Dunia ni gereza la roho za wafu

Dunia ni gereza la roho za wafu

Ambokile Amanzi

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2018
Posts
961
Reaction score
1,333
Binadamu huzaliwa, hukua, na hufa. Lakini binadamu huyu huzaliwa pasipo ufahamu wa chanzo chake na kuvaa umbo la mwili lililotengenezwa kwa yai la mama na mbegu ya baba.

Kabla hatujaendelea na uchambuzi wa mada, unaweza kujiuliza maswali yafuatayo ;

Je, kabla ya kuzaliwa ulikuwa wapi?

Je, ni kitu gani kinakufanya uhisi kuwa wewe ni wewe?

Je, kwanini hauhisi kwamba wewe sio yule mwingine, lakini wewe ni wewe?

Kitu gani kinakufanya kuwa wewe?

Je, wewe ni nani? Wewe ni mwili? wewe ni hisia ya kujisikia kuwa wewe ni wewe?

Je, ukifa, wewe unakwenda wapi?

Je, maiti yako ni wewe?

Baada ya maswali machache ya falsafa juu ya chanzo cha binadamu, tunabaini kuwa, binadamu ni viumbe wanaozaliwa na kufa, na huzaliwa tena na tena katika namna tofauti, miili tofauti, na maeneo tofauti katika mchakato uitwao incarnation.

Mwili wa binadamu unapokufa, nguvu au nafsi hai inatoka ndani ya mwili na kupitia mchakato mpya wa kutafuta makazi ndani ya mwili mwingine.

Nafsi zetu zimefungwa na adhabu endelevu ya karma ambayo inatufanya tuyalipe matendo yetu katika miili mipya baada ya kufa na kuzaliwa upya.

Baada ya kufa, nafsi yako itachagua maisha ambayo yatakulipa kisasi ama yatakurudishia wema kwa kadiri ya maisha yako kabla ya kifo. Kama ulikuwa muuaji katika maisha ya mwanzo, basi baada ya kuzaliwa upya nafsi yako itachagua maisha ya mtu mpya mwenye hali ya unyonge ili kusudi uadhibiwe kwa kisasi kile kile cha mauaji.

Vivyo hivyo, maisha ya sasa ya mtu mnyonge yatalipwa kwa wema na furaha katika maisha yajayo ndani ya mwili mpya.

Hii ndio dhana ya karma, ambayo huenda ina uhusiano wa moja kwa moja na mafundisho ya mbingu na jehanamu. Ama msemo wa wahenga usemao " malipo ni hapa hapa duniani" . Kimsingi, nafsi zetu zinachukua miili mipya kulipa karma kwa kadiri ya matendo yetu.

Incarnation inapotokea, nafsi yako inakuwa imeshafahamu maisha yako yote yajayo katika mwili mpya, na hivyo kukufanya upitie hatua zote za hatma yako. (destination).

Mchakato huu, unahusiana moja kwa moja na kitu kinachoitwa DEJA'VU, yaani kumbukizi zinazompata mtu ghafla na kutambua kuwa anafanya mambo ambayo alishakwisha kuyafanya.

Kumbukumbu hizi za DEJA'VU zinatupa taarifa kuwa maisha yetu yalishachorwa na nafsi zetu kabla hatujaja duniani. Huu ni ufunuzi wa kiroho unaotukumbusha kuwa tunapitia mambo ambayo yalishakwisha kuonwa na kupangiliwa.

Binadamu ni roho zilizotekwa ndani ya gereza la dunia, na ni roho ambazo zitaendelea kuja tena na tena katika miili tofauti ili kulipa KARMA na ku-experience maisha mapya tofauti na yale kabla ya kifo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binadamu huzaliwa, hukua, na hufa. Lakini binadamu huyu huzaliwa pasipo ufahamu wa chanzo chake na kuvaa umbo la mwili lililotengenezwa kwa yai la mama na mbegu ya baba.

Kabla hatujaendelea na uchambuzi wa mada, unaweza kujiuliza maswali yafuatayo ;

Je, kabla ya kuzaliwa ulikuwa wapi?

Je, ni kitu gani kinakufanya ujisikia kuwa wewe ni wewe?

Je, kwanini hauhisi kwamba wewe sio yule mwingine, lakini wewe ni wewe?

Kitu gani kinakufanya kuwa wewe?

Je, wewe ni nani? Wewe ni mwili? wewe ni hisia ya kujisikia kuwa wewe ni wewe?

Je, ukifa, wewe unakwenda wapi?

Je, maiti yako ni wewe?

Baada ya maswali machache ya falsafa juu ya chanzo cha binadamu, tunabaini kuwa, binadamu ni viumbe wanaozaliwa na kufa, na huzaliwa tena na tena katika namna tofauti, miili tofauti, na maeneo tofauti katika mchakato uitwao incarnation.

Mwili wa binadamu unapokufa, nguvu au nafsi hai inatoka ndani ya mwili na kupitia mchakato mpya wa kutafuta makazi ndani ya mwili mwingine.

Nafsi zetu zimefungwa na adhabu endelevu ya karma ambayo inatufanya tuyalipe matendo yetu katika miili mipya baada ya kufa na kuzaliwa upya.

Baada ya kufa, nafsi yako itachagua maisha ambayo yatakulipa kisasi ama yatakurudishia wema kwa kadiri ya maisha yako kabla ya kifo. Kama ulikuwa muuaji katika maisha ya mwanzo, basi baada ya kuzaliwa upya nafsi yako itachagua maisha ya mtu mpya mwenye hali ya unyonge ili kusudi uadhibiwe kwa kisasi kile kile cha mauaji.

Vivyo hivyo, maisha ya sasa ya mtu mnyonge yatalipwa kwa wema na furaha katika maisha yajayo ndani ya mwili mpya.

Hii ndio dhana ya karma, ambayo huenda ina uhusiano wa moja kwa moja na mafundisho ya mbingu na jehanamu. Ama msemo wa wahenga usemao " malipo ni hapa hapa duniani" . Kimsingi, nafsi zetu zinachukua miili mipya kulipa karma kwa kadiri ya matendo yetu.

Incarnation inapotokea, nafsi yako inakuwa imeshafahamu maisha yako yote yajayo katika mwili mpya, na hivyo kukufanya upitie hatua zote za hatma yako. (destination).

Mchakato huu, unahusiana moja kwa moja na kitu kinachoitwa DEJAVU, yaani kumbukizi zinazompata mtu ghafla na kutambua kuwa anafanya mambo ambayo alishakwisha kuyafanya.

Kumbukumbu hizi za DEJAVU zinatupa taarifa kuwa maisha yetu yalishachorwa na nafsi zetu kabla hatujaja duniani. Huu ni ufunuzi wa kiroho unaotukumbusha kuwa tunapitia mambo ambayo yalishakwisha kuonwa na kupangiliwa.

Binadamu ni roho zilizotekwa ndani ya gereza la dunia, na ni roho ambazo zitaendelea kuja tena na tena katika miili tofauti ili kulipa KARMA na ku-experience maisha mapya tofauti na yale kabla ya kifo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante kwa post fikirishi... Ni wachache wanaweza kuelewa umeandika nini

Jr[emoji769]
 
Mwanadamu anaweza akaandika na kutafakari kwa namna nyingi awezavyo juu ya asili yake, uwepo wake na hata hatma yake...

Katika fakari zote kila moja kwa jinsi yake, zote huishia kukiri uwepo wa 'super natural powers beyond our ordinary powers'...
 
Hili ndio tatizo la Waafrika wengi I,e kile ulichoaminishwa tangu utotoni unajua basi ndio mwisho wa maarifa_hauko tayari kupokea elimu mpya.pathetic

Sent using Jamii Forums mobile app
Waafrika hatuko tayari kujifunza vitu vipya na ndio maana hadi leo tumebaki nyuma sana! Hili jambo hata wapigania haki za mtu mweusi kule Ughaibuni linawakatisha sana tamaa. Mimi hiki naona kama ni Kilema na Laana!
 
Mwanadamu anaweza akaandika na kutafakari kwa namna nyingi awezavyo juu ya asili yake, uwepo wake na hata hatma yake...

Katika fakari zote kila moja kwa jinsi yake, zote huishia kukiri uwepo wa 'super natural powers beyond our ordinary powers'...
Waafrika tumekuwa nyuma siku zote sababu ya mtazamo wa kijinga kama wako! Fikra hizi zinaonesha ni mamna gani tusivyo "Curious" ma ndio maana hata kiwango chetu cha ubunifu ni duni sana sababu kwetu ukuu wa Mungu tunauconfuse na mambo yasiyohusiana.
 
Vizuri sana mkuu.

Kwa iyo mimi maisha magumu ninayoishi ina maana ni karma?

Yani nilifanyaga mabaya uko nyuma ..sasa nawezaje kujua uko nyuma niliishigii?

Sent using Jamii Forums mobile app
inawezekana kabisa ni karma na inawezekana pia kabla ya kifo chako uliishi maisha ya kifahari dunia nyingine au bara lingine, na kwamba nafsi yako ilinuia ku-experience maisha ya ufukara katika mwili mpya.

Hauwezi kufahamu kuwa uliishi maana memory yako inafutwa kabisa kukuwezesha kuishi maisha mapya bila marue rue ya kale.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu umeongea vitu vyamaana xana, it makes sense,kwa maana sometimes mtu unaweza ona, hisi kitu, afu ukahisi km ushawahi kukiona au fanya hapo kabla japo ni kwa Mara yakwanza kuexperience

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii inaitwa Deja'Vu. Unafanya jambo ambalo unahisi kabisa ulishawahi kuliona unalifanya katika namna ile ile.

Hapo nafsi yako inakufunulia kuwa, maisha yako yalishachorwa na kupangiliwa kabla haujazaliwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanadamu anaweza akaandika na kutafakari kwa namna nyingi awezavyo juu ya asili yake, uwepo wake na hata hatma yake...

Katika fakari zote kila moja kwa jinsi yake, zote huishia kukiri uwepo wa 'super natural powers beyond our ordinary powers'...
Hii inawezekana kabisa. Lakini pia huenda nafsi zetu ndio Mungu mwenyewe ndani ya miili yetu.

Ukirejelea maswala ya dejavu utaona ni namna gani tunaishi katika maisha yaliyopangiliwa kabla hatujazaliwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
haya maswali yote yanatokana na kwamba bibadamu tumeshindwa kuukubali ukweli mchungu kuhusu kifo, ndio maana tunatengeneza nadharia kibao za kufikirika ili kujifariji kuwa kuna cha zaidi baada ya kifo.
lakini ukweli unabaki palepale, binadamu ni myama kama wanyama wengine, kabla ya kuzaliwa haukuwepo kabisa, kuwa conscious kuwa wewe ni wewe haipo kwa binadamu pekee hata sokwe na tembo wanahuo uwezo. baada ya kifo it's over!

N.B ushauri wangu,
usivumilie upuuzi na dhiki duniani kwa kujipa moyo kuwa utaenda "kula bata" baada ya kifo, haya ndio maisha yako pekee hivyo basi jaribu kuhakikisha you get the best out of it. Nchi nyingi masikini zinaendelea kuoza kwenye umasikini na siasa za hovyo kwakuwa watu wake hawaoni umuhimu wa kupambana kubali hali kwani wanaamini wataenda "kupumzika" paradiso/peponi. Haya ni mawazo ya kikoloni yaliyoletwa na wanyonyaji wetu ili wao wafaidi maisha wakati sisi tunangojea kufaidi baada ya kifo.
 
Binadamu huzaliwa, hukua, na hufa. Lakini binadamu huyu huzaliwa pasipo ufahamu wa chanzo chake na kuvaa umbo la mwili lililotengenezwa kwa yai la mama na mbegu ya baba.

Kabla hatujaendelea na uchambuzi wa mada, unaweza kujiuliza maswali yafuatayo ;

Je, kabla ya kuzaliwa ulikuwa wapi?

Je, ni kitu gani kinakufanya ujisikia kuwa wewe ni wewe?

Je, kwanini hauhisi kwamba wewe sio yule mwingine, lakini wewe ni wewe?

Kitu gani kinakufanya kuwa wewe?

Je, wewe ni nani? Wewe ni mwili? wewe ni hisia ya kujisikia kuwa wewe ni wewe?

Je, ukifa, wewe unakwenda wapi?

Je, maiti yako ni wewe?

Baada ya maswali machache ya falsafa juu ya chanzo cha binadamu, tunabaini kuwa, binadamu ni viumbe wanaozaliwa na kufa, na huzaliwa tena na tena katika namna tofauti, miili tofauti, na maeneo tofauti katika mchakato uitwao incarnation.

Mwili wa binadamu unapokufa, nguvu au nafsi hai inatoka ndani ya mwili na kupitia mchakato mpya wa kutafuta makazi ndani ya mwili mwingine.

Nafsi zetu zimefungwa na adhabu endelevu ya karma ambayo inatufanya tuyalipe matendo yetu katika miili mipya baada ya kufa na kuzaliwa upya.

Baada ya kufa, nafsi yako itachagua maisha ambayo yatakulipa kisasi ama yatakurudishia wema kwa kadiri ya maisha yako kabla ya kifo. Kama ulikuwa muuaji katika maisha ya mwanzo, basi baada ya kuzaliwa upya nafsi yako itachagua maisha ya mtu mpya mwenye hali ya unyonge ili kusudi uadhibiwe kwa kisasi kile kile cha mauaji.

Vivyo hivyo, maisha ya sasa ya mtu mnyonge yatalipwa kwa wema na furaha katika maisha yajayo ndani ya mwili mpya.

Hii ndio dhana ya karma, ambayo huenda ina uhusiano wa moja kwa moja na mafundisho ya mbingu na jehanamu. Ama msemo wa wahenga usemao " malipo ni hapa hapa duniani" . Kimsingi, nafsi zetu zinachukua miili mipya kulipa karma kwa kadiri ya matendo yetu.

Incarnation inapotokea, nafsi yako inakuwa imeshafahamu maisha yako yote yajayo katika mwili mpya, na hivyo kukufanya upitie hatua zote za hatma yako. (destination).

Mchakato huu, unahusiana moja kwa moja na kitu kinachoitwa DEJAVU, yaani kumbukizi zinazompata mtu ghafla na kutambua kuwa anafanya mambo ambayo alishakwisha kuyafanya.

Kumbukumbu hizi za DEJAVU zinatupa taarifa kuwa maisha yetu yalishachorwa na nafsi zetu kabla hatujaja duniani. Huu ni ufunuzi wa kiroho unaotukumbusha kuwa tunapitia mambo ambayo yalishakwisha kuonwa na kupangiliwa.

Binadamu ni roho zilizotekwa ndani ya gereza la dunia, na ni roho ambazo zitaendelea kuja tena na tena katika miili tofauti ili kulipa KARMA na ku-experience maisha mapya tofauti na yale kabla ya kifo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hatari sana .... Tuna tumika tu "

Huyu anaye tutumia dhumuni lake haswa ni nini " !?
Maana tumeweza kuona kuwa tumekuja duniani bila ya ridhaa yetu ...

So wataka kuniambia kuwa huwenda mimi niliishi mwaka 1652

Sent using Jamii Forums mobile app
 
inawezekana kabisa ni karma na inawezekana pia kabla ya kifo chako uliishi maisha ya kifahari dunia nyingine au bara lingine, na kwamba nafsi yako ilinuia ku-experience maisha ya ufukara katika mwili mpya.

Hauwezi kufahamu kuwa uliishi maana memory yako inafutwa kabisa kukuwezesha kuishi maisha mapya bila marue rue ya kale.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mhh hapa umegusia huu mfano ... unafanana kabisa na wale binaadamu wa maabara human cloning maana na wao huwa wanakuwa hawana kumbu kumbu " kuwa chanzo chao alikuwa ninani !?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hatari sana .... Tuna tumika tu "

Huyu anaye tutumia dhumuni lake haswa ni nini " !?
Maana tumeweza kuona kuwa tumekuja duniani bila ya ridhaa yetu ...

So wataka kuniambia kuwa huwenda mimi niliishi mwaka 1652

Sent using Jamii Forums mobile app
Huenda wewe ni hayati katika dunia nyingine. Na huenda ulishakufa zaidi ya mara mia mbili huko nyuma.

Nafsi yako inavaa miili mipya kila baada ya kifo ili ku-experience maisha ya aina fulani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom