Duniani watu ni wanafiki Sana

kwisha

JF-Expert Member
Sep 9, 2021
1,666
4,365
Mrusi alivyoshambulia ukrain nakuchukuwa baadhi ya majimbo ya ukrain
Kuna watu walimuita putin shujaa mbambe wa dunia sijui nini wengine walikwenda mbali wakamuita baba mtakatifu Wa ukrain walivyo jaribu kulalamika nakuomba msaada wa dunia baadhi ya watu waliwaita wanafiki mashoga

Kuna watu uko Wanapewa kichapo kila kukicha wanazunguka mitandaoni wakitaka watu wote tuwaonee huruma

Kwa dunia ya sasa kila mtu na mnyonge wake
Kama nguvu munayo kweli nendeni kupambana kwenye uwanja wa vita uko sio mitandaoni
 
Mrusi alivyoshambulia ukrain nakuchukuwa baadhi ya majimbo ya ukrain
Kuna watu walimuita putin shujaa mbambe wa dunia sijui nini wengine walikwenda mbali wakamuita baba mtakatifu
Wa ukrain walivyo jaribu kulalamika nakuomba msaada wa dunia baadhi ya watu waliwaita wanafiki mashoga


Kuna watu uko Wanapewa kichapo kila kukicha wanazunguka mitandaoni wakitaka watu wote tuwaonee huruma

Kwa dunia ya sasa kila mtu na mnyonge wake
Kama nguvu munayo kweli nendeni kupambana kwenye uwanja wa vita uko sio mitandaoni
Vipi na wale wanaomtukana Putin na kumlaani kwa kumuita Shetani, mtu muovu kuliko wote duniani na kumpinga kwa kuivamia Ukraine na kuikalia ila kwa Wapalestina wanaunga mkono kunyanyaswa kwao na kupigwa na "Israel"?

Mimi binafsi nilipinga Putin kuivamia Ukraine, lakini kuna undumilakuwili wa ajabu unaoneshwa katika migogoro hii.

Haiwezekani tulaani anayofanya Putin kuwa ni ugaidi ila hayo hayo akifanya "Israel" ni kujilinda.

Haiwezekani tuwa shangilie waUkraine kwa kujitetea na kupigania uhuru wao bila kujali kuwepo kwa makundi ya kigaidi na yenye mrengo wa Kinazi kama Azov Battalion ila wapalestina tuwashambulie kuwa ni magaidi.

Haiwezekani WaUkraine wakipigwa na kubanwa pale wanapojaribu kujitetea tulazimishwe kuwaonea huruma lakini wapalestina wakipigwa pale wanapojaribu kujitetea tuseme waliyataka wenyewe.

Baadhi yenu ni mashahidi wakati Urusi anaivamia Ukraine, vyombo vya habari vili waonesha watu waliokuwa wakitengeneza Molotov cocktails kujiandaa dhidi ya Urusi na watu/raia waliokuwa waki pose na bunduki wakiwa proud kabisa kupigania nchi yao. Ila kwa Wapalestina wangeonekana ni magaidi.

Na baadhi ya watu wamekuwa wakimuunga mkono Putin kama kuonesha hasira tu ya namna mataifa ya magharibi yanavyopuuzia suala la Wapalestina ambalo lina miaka mingi mno na migogoro mengine. Huku suala la Ukraine lililoanza mwaka jana, au kama ukirudi nyuma zaidi limeanza mwaka 2014, reaction yao ikiwa tofauti kabisa.
 
Back
Top Bottom