Duuu...! Enzi hizo...bora turudi zamani...!

Duuu,

leo
nimekaa nimefikiria sana enzi za zamani kwa kweli nimetamani turudi
enzi hizo, enzi za zamani, kila kitu kilikuwa poa, upendo amani yaan
raha sana zamani kuliko sasa!!

nimekumbuka enzi hizo tunajiendea HOSPITALINI bureee yaani ukifika
manesi wanakupokea kwa furaha wanakuhudumia, na unapewa dawa
bureeee.....duuu enzi hizo jamani ilikuwa raha saaaana

nimekumbuka enzi hizo kweli ukisikia mwanafunzi kafaulu darasa la saba
au form four ujue kweli ni kichwa tena balaaa, yaani wale vichwa wa juu
walikuwa wanapatikana MZUMBE, ILBORU, KILAKALA, MSALATO..ifunda, iyunga
....teh teh jamani jamani enzi zetu.safi sana.

nakumbuka enzi izo ukitaja UDSM basi unataja hapo MUHIMBILI, ARDHI,
DUCE, IJMC na ilikuwa mtu ili aende chuo kikuuu kweli inaitaji usomeee,
kwanza kulikuwa hakuna migomo kabisa. lakini sasa

nakumbuka enzi za makamba dar es salaam, teh teh kina matonya, bongo
ilikuwa burudani sana, wanafunzi wa sekondari dar wanavaa
vikaptula...teh teh jamani enzi hizo ilikuwa bomba eeeh

.......!!!!

Enzi zile, kama dingi ana kauwezo fulani. sehemu maarufu za kuangalia film ni kwenye majumba ya Wadosi: Empress, NewChox, Avalon, Nulite, Cameo, Diamond Talkies, Liberty ....
 
Enz izo mtu akiingiza CM nyumban kwake anaogopwa,,,,cm unaunganshwa kama umeme,!

Enz izo kupiga cm mpaka pista,,,!
Enz izo tv hakuna,,,!

Nakumbuka kwa mara ya kwanza TV niliiona mwaka 86 kwa jiran etu alikua tajir mnooo!

Ilikuwa mpaka upige 900 ili oparator akuunganishe. Na kama siku hiyo ameamka vibaya na mumewe basi utashinda posta kusiubiri simu
 
Enzi hizo kutongoza msichana ilikuwa kazi kubwa. Ilikuwa unaandika barua au unamtuma rafiki yako. Ukijitahidi kutongoza mwenyewe ilikuwa msichana hakuangalii usoni anatafuna unyasi au anasugua kidole gumba cha mguuni chini akiwa amegeukia pembeni. Unaweza kusota miezi kabla hujapata mechi ya kirafiki. Sasa hivi kutongoza kazi rahisi sana. Ndani ya dakika mbili umemeliza kazi na wasichana wa siku hizi wanakuangalia mpaka unaweza kupoteza mwelekeo. Kuandika barua siku hizi watu hawajui zaidi ya sms. Gonjwa la ngono lililozoeleka waktin huo ni kisonono ambapo wazoefu walikuwa wanaliita "mafua" Kaswende ndiyo iliyokuwa inaogopwa zaidi

Siku hizi vijana wanavaa mlegezo yaani kata k wakati huo vijana walivaa "don't touch

Dini za kuombea kuombea na kufanya miujiza wakati ule hazikuwepo wala hatukusikia manbii na mitume kama sasa. Zamani ilikuwa kama ni mkristo sana sana utakuwa RC,Litherani,assemblies of Godi,Sabato,Aic au moravian. sasa hivi kila kona kuna kanisa!

Wakati huo waganga wa kienyeji walikuwa wanaishi vijijini tena mbali kabisa na wanavijiji wengine. Siku hizi wameingia mijini na kuweka mabango Kukubwa zaidi ni kuwa wamasai walikuwa hawaishi mijini. Ukimuona mjini ujue kaja hospitali. Lakini sasa wamejaa na walianza kama walinzi kwenye nyumba za watu

Jamani naimiss zamaniiiiiiiiii!
 
Back
Top Bottom