Ndugu wana JF habari zenu ,poleni kwa kazi na majukumu mbalimbali ya ujenzi wa taifa.Nimeamua kuchukua uamuzi huu mgumu wa kuwashirikisha maisha yangu pengine naweza kupata faraja maana ni mzigo ambao unazidi kunielemea kadri siku zinavyozidi kwenda. Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28 nina mke na mtoto mmoja na naishi maeneo ya mbagala Dar es laam nikijishughulisha na kazi za ujenzi wa nyumba ,kama msaidizi wa mafundi ujenzi.
Stori yenyewe ni hii, toka mwaka 2014 nimekuwa najisikia maumivu makali sana tumboni ambayo huwa yananipata kwa muda na kupotea, hivyo sikufuatilia sana nikijua labda ni tatizo la kawaida tu maana maumivu yenyewe hunipata na kupotea hata kwa miezi kadhaa, lakini kadri ya siku zilivyozidi kwenda ndipo maumivu haya yaliendelea kunisumbua mara kwa mara na pia ikajitokeza tatizo la tumbo kujaa gesi ,baadhi ya watu wakaniambia labda nitakuwa na vidonda vya tumbo na kunishauri kuepuka vyakula aina fulani na kula aina flan flan pia kuzingatia mda wa kula kuepuka kushinda njaa nilifanya hivyo bila mafanikio yeyote baadae nikaenda kituo cha afya cha jiran nilivyowaeleza pia wakaniambia kuwa ni dalili ya vidonda vya tumbo wakanipatia utaratibu ambao niliufuata lakini sikupata nafuu maumivu yaliendelea japo yalikuwa yakipotea na kuyasahau lakini baadae yananirudia na kuathiri shughuli zangu za kujitafutia mahitaji.
Kufika mwezi wa nane 2017 ,nikaamua kwenda kupata vipimo zaidi maana tatizo lilizidi nikawa napungua uzito pamoja na kuanza kuona damu kidogo nyeusi kwenye haja kubwa, ilinishtua sana hali hii nikaamua niende hospitali ya Temeke kupata vipimo zaidi.
Baada ya vipimo Temeke wakanipa rufaa ya muhimbili, nikaenda muhimbili wakanifanyia vipimo , majibu yake ndio yaliyonifanya niandike hapa ,nilipata mshituko mkubwa sana nilivyoambiwa kuwa nina kansa ya utumbo mpana (colon cancer ) na iko stage IIA. wakaniambia watanitransfer ocean road nianze matibabu mara moja ambapo yatahusisha operation.
Kwakweli toka siku hiyo nimekuwa ni mtu wa kuchanganyikiwa nisijue la kufanya nikiangalia maisha yangu mimi ndio tegemeo la mama yangu huko kijijini pamoja na familia yangu hapa mjini na maisha yangu yanategemea kazi zangu hizi za kutumia nguvu nitawezaje kupata matibabu na hata baada ya matibabu nitaendeshaje maisha yangu, kwanini mungu ameamua kunipatia haya majanga katika umri wangu huu mdogo nikiwa mwenye majukumu mengi na kutegemewa sana na familia yangu ,hata hivyo sina uwezo wa kulaumu wala kujua mpango wa Mungu katika maisha yangu.
Nimeshindwa hata kumjulisha mama yangu kijijini maana najua nitamwongezea msongo wa mawazo tu. Nimejaribu kuwaomba ndugu marafiki msaada ambapo napata ahadi tu bila msaada na siwezi kuwalaumu maana natambua hali zao pia.
Nimekuwa nikitumia dawa ambazo ni za maumivu tu, nikiendelea kutafuta hela za matibabu japo hii hali imeathiri sana sana kazi zangu na kipato changu pia ila sina namna nyingine siwezi kufa nimekaa bora nifie kazini .Hela niliyoambiwa inahitajika kwa matibabu ya awali na operation ni sh.593,000/=ndio ambayo bado nahangaika kuitafuta japo nianze matibabu japo sijui nikiwa kwenye matibabu familia yangu itaishi vipi maana bila kutoka kutafuta chochote hata chakula itakuwa ngumu kupatikana na kazi zangu ni za kutumia nguvu .
Hivyo ndugu zangu NIMEAMUA NIWASHIRIKISHE WATU WENGI ZAIDI KUHUSU TATIZO LANGU MAANA SIWEZI KUJUA NI WAPI NAWEZA KUPATA MSAADA AMA FARAJA.Nimekaa nalo naona msongo wa mawazo unanizidia nimeamua kushirikisha watu naweza pata ushauri, faraja ,matumaini ,kukutana na walio wahi kupata tatizo kama langu na kufarijiana na hata msaada pia kwa atakayeguswa na shida yangu akanichangia atakachojaliwa kikanisaidia pia katika hali yangu ngumu.
Kwa atakaye guswa na hali yangu anaweza kunisaidi atakachojaaliwa chochote namba yangu ni [HASHTAG]#0678856312[/HASHTAG] jina Fidelis peter.nitashukuru sana.
Samahanini sitaweza kuwa online mara nyingi maana naingia kwa kutumia computer ya rafiki yangu sio mara zote naweza kuwa naye karibu nilikuwa na smartphone nikaiuza kutokana na tatizo hilhili ili kusaidia familia maana kazi zangu zimeathirika sana.
Asanteni ,