Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,971
- Thread starter
- #441
SEHEMU YA 81
Alikuwa na mawazo tele, ubongo wake ulikuwa ukifikiria kupita kawaida. Alipewa muda wa mwezi mmoja kukamilisha deni alilokuwa akidaiwa, hakujua ni mahali gani ambapo angepata kiasi kikubwa namna hiyo na kukilipa.
Alijaribu kuwasiliana na ndugu zake wengine, wote walipogundua tatizo alilokuwa nalo, hata simu hawakuwa wakipokea. Hakuchoka, aliendelea kuwatafuta lakini majibu yalikuwa yaleyale.
Wakati zikiwa zimebaki siku kumi, akajaribu kumpigia simu Edward kwa ajili ya kumuomba msaada wa kisheria zaidi lakini kitu cha ajabu kabisa, mwanaume huyo hakuwa anapokea simu zake na hata alipokuwa akimtafuta ofisini kwake, mwanaume huyo alijifanya kuwa bize na kutokuwa na muda wa kuzungumza na mtu yeyote yule.
Hilo lilimuuma mno moyoni mwake. Edward, mwanaume ambaye kila siku alimwambia kwamba angepigana naye kwa moyo mmoja leo hii hakutaka kupokea simu zake na mbaya zaidi hata alipokwenda kumuona ofisini kwake, hakutaka kabisa kuonana naye.
Hakujua cha kufanya, akarudi nyumbani kwake na kutulia sebuleni. Kila alipokuwa akiwaona watoto wake, mawazo yake yalikuwa ni juu ya maisha ambayo wangeishi baada ya nyumba hiyo kupigwa mnada.
Alikitegemea kiasi cha shilingi milioni mia mbili kilichokuwa kwenye akaunti yake, akahisi kwamba hicho kingemsaidia kuyaendeleza maisha yake, angenunua nyumba ya kawaida kuendelea na maisha yake na watoto wake.
“Mama nimerudi tena!” alisema mwanaume mmoja aliyemfuata nyumbani kwake.
“Eeh! Jamani! Kuna nini tena?”
“Nimekuletea barua!”
“Nyingine?” aliuliza huku akionekana kushangaa.
“Ndiyo! Hii hapa!”
Mwanaume yule akampa barua hiyo. Rosemary alibaki akitetemeka, hakujua ni kitu gani ambacho angekutana nacho katika barua ile. Alipoifungua, maneno ya kwanza aliyokutana nayo ni kuhusu kufungwa kwa akaunti yake ya benki ya mume wake.
“Nini? Wanafunga akaunti?” alijiuliza huku akishtuka kupita kawaida.
Akasoma maelezo kwa kirefu. Benki hiyo iliyokuwa ikimdai mumewe ilieleza kwamba kwa kiasi cha shilingi milioni mia mbili kilichokuwa benki kilitakiwa kuchukuliwa chote na kisha nyumba hiyo kuuzwa kwa bei ya kawaida kwa ajili ya kupata hata nusu ya fedha walizokuwa wakimdai.
Alikuwa na mawazo tele, ubongo wake ulikuwa ukifikiria kupita kawaida. Alipewa muda wa mwezi mmoja kukamilisha deni alilokuwa akidaiwa, hakujua ni mahali gani ambapo angepata kiasi kikubwa namna hiyo na kukilipa.
Alijaribu kuwasiliana na ndugu zake wengine, wote walipogundua tatizo alilokuwa nalo, hata simu hawakuwa wakipokea. Hakuchoka, aliendelea kuwatafuta lakini majibu yalikuwa yaleyale.
Wakati zikiwa zimebaki siku kumi, akajaribu kumpigia simu Edward kwa ajili ya kumuomba msaada wa kisheria zaidi lakini kitu cha ajabu kabisa, mwanaume huyo hakuwa anapokea simu zake na hata alipokuwa akimtafuta ofisini kwake, mwanaume huyo alijifanya kuwa bize na kutokuwa na muda wa kuzungumza na mtu yeyote yule.
Hilo lilimuuma mno moyoni mwake. Edward, mwanaume ambaye kila siku alimwambia kwamba angepigana naye kwa moyo mmoja leo hii hakutaka kupokea simu zake na mbaya zaidi hata alipokwenda kumuona ofisini kwake, hakutaka kabisa kuonana naye.
Hakujua cha kufanya, akarudi nyumbani kwake na kutulia sebuleni. Kila alipokuwa akiwaona watoto wake, mawazo yake yalikuwa ni juu ya maisha ambayo wangeishi baada ya nyumba hiyo kupigwa mnada.
Alikitegemea kiasi cha shilingi milioni mia mbili kilichokuwa kwenye akaunti yake, akahisi kwamba hicho kingemsaidia kuyaendeleza maisha yake, angenunua nyumba ya kawaida kuendelea na maisha yake na watoto wake.
“Mama nimerudi tena!” alisema mwanaume mmoja aliyemfuata nyumbani kwake.
“Eeh! Jamani! Kuna nini tena?”
“Nimekuletea barua!”
“Nyingine?” aliuliza huku akionekana kushangaa.
“Ndiyo! Hii hapa!”
Mwanaume yule akampa barua hiyo. Rosemary alibaki akitetemeka, hakujua ni kitu gani ambacho angekutana nacho katika barua ile. Alipoifungua, maneno ya kwanza aliyokutana nayo ni kuhusu kufungwa kwa akaunti yake ya benki ya mume wake.
“Nini? Wanafunga akaunti?” alijiuliza huku akishtuka kupita kawaida.
Akasoma maelezo kwa kirefu. Benki hiyo iliyokuwa ikimdai mumewe ilieleza kwamba kwa kiasi cha shilingi milioni mia mbili kilichokuwa benki kilitakiwa kuchukuliwa chote na kisha nyumba hiyo kuuzwa kwa bei ya kawaida kwa ajili ya kupata hata nusu ya fedha walizokuwa wakimdai.