Dunia imejaa watu waongo

Kwani Wewe uovu unaolalamikia hapa kuwa MUNGU kauachilia ni upi?
Na nani kaamua huo ni uovu?
Mungu hajaachilia uovu, na Mungu hawezi kuzuia uovu.

Umesema Dunia ni Mali ya Mungu, ndiyo nikakuuliza kama Dunia ni Mali yake, kwanini aruhusu vita na majanga ya Asili yatokee kwenye himaya yake wakati yeye ni mwenye Upendo wote na nguvu zote?
 
Umesema Dunia ni Mali ya Mungu, ndiyo nikakuuliza kama Dunia ni Mali yake, kwanini aruhusu vita na majanga ya Asili yatokee kwenye himaya yake wakati yeye ni mwenye Upendo wote na nguvu zote?
Ndo nakuuliza wewe humu duniani umefanya maovu mangapi na amekuacha?

Au wewe hujafanya uovu wowote?
 
Tunaweza kuthibitisha AI maana ipo na tunaitumia Kila siku.
Lakini kuthibitisha uwepo wa Mungu bila mikanganyiko ya kimantiki haiwezekani
Ukushasema Mantiki ndo ushamtaja MUNGU hivyo: MUNGU wetu wa milele, habadiliki: sheria za mantiki / kweli (truth) zinaakisi utu wake.

Eternal constants from the Eternal heavens where only TRUTH resides.

Ndomana na bibilia inasema MUNGU ni Kweli. Sio ana kweli, Yani ndio kweli yenyewe.

Ili chochote ki make sense tunamuuliza MUNGU mwenyewe, tunamtegemea yeye kwa kutumia sheria zake za mantiki na sheria zake za milele za maadili.

Yani hadi kumkana MUNGU inabidi MUNGU awepo, asingekuwepo usingekuwa na msingi kumkana: sheria za milele za mantinki.
 
Eti Biblia inasema Mungu ni kweli.
Kwahiyo unakubali Spider man yupo kisa kuna vitabu vinasema hivyo.
 
Eti Biblia inasema Mungu ni kweli.
Kwahiyo unakubali Spider man yupo kisa kuna vitabu vinasema hivyo.
Did spiderman rise from the dead?

And is spiderman's ressurection a provable historical fact beyond reasonable doubt, like JESUS' resurrection?
 
Mfano mimi huyo Mungu nimemkosea kiasi gan hata nistahili haya? Nina 27yrs lakin hakuna langi sijaona nimezaliwa nikakuta familia isioeleweka ,iliyojaa migogoro ,nikaozeshwa nikiwa bado mdogo kwa mwanaume ambaye hata sikua namjua kwa namna yoyote na hata sikumpenda ,ndoa nayo ikawa chungu familia iliyonilazimisha kuolewa haina msaada wowote watu hapo ni kwa kifupi ,kosa langu ni lipi hasa ?hii dunia imelaaniwa na haina faida kama kifo ni suruhu kher nijifie taratibu mamaeee
 
Yote uliyoyasema ni sahihi.
Pole kwa unachokipitia kwa sasa!
 
kama kungekua na option ya kuchagua uzaliwe au usizaliwe ningechagua kutokanyaga kwenye dunia hii iliyojaa watu
Utachaguaje Sasa wakati ujazaliwa eti Kiranga huyu jamaa vipi unawezaje kichagya uzaliwe au usizaliwe wakati hujui HATA kama Kuna KITU kinaitwa ubongo.


Naamini mtoa MADA hajaelewa ila Kiranga namsubiri
 
Pamoja na yote hayo mkuu anakuja mtu anakwambia Maisha yetu yote Mungu anajua mwanzo na mwisho, yaani Mungu ameshapanga tutazaliwa vipi mpaka kifo chetu kitakuwaje.
Kwahiyo matatizo yote unayopitia Mungu alishapanga uyapitie 🤣🤣 Mungu amekupangia upate joto la jiwe mpaka useme 🤣
 
Me nina 30 nimeshaenda kuzimu na kurudi hapa hapa duniani, yani cha moto nimekiona.

Kwa kifupi hakuna pigo halijanipiga, kutoka kila kona. Si magongjwa, si uchumi, si mahusiano, labda kifo tu nimeepushwa sijafa, sijafiwa lakini watu hao hao walio hai wanakufanya uone bora ukalale njaa kwenye mti kuliko kuwa karibu nao.

Nikimuangalia Ayubu najiona mimi kabisa.

Maumivu yangu yamenipeleka kwa MUNGU wangu.

Kadri navyoona uovu ndivyo navyouona uso wa MUNGU: yeye ni kinyume kabisa uovu.

Najua kwasababu alishajifunua kwenye sheria zake na kupitia YESU.

Muangalie aliyekuumiza kwa hakika ameenda kinyume na MUNGU alivyoagiza.

Possibly na wewe ushaenda kinyume mara nyingi na umeumiza wengine, na MUNGU alikuacha.

Kwahiyo hii Neema / Rehema uliyoonyeshwa, ielekeze na kwa wengine.

Hawajui walitendalo.

Badala ya kumnyooshea MUNGU kidole, wewe tubu ya kwako,

na kumuomba akuokoe kutoka kwenye hali ngumu / akuondoe kutoka kwa watesi wako.

Utauona mkono wa MUNGU.


"Ni yule mwenye mikono safi na moyo mweupe, yule ambaye hakuinulia sanamu nafsi yake au kuapa kwa kitu cha uongo.

Huyo atapokea baraka kutoka kwa Bwana, na hukumu ya haki kutoka kwa Mungu Mwokozi wake."

Psalm.24.4-5.NENO
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…