Duniani kuna mengi sikutegemea hili kunipata

Duniani kuna mengi sikutegemea hili kunipata

Pole sana ndg ila kuna wachangiaji wamekuambia, weka wazi vielelezo vyako. Usione ati kuna mtu anataka kukudhalilisha bali kuaminiana kumepotea kabisa leo. Wewe weka hapa vifaa vyako kama hivyo vyeti na kadhalika uoane misaada utakayo mwagiwa.
Mfano: Ni Juzi tu alinipigia sim kama vile ni ku beep. Nikampigia. Akawa analia kabisa kuwa yupo kijijini, mahali fulani, anashida kubwa. akasema hawajala siku 3 yeye pamoja na watoto wake wachanga 4 aliachwa na bwanake akakimbia wala hawajui aliko. Nikamuuliza vizuri, upo wapi, akanitajia kile kijiji. Kumbe ni mahali napafaham sana. Nikamwambia, njoo kwenye njia ya kwenda shule ya sekondari hapa nakungoja nitakupa msaada. Ukifika tu hapo njiani, ni beep ntakuja kukusaidia. Akaanza; Oh! Kwani lazima unifaham?? Nikamwambia, sharti ni kumpa msaada ninaye mfaham. Akakata sim na hadi leo hajawahi nipigia tena. Toa vielelezo utasaidiwa
 
Pole sana, mungu akusaidie na kukuponya. Mimi nipo tayari kukuchangia hela ya matibabu na pia kukuombea mchango from my coworkers, kama hutojali kuweka wazi vielelezo vitavyosaidia kuthibitisha ukweli wa hii habari. eg. makaratasi ya huko hospitali ocean road re: the diagnosis and required treatment
Point
 
Pole sana, mungu akusaidie na kukuponya. Mimi nipo tayari kukuchangia hela ya matibabu na pia kukuombea mchango from my coworkers, kama hutojali kuweka wazi vielelezo vitavyosaidia kuthibitisha ukweli wa hii habari. eg. makaratasi ya huko hospitali ocean road re: the diagnosis and required treatment
Naunga mkono hoja awe muwazi na mi nipo tayali kumchangia mkuu pole sana ebu msikilize Nemo alivyosema
 
Pole sana, mungu akusaidie na kukuponya. Mimi nipo tayari kukuchangia hela ya matibabu na pia kukuombea mchango from my coworkers, kama hutojali kuweka wazi vielelezo vitavyosaidia kuthibitisha ukweli wa hii habari. eg. makaratasi ya huko hospitali ocean road re: the diagnosis and required treatment
Mungu atakukipa nemo kwa moyo wako
 
Yatapita Mkuu, kwanza anza kuweka mwili wako katika mazingira ya kula na kupumzika vizuri, stress inasababisha ugonjwa kuwa mkubwa zaidi, fanya mipango ya finacial status na omba MUNGU akuvukishe katika hili, POLE SANA Mkuu& ugua pole
 
Pole sana ndg ila kuna wachangiaji wamekuambia, weka wazi vielelezo vyako. Usione ati kuna mtu anataka kukudhalilisha bali kuaminiana kumepotea kabisa leo. Wewe weka hapa vifaa vyako kama hivyo vyeti na kadhalika uoane misaada utakayo mwagiwa.
Mfano: Ni Juzi tu alinipigia sim kama vile ni ku beep. Nikampigia. Akawa analia kabisa kuwa yupo kijijini, mahali fulani, anashida kubwa. akasema hawajala siku 3 yeye pamoja na watoto wake wachanga 4 aliachwa na bwanake akakimbia wala hawajui aliko. Nikamuuliza vizuri, upo wapi, akanitajia kile kijiji. Kumbe ni mahali napafaham sana. Nikamwambia, njoo kwenye njia ya kwenda shule ya sekondari hapa nakungoja nitakupa msaada. Ukifika tu hapo njiani, ni beep ntakuja kukusaidia. Akaanza; Oh! Kwani lazima unifaham?? Nikamwambia, sharti ni kumpa msaada ninaye mfaham. Akakata sim na hadi leo hajawahi nipigia tena. Toa vielelezo utasaidiwa
Pole sana kaka yangu mungu atakusaidia kuwa naimani tu...nenda hospital usisikilize watu wanao kuambia uende kanisani kwenye maombi. Hakuna kitu kama hicho. Nenda ocean road matibabu ya cancer ni bure. Nitakutafuta kwa namba yako kwa msaada zaidi

Ndugu wana JF habari zenu ,poleni kwa kazi na majukumu mbalimbali ya ujenzi wa taifa.Nimeamua kuchukua uamuzi huu mgumu wa kuwashirikisha maisha yangu pengine naweza kupata faraja maana ni mzigo ambao unazidi kunielemea kadri siku zinavyozidi kwenda. Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28 nina mke na mtoto mmoja na naishi maeneo ya mbagala Dar es laam nikijishughulisha na kazi za ujenzi wa nyumba ,kama msaidizi wa mafundi ujenzi.

Stori yenyewe ni hii, toka mwaka 2014 nimekuwa najisikia maumivu makali sana tumboni ambayo huwa yananipata kwa muda na kupotea, hivyo sikufuatilia sana nikijua labda ni tatizo la kawaida tu maana maumivu yenyewe hunipata na kupotea hata kwa miezi kadhaa, lakini kadri ya siku zilivyozidi kwenda ndipo maumivu haya yaliendelea kunisumbua mara kwa mara na pia ikajitokeza tatizo la tumbo kujaa gesi ,baadhi ya watu wakaniambia labda nitakuwa na vidonda vya tumbo na kunishauri kuepuka vyakula aina fulani na kula aina flan flan pia kuzingatia mda wa kula kuepuka kushinda njaa nilifanya hivyo bila mafanikio yeyote baadae nikaenda kituo cha afya cha jiran nilivyowaeleza pia wakaniambia kuwa ni dalili ya vidonda vya tumbo wakanipatia utaratibu ambao niliufuata lakini sikupata nafuu maumivu yaliendelea japo yalikuwa yakipotea na kuyasahau lakini baadae yananirudia na kuathiri shughuli zangu za kujitafutia mahitaji.

Kufika mwezi wa nane 2017 ,nikaamua kwenda kupata vipimo zaidi maana tatizo lilizidi nikawa napungua uzito pamoja na kuanza kuona damu kidogo nyeusi kwenye haja kubwa, ilinishtua sana hali hii nikaamua niende hospitali ya Temeke kupata vipimo zaidi.

Baada ya vipimo Temeke wakanipa rufaa ya muhimbili, nikaenda muhimbili wakanifanyia vipimo , majibu yake ndio yaliyonifanya niandike hapa ,nilipata mshituko mkubwa sana nilivyoambiwa kuwa nina kansa ya utumbo mpana (colon cancer ) na iko stage IIA. wakaniambia watanitransfer ocean road nianze matibabu mara moja ambapo yatahusisha operation.

Kwakweli toka siku hiyo nimekuwa ni mtu wa kuchanganyikiwa nisijue la kufanya nikiangalia maisha yangu mimi ndio tegemeo la mama yangu huko kijijini pamoja na familia yangu hapa mjini na maisha yangu yanategemea kazi zangu hizi za kutumia nguvu nitawezaje kupata matibabu na hata baada ya matibabu nitaendeshaje maisha yangu, kwanini mungu ameamua kunipatia haya majanga katika umri wangu huu mdogo nikiwa mwenye majukumu mengi na kutegemewa sana na familia yangu ,hata hivyo sina uwezo wa kulaumu wala kujua mpango wa Mungu katika maisha yangu.

Nimeshindwa hata kumjulisha mama yangu kijijini maana najua nitamwongezea msongo wa mawazo tu. Nimejaribu kuwaomba ndugu marafiki msaada ambapo napata ahadi tu bila msaada na siwezi kuwalaumu maana natambua hali zao pia.

Nimekuwa nikitumia dawa ambazo ni za maumivu tu, nikiendelea kutafuta hela za matibabu japo hii hali imeathiri sana sana kazi zangu na kipato changu pia ila sina namna nyingine siwezi kufa nimekaa bora nifie kazini .Hela niliyoambiwa inahitajika kwa matibabu ya awali na operation ni sh.593,000/=ndio ambayo bado nahangaika kuitafuta japo nianze matibabu japo sijui nikiwa kwenye matibabu familia yangu itaishi vipi maana bila kutoka kutafuta chochote hata chakula itakuwa ngumu kupatikana na kazi zangu ni za kutumia nguvu .

Hivyo ndugu zangu NIMEAMUA NIWASHIRIKISHE WATU WENGI ZAIDI KUHUSU TATIZO LANGU MAANA SIWEZI KUJUA NI WAPI NAWEZA KUPATA MSAADA AMA FARAJA.Nimekaa nalo naona msongo wa mawazo unanizidia nimeamua kushirikisha watu naweza pata ushauri, faraja ,matumaini ,kukutana na walio wahi kupata tatizo kama langu na kufarijiana na hata msaada pia kwa atakayeguswa na shida yangu akanichangia atakachojaliwa kikanisaidia pia katika hali yangu ngumu.

Kwa atakaye guswa na hali yangu anaweza kunisaidi atakachojaaliwa chochote namba yangu ni [HASHTAG]#0678856312[/HASHTAG] jina Fidelis peter.nitashukuru sana.

Samahanini sitaweza kuwa online mara nyingi maana naingia kwa kutumia computer ya rafiki yangu sio mara zote naweza kuwa naye karibu nilikuwa na smartphone nikaiuza kutokana na tatizo hilhili ili kusaidia familia maana kazi zangu zimeathirika sana.


Asanteni ,
 
Ocean road kwa matangazo ni bure ila pata mgonywa au umwa uende hapo utajuta kuzaliwa hakuna cha bure pale ndugu zangu watanzani vitu vya bure pale ni vidogo vidogo sana hakuna dawa za kumpa mtu bure pale za bei kubwa utapewa panado hata dawa ya kikohozi benline hawana utaambiwa ukanunue hapo nje duka la dawa na nje inauzwa 14500 ni hatari sana
 
Pôle sana mkuu ni sehemu ya maisha ila ingekuwa vizuri ukapost vielelezo /documents Za diagnosis na refferal hapo itakuwa rahisi watu kukusaidia maana siku hizi utapeli umekuwa mwingi watu si rahisi kuamini bila hizo nyaraka
 
Back
Top Bottom