Duniani kuna mengi sikutegemea hili kunipata

Duniani kuna mengi sikutegemea hili kunipata

Toa vielelezo kamamoja alivyosema.Itasaidia sana.Kama hujui.namna ya kutumia.Mtafute MTU yeyote Pm Mwombe no.Ya Whatsaap.Mtumie vielelezo.kwa.njia ya Whatsaap ambayo ni rahisi.Then yy ataweka hapa.Mana kuweka hapa ni ujuzi mwingine.Wengi hawajui.
 
Utapata matibabu vizuri kabisa kwa kutumia bima ya afya kwa hiyo 76,500 kwa mwaka
Hebu nieleweshe hii njia inavofanya kazi naweza nikamlipia hio nina ya afya!! Please reply
 
Duuu pole sana mkuu nimehuzunika sana usijali MUNGU mkubwa atakufanyia wepesi
 
Matibabu pale ocean road naambiwa ni kama bure vile!
Sina uhakika.
Pole kwa mtihani unaokukabili.
Bure za kwenye makaratasi tu ndugu mwimbili kwenyew wanasema almost free ukiulizia unaambiwa 8m
Mungu amjaalie ndugu yetu uyo apate matibabu
 
Pole sana, mungu akusaidie na kukuponya. Mimi nipo tayari kukuchangia hela ya matibabu na pia kukuombea mchango from my coworkers, kama hutojali kuweka wazi vielelezo vitavyosaidia kuthibitisha ukweli wa hii habari. eg. makaratasi ya huko hospitali ocean road re: the diagnosis and required treatment
Nimependa ulivyo waza
 
Pole sana, mungu akusaidie na kukuponya. Mimi nipo tayari kukuchangia hela ya matibabu na pia kukuombea mchango from my coworkers, kama hutojali kuweka wazi vielelezo vitavyosaidia kuthibitisha ukweli wa hii habari. eg. makaratasi ya huko hospitali ocean road re: the diagnosis and required treatment
Inawezekana wala hawezi kufanya hizo mambo mkuu,km kweli Mungu kakuelekeza kwake nakushauri umpigie umuelekeze pa kukukuta na umweleze aje na viambatanisho vyote vya Hospital, ikibidi kuanzia vile vya Temeke,Muhimbili hadi Ocean road,....naimani utapata malipo makubwa mbele za Mungu.
 
Mkuu sis ni vijana wenzako na wengine ni wazaz wako tunapenda sana kukupa msaada kaka yetu mpendwa kwa sababu tumeguswa na tatizo lako kama member mwenzetu..tunaomba tu uweke document za matibabu hapa ili tuthibitishe na tuweze kukusaidia kwa tulichojaliwa.kukwambia uweke document haina maana ya kukudhalilisha bali ni sisi kua na aman na jinsi ya kukusaidia ndugu yetu..tunakuomba tafadhali weka documents tuthibitishe huwezi jua mwenyezi mungu akawa amepanga tukusaidie hapa jamii forums
 
Naomba ujibu maswali haya..
Maumivu yako yakikushika je hua unatapika?
Ukitapika tumbo linatulia?
Wakati wa maumivu unasikia kizunguzungu?
Ndugu wana JF habari zenu ,poleni kwa kazi na majukumu mbalimbali ya ujenzi wa taifa.Nimeamua kuchukua uamuzi huu mgumu wa kuwashirikisha maisha yangu pengine naweza kupata faraja maana ni mzigo ambao unazidi kunielemea kadri siku zinavyozidi kwenda. Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28 nina mke na mtoto mmoja na naishi maeneo ya mbagala Dar es laam nikijishughulisha na kazi za ujenzi wa nyumba ,kama msaidizi wa mafundi ujenzi.

Stori yenyewe ni hii, toka mwaka 2014 nimekuwa najisikia maumivu makali sana tumboni ambayo huwa yananipata kwa muda na kupotea, hivyo sikufuatilia sana nikijua labda ni tatizo la kawaida tu maana maumivu yenyewe hunipata na kupotea hata kwa miezi kadhaa, lakini kadri ya siku zilivyozidi kwenda ndipo maumivu haya yaliendelea kunisumbua mara kwa mara na pia ikajitokeza tatizo la tumbo kujaa gesi ,baadhi ya watu wakaniambia labda nitakuwa na vidonda vya tumbo na kunishauri kuepuka vyakula aina fulani na kula aina flan flan pia kuzingatia mda wa kula kuepuka kushinda njaa nilifanya hivyo bila mafanikio yeyote baadae nikaenda kituo cha afya cha jiran nilivyowaeleza pia wakaniambia kuwa ni dalili ya vidonda vya tumbo wakanipatia utaratibu ambao niliufuata lakini sikupata nafuu maumivu yaliendelea japo yalikuwa yakipotea na kuyasahau lakini baadae yananirudia na kuathiri shughuli zangu za kujitafutia mahitaji.

Kufika mwezi wa nane 2017 ,nikaamua kwenda kupata vipimo zaidi maana tatizo lilizidi nikawa napungua uzito pamoja na kuanza kuona damu kidogo nyeusi kwenye haja kubwa, ilinishtua sana hali hii nikaamua niende hospitali ya Temeke kupata vipimo zaidi.

Baada ya vipimo Temeke wakanipa rufaa ya muhimbili, nikaenda muhimbili wakanifanyia vipimo , majibu yake ndio yaliyonifanya niandike hapa ,nilipata mshituko mkubwa sana nilivyoambiwa kuwa nina kansa ya utumbo mpana (colon cancer ) na iko stage IIA. wakaniambia watanitransfer ocean road nianze matibabu mara moja ambapo yatahusisha operation.

Kwakweli toka siku hiyo nimekuwa ni mtu wa kuchanganyikiwa nisijue la kufanya nikiangalia maisha yangu mimi ndio tegemeo la mama yangu huko kijijini pamoja na familia yangu hapa mjini na maisha yangu yanategemea kazi zangu hizi za kutumia nguvu nitawezaje kupata matibabu na hata baada ya matibabu nitaendeshaje maisha yangu, kwanini mungu ameamua kunipatia haya majanga katika umri wangu huu mdogo nikiwa mwenye majukumu mengi na kutegemewa sana na familia yangu ,hata hivyo sina uwezo wa kulaumu wala kujua mpango wa Mungu katika maisha yangu.

Nimeshindwa hata kumjulisha mama yangu kijijini maana najua nitamwongezea msongo wa mawazo tu. Nimejaribu kuwaomba ndugu marafiki msaada ambapo napata ahadi tu bila msaada na siwezi kuwalaumu maana natambua hali zao pia.

Nimekuwa nikitumia dawa ambazo ni za maumivu tu, nikiendelea kutafuta hela za matibabu japo hii hali imeathiri sana sana kazi zangu na kipato changu pia ila sina namna nyingine siwezi kufa nimekaa bora nifie kazini .Hela niliyoambiwa inahitajika kwa matibabu ya awali na operation ni sh.593,000/=ndio ambayo bado nahangaika kuitafuta japo nianze matibabu japo sijui nikiwa kwenye matibabu familia yangu itaishi vipi maana bila kutoka kutafuta chochote hata chakula itakuwa ngumu kupatikana na kazi zangu ni za kutumia nguvu .

Hivyo ndugu zangu NIMEAMUA NIWASHIRIKISHE WATU WENGI ZAIDI KUHUSU TATIZO LANGU MAANA SIWEZI KUJUA NI WAPI NAWEZA KUPATA MSAADA AMA FARAJA.Nimekaa nalo naona msongo wa mawazo unanizidia nimeamua kushirikisha watu naweza pata ushauri, faraja ,matumaini ,kukutana na walio wahi kupata tatizo kama langu na kufarijiana na hata msaada pia kwa atakayeguswa na shida yangu akanichangia atakachojaliwa kikanisaidia pia katika hali yangu ngumu.

Kwa atakaye guswa na hali yangu anaweza kunisaidi atakachojaaliwa chochote namba yangu ni [HASHTAG]#0678856312[/HASHTAG] jina Fidelis peter.nitashukuru sana.

Samahanini sitaweza kuwa online mara nyingi maana naingia kwa kutumia computer ya rafiki yangu sio mara zote naweza kuwa naye karibu nilikuwa na smartphone nikaiuza kutokana na tatizo hilhili ili kusaidia familia maana kazi zangu zimeathirika sana.


Asanteni ,
 
Pole kwa shida unayopitia, lakini nina mashaka makubwa kama Kweli wamegundua una kansa ya utumbo mpana(ca colon) Kwa sababu ya umri wako. Aina ya kansa iyo uwapata wazee ambao umri umekwenda Ie above 60.Yawezekana ukawa na vivimbe tu kwenye utumbo mpana ambavyo havijabadilika kuwa kansa.
Kama ni Kweli umekutwa na iyo kansa yawezekana ukawa wa kwanza kwa umri huo kukutwa na ca Colon.
Ata hivyo uwezekano upo wa kupata kansa ya colon kwa umri mdogo, hivyo basi weka documents mbambali kuthibitisha hilo ili tuwe na imani ya kuchangia.
Cha muhimu weka vielelezo ili tuwe na imani zaidi
 
Pole rafiki.. Ukifuata ushauri naamini utapona,tuko pamoja.
 
Pole sana, mungu akusaidie na kukuponya. Mimi nipo tayari kukuchangia hela ya matibabu na pia kukuombea mchango from my coworkers, kama hutojali kuweka wazi vielelezo vitavyosaidia kuthibitisha ukweli wa hii habari. eg. makaratasi ya huko hospitali ocean road re: the diagnosis and required treatment
Mimi pia nitamchangia nikiona vithibitisho,mjini sasa kumeharibika.
 
kwa kuwa upo dar nakushauri pambana nenda kwa rc makonda,nakuhakkishia ukikutana nae tuu jua, umesaidiwa, pia afya ndo kila kitu ndugu, kama we ni muislamu au mkiristo shiriki kwenye nyumva za ibada omba nafasi kwa waumini, jieleze hela unayoihitaj n ndogo tu watakuchangia;! NB; fanyia kaz
 
Pole sana, mungu akusaidie na kukuponya. Mimi nipo tayari kukuchangia hela ya matibabu na pia kukuombea mchango from my coworkers, kama hutojali kuweka wazi vielelezo vitavyosaidia kuthibitisha ukweli wa hii habari. eg. makaratasi ya huko hospitali ocean road re: the diagnosis and required treatment
 
Pole sana huwa kuna usemi wa kizungu unasema Nothing just happen. Mungu ataonesha njia Hakika.
Pole sana .
 
Huyu mgonjwa hajarudi tena? Amekwamia wapi?
 

Pia amtafute humu kuna member mwenzetu anaitwa FADILI PAUL, huyu ana utaalamu wa tiba hizi za kawaida za kutumia vyakula na majani.
Kuna dawa aliwahi kuizungumzia ni very simple,ni majani ya mstafeli, alisema ni tiba nzuri ya aina nyingi za kansa.
Kwa hiyo namshauri awasiliane nae anaweza kumpa ushauri utakao leta faraja kwake.
Pia aingie youtube aandike SOUR SOUP ataona hayo majani nisemayo,lakini ni bora sana awasiliane ma huyu member mwenzetu kwa kuwa anweza mwelekeza namna ya kufanya.
Huo ndio mchango wangu kwa member mwenzetu huku nikimtakia afya njema ma matumaini.
 
Back
Top Bottom