Duuu...! Enzi hizo...bora turudi zamani...!

Duuu...! Enzi hizo...bora turudi zamani...!

Enzi hizo wanafunzi wanasafiri kwa gari moshi kwa warrant hakuna malipo mkoa hadi mkoa
 
Enzi hizo majeneza yalikuwa mpaka mtu afe ndo linachongwa lakini siku hizi dah majeneza kila kona na viwango kama magari.
 
Duuu,

leo nimekaa nimefikiria sana enzi za zamani kwa kweli nimetamani turudi enzi hizo, enzi za zamani, kila kitu kilikuwa poa, upendo amani yaan raha sana zamani kuliko sasa!!

nimekumbuka enzi hizo tunajiendea HOSPITALINI bureee yaani ukifika manesi wanakupokea kwa furaha wanakuhudumia, na unapewa dawa bureeee.....duuu enzi hizo jamani ilikuwa raha saaaana

nimekumbuka enzi hizo kweli ukisikia mwanafunzi kafaulu darasa la saba au form four ujue kweli ni kichwa tena balaaa, yaani wale vichwa wa juu walikuwa wanapatikana MZUMBE, ILBORU, KILAKALA, MSALATO..ifunda, iyunga ....teh teh jamani jamani enzi zetu.safi sana.

nakumbuka enzi izo ukitaja UDSM basi unataja hapo MUHIMBILI, ARDHI, DUCE, IJMC na ilikuwa mtu ili aende chuo kikuuu kweli inaitaji usomeee, kwanza kulikuwa hakuna migomo kabisa. lakini sasa

nakumbuka enzi za makamba dar es salaam, teh teh kina matonya, bongo ilikuwa burudani sana, wanafunzi wa sekondari dar wanavaa vikaptula...teh teh jamani enzi hizo ilikuwa bomba eeeh

.......!!!!

kwenye migomo hapo umechemka muulize Sita mb alifanyweje na nyerere
 
Enzi hizo tulikuwa tunafanya kazi bila komputer masaa nae, tunatumiana barua kwa posta, tunapanda UDA bila foleni barabarani, tunakula mikate ya siha, tunaangalia sinema za bure Drive In, kuna treni kila siku kwenda Mwanza na Kigoma na mara kadhaa kwa wiki kwenda Arusha, tunalala chuma kimoja watu wawili na tunajifungulia chai na maziwa kweye vibomba UDSM, tukipikiwa wali maharage lazima litoke tangazo kutuomba radhi pale UDSM, tunaheshimu wanasiasa, tunaandamana siku kuu za sabasaba na kushona (sio kununua) nguo mpya, tunapangiwa kazi hadi Uganda na Kenya tkiwa shirika la East African au customs, raisi na mawaziri wakitembelea mikoani tunaenda kuwapokea na matawi ya miti mikononi!

Yaani, basi tu!

Mwisho wa mambo mazuri bwana ilikuwa Idd Amin alipochukua nchi Uganda na Arap Moi alipochukua nchi Kenya.

Tukapigana vita Uganda

Tukaanza kupanga foleni ya unga na sukari, tukajua kuna mwendo wa kuruka, tukaujua ugali wa yanga, tukawa na maduka ya kaya, zikaingia dala dala, tukaanza kununua bia na soda kwa vibali, ice cream zikapotea, Blue Band za Kenya zikapotea, tukaanza kununua Colgate na kanga toka Kenya kwa magendo, tuaka tunatakiwa kuwa na kibali kuleta debe moja ya mchele toka Mbeya kuja Dar, tukawa tukienda ulaya tunafanya shopping ya colgate, sabuni Imperial na viatu vya kukimbilia (raba mtoni), suruali za Jeans na kodurai zikawa mali adimu sana, tukawa tunakosa usafiri wa kwenda mikoani kwa sababu mabasi ya Relwe na Kamata na Kwacha yamejaa mwezi mzima.

Mmh, kweli mambo hubadilika.
hahahaaaaaa sana mkuu umenikumbusha sabuni ya imperial ukitoka hapo unapaka mafuta ya kutoka zanzibari yalikuwa kwenye vimikebe hivi yananukia balaaaa mkuu Synthesizer nikumbushe jina la haya mafuta kama unalikumbuka yalikuwa na pisha ya ngalawa
 
Last edited by a moderator:
Enzi zako za zamani ni mwaka gani?

Hata mimi ndo nimejiuliza ni miaka ipi anaongelea maana shule ninazozijua zilizokuwa zikichukua wanafunzi walifanya vizuri toka mkoloni huwezi kuacha kutaja Tabora boys na girls,hata Kibaha ndo magwiji wa siku nyingi.
 
Enzi hizo ukienda kuanza darasa la kwanza ukubwa unapimwa kwa kupitisha mkono juu ya kichwa ili kushika sikio la kushoto,shule nyingi zilikuwa mbali na unawahi namba maana kutoka nyumbani hadi shuleni ni kukimbia,shuleni kulikuwa na vikundi mbalimbali vya fani mfano kuchora,mwandiko,hisabati , kukimbia nk,kipindi hicho mipira tunacheza peku lakini mtu akikukanyaga/akikuchezea rafu unaweza chechemea mwezi mzima...lol! FRANKLY, THOSE WERE GOOD OLD DAYS
 
Enzi hizo tulikuwa tunafanya kazi bila komputer masaa nae, tunatumiana barua kwa posta, tunapanda UDA bila foleni barabarani, tunakula mikate ya siha, tunaangalia sinema za bure Drive In, kuna treni kila siku kwenda Mwanza na Kigoma na mara kadhaa kwa wiki kwenda Arusha, tunalala chuma kimoja watu wawili na tunajifungulia chai na maziwa kweye vibomba UDSM, tukipikiwa wali maharage lazima litoke tangazo kutuomba radhi pale UDSM, tunaheshimu wanasiasa, tunaandamana siku kuu za sabasaba na kushona (sio kununua) nguo mpya, tunapangiwa kazi hadi Uganda na Kenya tkiwa shirika la East African au customs, raisi na mawaziri wakitembelea mikoani tunaenda kuwapokea na matawi ya miti mikononi!

Yaani, basi tu!

Mwisho wa mambo mazuri bwana ilikuwa Idd Amin alipochukua nchi Uganda na Arap Moi alipochukua nchi Kenya.

Tukapigana vita Uganda

Tukaanza kupanga foleni ya unga na sukari, tukajua kuna mwendo wa kuruka, tukaujua ugali wa yanga, tukawa na maduka ya kaya, zikaingia dala dala, tukaanza kununua bia na soda kwa vibali, ice cream zikapotea, Blue Band za Kenya zikapotea, tukaanza kununua Colgate na kanga toka Kenya kwa magendo, tuaka tunatakiwa kuwa na kibali kuleta debe moja ya mchele toka Mbeya kuja Dar, tukawa tukienda ulaya tunafanya shopping ya colgate, sabuni Imperial na viatu vya kukimbilia (raba mtoni), suruali za Jeans na kodurai zikawa mali adimu sana, tukawa tunakosa usafiri wa kwenda mikoani kwa sababu mabasi ya Relwe na Kamata na Kwacha yamejaa mwezi mzima.

Mmh, kweli mambo hubadilika.

Duuu! mwana kweli wewe wa zamani kinoma noma!
 
nakumbuka nesi mmoja alikuwa akikuchoma sindano unavimba kalio la upande mmoja.....Ukifika zahanati ukimwona unaliaaaaaaa....hadi unakaukiwa machozi... kuna mwenzie ulikuwa ukimwona unafurahiii akikuchoma sindano hata husikiiiiiiiiiiiii akifikicha hapo na pamba yenye spirit ndo rahaaa inaongezeka then anakwambia poleeee poleeeee we zamani rahaaaa
 
enzi hizo ngono ilikua nyama nyama tofauti na sasa nyama mpira nyama

enzi hizo hatukuwa na maneno ya kuchekesha kama kapuyanga alivyonichekesha mpaka nimepaliwa......ha ha ha hawa watoto wa siku hizi wanchekesha kidigital zaidi.
 
Haya wazee wa zamani tumewaelewa...
Population inakua, changes are inevitable, na uchumi unazidi kuporomoka, hela wanakopa IMF ili wajenge nyumba zao Dubai na California... Kazi burebure si sababu wazungu waliondoka wakawaachia kampuni kibao huku watu wenye elimu ndio walikua wameanza anza kuonekana, kila mtu na degree siku hizi mnategemea nini kama sio kunyang'anyana, mjanja lazima apewe...
Usijeshangaa serikali inasema inatumia zaidi ya bilioni kumi kununulia walimu chai asubuhi..
 
bora sikuwepo enzi hizo nisingefaidi mambo ya smartphone,tv bwelele,computer kibwena,kila mtu anafika sekondari miaka yenu mnamaliza la 7 watoto 150 alafu anafaulu 1...dunia hii ndio tamu acheni kusifia uongo nyie mababu
 
Back
Top Bottom