Kumbuka hakuna malipo yoyote ambayo utatakiwa kuyafanya mpaka siku ya kuitwa ubalozini kwakuwa uko Tanzania.
Na hiyo itakuwa baada ya kukamilisha hatua zote hizo ambazo si chini ya miezi 6(napo sema miezi sita mara nyingi ni zaidi ya hiyo miezi) kwa maana taarifa zako zote na historia yako maafisa wa FBI na makachelo wengine wa kimarekani watazifanyia kazi wakisha kuclear kwamba siyo jambazi au huna matatizo yoyote ya kiafya n.k ndipo watakapo kujulisha tarehe na saa ya interview hapo ubalozini.

Siku ya interview huna maelezo mengi wanachotaka ni kukuona physically maana kumbuka muda wote utakuwa umekuwa unawasiliana nao kwa makaratasi na picha tu,hivyo wanachofanya siku hiyo nikukagua document's ulizowatumia na original copies ulizo nazo.Hivyo mpaka kufikia hatua hiyo huwa kuna miezi kadha. Jitahidi kuwa mkweli maana hawa jamaa watafika mpaka kijijini kwako(Kufanya Vetting).

Huchagui aina ya visa/viza kwani hiyo greencard or DV lottery Visa inajieleza, ni visa inayokupa status ya kuwa mkazi wa marekani(permanent residence),ambapo unakuwa na haki zote za raia wa Marekani isipokuwa kupiga kura kwenye uchaguzi wa ngazi za kitaifa(federal).

Hivyo na sisitiza kama una barua hiyo na huna uhakika nayo nenda Ubalozi wa marekani uthibitishe kwani kuna utapeli umeenea hasa kwa kuzingatia kuwa watu wengi ni wageni kwenye swala hili, usimtumie mtu malipo yoyote malipo yanalipwa siku ya interview ambayo haifanyiwi mahala popote zaidi ya ubalozini.
 
Nilipata email kama two weeks ago ikinitaarifu kuwa nimebahatika kuwa chosen, na nilipie USD 800 per person. Actually nikawapigia watu wa kitengo cha diversity visa US Embassy ku-confirm nao wakaniambia it is absolutely scammer. Ningependa kutoa tahadhari kuwa usijiingize kwenye kulipia kwa postal orders au online. Ni vizuri ukalipie ubalozini kwani uwezekano wa kuibiwa ni mkubwa sana. This is from my personal experience not from someone else.

Walijua vipi ulikua umeshiriki?
 
Boss, wacha uongo zako mingi mingi mingi, hakuna makachero watakao tumwa kijijini kwa uchungizi, hakuna FBI watachunguza mienendo yako ukishinda green card, so, wacha kuweka watu uoga bure
Wajinga ndio waliwao...
Kila kitu Sasa ni digital. Wakutapeliwa na atapeliwe. Lakini Hilo halikua swala haswa, swala ni kuhusu makachero kufuata hadithi na mienendo ya mshiriki
 
We mtoto mdogo ndo unatoka high school, mi ni kama baba yako! Soma uzi wa lini huu na ulikuwa na umri gani? By the way nilihamia Marekani miaka mingi kwa hiyohiyo program na nina wadogo zako wa umri wako! Jielimishe kabla hujaropoka, ndo mana mnafeli sana vijana kama hamjacrem
Tumia hekma unapojibishana na watoto wa Rika langu, greencard ya kuenda marekani ni kuanzia October 5th Hadi November 7th. Hio ya miezi mbili ni Ile marekani umejitengenezea mwenyewe Kijiji kwenyu kigoma 🤣😂
 
Yes mpumbavu anajibiwa kipumbavu, kama umejua hii programu mwaka jana usilazimishe watu waliotoa maelezo miaka 10 iliyopita wakufuate mtoto! Kwa hiyo ukikariri mambo ya mwaka jana ulipofunguka macho unataka na waliofanya kabla ya mabadiliko wakufuate? Ndo maana tunasema kwa elimu yenu ya kakariri hamtajifunza kitu hadi waliowakaririsha warudi kuwafundisha upya! Grow up boy

Anyway am off this shit, chukua unachotaka vingine acha!

Kumbe kuzeeka sio kua na hekima?

Kumbe Kuna waliobaki analogue, washamba na bado hawana habari.

Eti uko marekani?

New Orleans ama little Haiti?

Wewe upo pepo ya magurubasi.

😂🤣
 
We mtoto mdogo ndo unatoka high school, mi ni kama baba yako! Soma uzi wa lini huu na ulikuwa na umri gani? By the way nilihamia Marekani miaka mingi kwa hiyohiyo program na nina wadogo zako wa umri wako! Jielimishe kabla hujaropoka, ndo mana mnafeli sana vijana kama hamjacrem
Kwani wewe umri wake unaujua ?

Mbona unabwabwaja maneno hovyo kama Katibu mwenezi wa ccm.
 
Tumia hekma unapojibishana na watoto wa Rika langu, greencard ya kuenda marekani ni kuanzia October 5th Hadi November 7th. Hio ya miezi mbili ni Ile marekani umejitengenezea mwenyewe Kijiji kwenyu kigoma 🤣😂

Ok samahani! Nakuwa muungwana basi kijana! Nilicheza DV lottery mwaka 2008 na by that time ilikuwa entries zinafanywa miezi miwili, walikuja kupunguza baadaye. Nilicheza mara 1 tu na nikachaguliwa nikaja na familia mwaka 2009. So hiyo ya mwezi mmoja ilikuja kuanza nafikiri 2010 au 2011, sina uhakika
 
Kumbe kuzeeka sio kua na hekima?

Kumbe Kuna waliobaki analogue, washamba na bado hawana habari.

Eti uko marekani?

New Orleans ama little Haiti?

Wewe upo pepo ya magurubasi.

😂🤣

No! Japo New Orleans ni US pia ila sipo huko! Nipo Denver Colorado, nimeishi State 2 tu miaka yote hiyo, Joliet City IL, na Denver CO kuepuka kuhamahama sana wkt nimekuja na familia na watoto wanasoma. Natengeneza pesa nzuri tu ya kuishi na kufanya investments zangu home, sijawahi kujututia kuja hapa, na familia yangu yote ilishapata citizenship mimi tu sijachukua kwa sababu sitaki sheria za Tz hazieleweki na nina mali huko. Nikitaka nachukua muda wowote, but green card bado inakidhi mahitaji yangu kwa sasa
 
Back
Top Bottom