Hii haichekeshi lakini imenibidi nicheke, anyway pole sana dada!
Kwa mtazamo wangu nafikiri ni busara kabisa kuweka tatizo hili wazi kabla hamjaingia kwenye commitment kubwa kama ndoa. Sasa kwa kuwa umemuuliza na yeye amekiri kwamba ni kweli mambo hayako sawa na yeye pia hajui tatizo, ni bora mkawaona wataalam wa afya ili waweze kuwapa majibu ya kitaalamu yanayoeleweka ambayo ndiyo yatakayowapa mustakabali wa kuendelea kwa ndoa yenu ama la.
Naamini mapenzi hasa tendo la ndoa ni furaha sasa linapogeuka kuwa karaha sidhani kama ni kitu cha kukaa nacho kimya. Kabla ya wazazi hawajakuuliza sababu hasa ya wewe ku hold back, mshauri mwenza wako mkaonane na madaktari ili kuona kama kuna ufumbuzi wa tatizo lake, isije kuwa unajifanya unavumilia mara kitu kikatokea mdomoni siku moja bure.
Ni hayo tu dada
Grace Komba, pole though