Dunia inazungukaje?

nimetaka aya ambayo Allah anajisifia ufundi wa kuumba alafu hilo liwe linamaanisha
Huu sio msingi katika kufasiri Qur'aan na ndio maana nilikwambia huko nyuma aya hufasiriwa kulingana na muktadha na mtiririko ulivyo na kutokana na athari,ndio maana nimekuwekea hiyo aya ili ujue na uone kwamba hicho unachokiulizia sio msingi na hakipo.

Soma aya angalia wanazuoni wamefasiri kutoka kwa mtume au kwa maswahaba.

Ndio maana nakuuliza hivi huo msingi unao usema umeutoa wapi ? Naomba ujibu hili swali.
 
kwani hayo maarifa mapana wewe unayapimaje ?

kwani kufasiri Qurani kunataka uwe na maarifa mapana kumbeeee...?
Kunataka maarifa mapana hasa,na usomeshwe,huoni kwamba watu huwa wanafundishwa misingi ya kutafsiri Qur'aan na kusomeshwa Tafsiri ya Qur'aan.

Nayapima kwa kuwaangalia wanachuoni wakubwa ambao wamethibitishwa ya kuwa wao ni wanachuoni kutoka kwa wanachuoni wa kubwa.
 
kabla ya yote naomba uniambie hasa hyo namba 3 kwa ushahidi upi au kwa mujibu wa nani..?
Asili ya hili ni kutoka kwa mtume,ukisoma fani ya Tajweed utakutana na jadithi ya mtume inayosema ukitaka kuisoma Qur'aan basi soma kama anavyoisoma "Ibn Amiiy" akimkusudia swahaba Abdullah Ibn Mas'oud hii ndio inaitwa ijaza.

Allah anasema waulizeni wanao fahamu kama nyinyi hamfahamu,na tunasomewa ya kuwa wanachuoni ni warithi wa mitume.

Na hili utalikuta kwa maswahaba pia,kwa maana walikuwepo maswahaba ambao ni wasomi wakubwa na wenye kutoa fatwa,hawa ulikuwa unaelekezwa kabisa kwamba ukitaka majibu kuhusu jambo fulani mfate fulani.

Hili likaenda mpaka kwa matabiina,ukisoma athari utaona hili kwa Imaam Atwaa bin Abi Rabaha,ilifikia hatua mtawala akasema haruhusiwi mtu kutoa fatwa hapa makka isipokuwa Atwaa na yeye Atwaa alikuwa ana kaimu kiti cha Sayyid bin Jubeir kama sikosei na huyu Atwaa alisoma kwa mama Aisha na Abdullah Ibn Abbas Allah awaridhie,kwa maana wasomi walijulikana na nafasi yao ilikuwa wazi,na hii ni kutokana na ikhlaswi yao na maarifa yao makubwa.

Sababu elimu huenda kwa kurithishana hilo limetufikia mpaka kwetu sisi na litaendelea.

Kwahiyo namba 3 ina asili toka kwenye Qur'aan,kutoka kwa mtume ikafanyiwa kazi na maswahaba kisha matabiin na kisha waliowafata wao mpaka imetufikia sisi.
 
alafu unaporuia kusema eti awe amekubaliwa na wanachuoni wakubwa hapa ndo sifa hii ?

hao wanachuoni wakubwa wanasifa gani ?
Hii ni sifa anuai,kwani imeanzia huko kwa mtume mpaka imetufikia sisi. Hao wanachuoni wakubwa kabla ya kuwa hovyo na wao walikuwa na wakubwa zao. Kwahiyo ni juu yako kulifikiria hilo kiutu uzima,kwani na wao hao kabla walipota katika mchujo huo huo.

Mtume alikuwa anawaweka watu katika nafasi zao.
 
Kuna group la wanasayansi wakipakistan waliwachallenge NASA kuwa dunia sio shape ya duara/sphere.NASA wala hawakujibu chochote,
Mi naona waliwaona hao jamaa wana akili ndogo sana.Ok na wewe njoo na evidence uwa challenge wanasayansi,sio maneno tu
 
Huwezi kupata majibu ya swali lako hapa! Jitahidi kusoma Physics utajua!

Wewe uliyedoma Physics ukaelewa si ndio wakati muafaka wa kudafavua na kutunisha kifua kutuelewesha?

Siamimi ulipoteza muda kusoma Physics.
 
Huu mfano wako bado haujakidhi tafari zetu.

Ukirusha jiwe litashuka ktk mkono coz mkono haumove, kinachomove ni gari.

Tulete huu mfano wa mtu kuwa ndani ya ndege na dunia, kwa kasi inayokimbia dunia 10,000km/h hakuna chombo ambacho kingetoka nje ya huu ulimwengu theni kikarudi sehemu ile ile husika.
 
Akishajibu hili swali twaweza endelea na mada, dunia kweli izunguke 10,000km kwa Lisaa limoja na sisi tusihisi chochote?
 
Hii ya leo kali, jua halizunguki mkuu?
 
Uwe unanukuu matini ya kiarabu au kuweka tarjama hivi unakuwa unapoteza maana ya aya,kwani unaandika kinyume na ilivyo matini.



و قال الرسول يا رب إن قومي أتخذوا هذا القران مهجورا

(25:30).
 
Nani alikwambia jua lina kiini na joto ridi lake ni 1,000,000 deg C ? Walipima joto hilo kwa kutumia kifaa gani na nani alikuwa wa kwanza katika hilo ?


Kweli tupo na mtu wa karne ya 10 wakati leo karne ya 21, hata Treni ya SGR ya Magufuli ukiiona kwa macho ikifanya kazi hutoamini kama inafanya kazi hadi uipande.

Kaka, naishia hapo, kiwango cha elimu yako ni kidogo mno kuweza kujua nitakacho kuelewesha.


Jua linatoa nishati ya kinyuklia nishati za nyuklia zipo za aina 2, moja inatokana na fission reaction, na ya pili inatokana na fusion reaction, katika jua ni hii ya pili, yaani Hydrogen gas inareact kuwa Helium gas ( thermal nuclear reaction) hapo huzalishwa, joto kubwa mno, Miale gamma rays nk, Mwanga nk, Makombora yote ya nyuklia ya siku hizi yanaitwa thermo nuclear/hydrogen bomb kwasababu katika hatua ya kulipuka hatua ya katikati wameweka hydrogen na inapolipuka (kama reaction ya kwenye jua) inazalisha Helium gas na Joto kali mno na Neutrons nyingi ili kuelekea hatua ya 3 na ya mwisho ya mlipuko, sasa ni hivi ile reaction KAMA ya kwenye jua watu tumeweza kuitekeleza hapa duniani na kuweza kupima joto la kiini cha mlipuko kwa kutumia kifaa cha mbali (thermometer) inayojulikana kama "Pyrometer"--- leo zipo pyrometers za kisasa mno zinazotumia digital na kuunganishwa kwenye computer mithili yake ni kama zile zinazotumika mipakani kupima joto la watu ili kutambua uwezekano kama wana homa ya Ebola, kifaa hicho kinapima joto kwa mbali bila kugusa kitu kinachopimwa.

Nimeamua kuandika hivi kwa uchache lakini nimehuzunika sana. Na kujadiliana nawe katika mambo haya ni kupoteza muda, kwasababu unahoji vitu "very basic" anavyoweza kuhoji mtoto wa darasa la pili au mtu wa karne ya 13.

Alrasulullah (saw) alisema; tafuteni elimu hadi China. China hakuna elimu ya dini.
 



Kama wewe kaka umehuzunika, basi mimi ndio zaidi, mambo hayo unayoyauliza walianza kuyafanyia kazi Mababu zako wa Kiislamu (wanasayansi) kabla ya hawa wazungu wa karne ya 19 hawajashika Kasi.

Kauli yangu ya mwanzo kutaka kujua kiwango cha Elimu yako ya Secular hapa ndiyo kime- materialise.

Maswali hayo ni mepesi kama unajua kiwango "Mathematics+Phydics"--- hizo ni nyenzo zinazomfanya Mzungu leo aitawale dunia, hadi leo Zurri unapanda ndege na Magari na upo na Laptop au Smartphone tuna chart hapa,---- hiyo yote ni Maths na Physics.

Leo unauliza eti uzito wa dunia unapimwaje??, karne ya 21.🤣, halafu hujui unaamua kusema, eti, huo ni UONGOOOO !!!


M=gr²/G , where M, mass of the earth, g ni acceleration of gravity, r ni radius of the Earth, utauliza r inapatikana vipi???🤣🤣
 


Umeweka tu hapo tarjama bila kuweka tafsiri ili tukuelewe, kama umeshindwa kuweka tafsiri tuwekee tafsir ya ibn kathir tusikie naye anasemaje!!,--- au naye kashindwa kama alivyoshindwa kwenye 21:33, 🤣🤣🤣
 


Umeweka tu hapo tarjama bila kuweka tafsiri ili tukuelewe, kama umeshindwa kuweka tafsiri tuwekee tafsir ya ibn kathir tuone naye anasemaje!!,--- au naye kashindwa kama alivyoshindwa kwenye (21:33), 🤣🤣🤣
 
Kazi kweli kweli,nimekuuliza maswali badala ya kujibu unaleta porojo.

Wewe jibu maswali niliyo kuuliza japokuwa ni mapesi sana.
 
Umeweka tu hapo tarjama bila kuweka tafsiri ili tukuelewe, kama umeshindwa kuweka tafsiri tuwekee tafsir ya ibn kathir tuone naye anasemaje!!,--- au naye kashindwa kama alivyoshindwa kwenye (21:33), 🤣🤣🤣

Ulinichekesha sana,uliposema umefungua tafsiri ya Ibn Kathiir ukatafuta maana ya aya hiyo hukuiona 21 : 33, nikaona wewe sio msomaji na mvivu na huwa husomi Tafsiri za Qur'aan.

Yule ni imaamu,sasa ulizia katika Uislamu unapo ambiwa mtu fulani ni "Imaamu".

Wewe ndio umeshindwa kusoma hiyo Tafsiri,na hiyo aya isome utaikuta humo.
 
Alrasulullah (saw) alisema; tafuteni elimu hadi China. China hakuna elimu ya dini.
Hii Hadithi dhaifu,mtume hajasema maneno haya. Huku ndio usiingie kabisa.

Kaka naomba ujibu maswali yangu tu,mbona rahisi sana.
 


Angalia list ya Wanasayansi wa kiislamu walioijua Qur'an kuliko wewe:-

(1) Avicenna (Abusina)----980 AD---1037

(2) Ibn al Hytham -965AD-1040.
(3) Al kindi -- ---873 AD.
(4) Al zahrawi- 936 AD --1013.
(5) Ibn al Baitar 1197-1248
(6) Abdus salaam 1926---1996
(7) Ibn Battula 1304-1317
(8) Toby Huff
(9) Ibn Sahl 940AD--1000
(10) Perez Hoodboy
(11) Maslama al Majrit 950AD-1007
(12) Abu dahl al Quln 940 AD- 1000
(13) Sl Farabi 872AD--980
(14) Hanayn Ibn Ishaq 809AD--873 AD
(15) Ismail al Jazar 1136--1206.

List ni ndefu sana, na kila mmoja alitoa mchango wake katika nyanja mbalimbali za sayansi, na walikuwa wanaijua Qur'an, sasa unakuja hapa kunajisi Elimu ya kweli ya sayansi.

Vyombo vinaonyesha dunia inajizungusha kwenye mhimili wake na inalizunguka jua, mwezi na dunia siku zote vimeambatana , giza na nuru ni matukio yanayotokea duniani, sasa kama mwezi unazunguka jua utakataaje kwamba dunia haizunguki.

Kitabu adhimu tulichokiteremsha kwako, chenye baraka ili wapate kuzitafakari aya zake, na wenye akili washike nasaha. (38:29).
 
Kaka naomba ujibu maswali yangu tu,mbona rahisi sana.
[/QUOTE]


Sasa kama ni maswali rahisi kwanini uniulize???, umenitega??🤣🤣

Sasa kaka ni mwendo wa kutegana na sio mwendo wa kuelimishana!!!, imekuwa ligi???🤣 kutafuta nani kashinda na nani kashindwa???.

Basi Umeshinda na mimi nimeshindwa. Nadhani umeridhika kaka, tuendelee na maisha.

Ila usiibeze sayansi hata kama "ilikupiga" wewe iheshimu tu, hiyo touch yako ni matokeo ya sayansi.

Kwaheri kaka, nakwenda kutafuta riziki ya watoto.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…