Duni Haji: Ndani ya CHADEMA kila mtu ni Kambale

Duni Haji: Ndani ya CHADEMA kila mtu ni Kambale

Huo ni ugatuzi wa madaraka, kukua kwa demokrasia sio makao makuu wajione wao ndio kila kitu, ngazi ya jimbo ndio wanaofahamu mazingira ya eneo na wapo karibu na wanachama husika mambo ya kuamuliwa na makao makuu ni kuchelewesha maamuzi
Wewe ndiyo mwana CHADEMA uliandika kulingana hoja uliopo mezani hongera sana, hivi ndivyo inavyotakiwa kuzijibu hoja na sio kushambuliana nyie mnaojadili. Viva umpinzani viva CCM, hebu chukua Like.
 
Kwani babu duni ni nani nae ni binadamu tu kama wengine pia nae alikuwa kimaslahi zaidi mbona mwanzo hakusema chochote ?kakosa unaibu analeta maneno .Mtasema sana chadema ina wanachama wengi sana ambao hawageuki nyuma .peopleeees .
Powerrrrrrrrr!!!!
 
Ina maana Duni hajui maana ya ugatuzi wa madaraka?. Kuna kitu kakiona hakiko sawa...chama kimejaa majambawazi...kila mtu ni kamanda...
Anaweza kuwa anafahamu, tatizo ni kule kufiri kwamba maamuzi yakitoka juu hayawezi kujadiliwa na kutolewa maoni tofauti na ngazi ya chini, mnaposigana ndio kukua kwa demokrasia, kama itakua maamuzi ya ngazi ya taifa yakishuka chini ni ndiooo!!, tutajenga utamaduni wa kikundi cha sekretariet kuwa ndio kila kitu, mazingira ya dar ni tofauti na mbeya, ni tofauti na mtwara, tofauti na mwanza n.k. na hii imesaidia chama kukua wanaosubiri mawazo ya katibu mkuu ndio yaendeshe chama wanajua wapo wapi mpaka sasa ktk kukijenga chama
 
Katika mahojiano yake na Azam TV Babu Duni ambaye juzi amerudi CUF amesema kuwa ndani ya CHADEMA kila mtu ni kambale.

Babu Duni amesema kwamba kuna bureaucracy kubwa sana ndani ya CHADEMA kiasi kwamba agizo linalotoka juu ngazi ya Taifa linaweza kukataliwa na ngazi ya jimbo kwakuwa kila mtu ana sharubu.

My Take: Babu Duni alikuwa akiwachora CHADEMA na ameona ni chama ambacho hakijawa tayari kuongoza nchi kwakuwa mfumo wake wa kiutendaji ndani ya chama ni 'chaos', je hawa watu tukiwapa nchi si haitatawalika kwakuwa kila mtu/kiongozi atakuwa ni kambale?. CHADEMA mrudisheni Dr Slaa aimarishe chama...

Source: Azam news ya saa 2 usiku.
Haji Duni akosoa Muundo wa CHADEMA. Aliyekuwa mgombea Mwenza wa Rais kwa tiketi ya CHADEMA, Juma Haji Duni ambaye wiki hii amerejea katika chama chake cha awali cha CUF amekosoa muundo wa uongozi wa chama hicho alichojiunga nacho mwaka jana ili kutimiza matakwa ya sheria na taratibu za uchaguzi mkuu.Akiongea katika mahojiano maalum na kituo cha runinga cha Azam Two, Duni ameeleza kuwa muundo wa uongozi wa CHADEMA una urasimu mkubwa unaosababisha kila kiongozi katika ngazi fulani kujiona mkubwa na anayeweza kutoa maamuzi yake.

“Ule muundo wake wa kiutawala ni mkubwa mno, bureaucracy ni ndefu sana kiasi kwamba kila mmoja kule ni kambare ana sharubu. Kule kuna [ngazi]Taifa, kuna Kanda, kuna Mkoa, kuna Wilaya, kuna Jimbo. Sasa uamuzi unaweza ukatoka Taifa lakini mtu wa Jimbo akasema huo uamuzi mimi siukubali,” alisema Haji Duni.Alisifafanua kuwa muundo huo mrefu wa uongozi unachelewesha na kukwamisha maamuzi yatokayo katika ngazi ya Juu.Katika hatua nyingine, Mwanasiasa huyo alisisitiza kuwa kuna faida kubwa waliyoipata kutokana na kuunda Ukawa na kwamba ndio njia pekee ya kuiondoa CCM madarakani.

“Kitu kimoja ambacho nakiamini ni kwamba bila Ukawa hatuwezi kuiondoa CCM. Na matokeo ya mwaka huu yameonesha kwamba Chama cha CUF hakijawahi hata mara moja kwa miaka 20 iliyopita kupata viti vingi bara, kupata madiwani wengi Bara na kupata Halmashauri hadi Halmashauri ya Tanga ambayo tumenyang’anywakwa nguvu,” alisema.Alifafanua kuwa hali hiyo inaonesha dhahiri kuwa wapinzani wakishirikiana wanaweza kuiondoa CCM madarakani.



Source: Baqir Media
 
WanaCCM waacheni Chadema Na mambo yao mbona CCM MNA misukosuko mingi ? Mngetumia muda mwingi kusema yenu , wabunge wenu wala Rushwa , majipu ni Wanaccm, ili mradi kila uozo wa nchi ni ccm
Aliyeongea hayo ni Juma Duni Haji mwanachama wa CUF na sio CCM..kuwa muelewa
 
Naliona anguko KUU la Ukawa kabla ya 2020
 
Tatizo maamuzi yanayotolewa na hiyo ngazi ya taifa hayashirikishi ngazi za chini sasa unategemea nini?

Ni mkutano gani ulikaa ukaazimia kuunda UKAWA? Wajumbe gani walishiriki? Waliazimia nini?

Lowassa alipitishwa kugombea na akina nani? Kwa utaratibu upi?
Lazima tukubaliane kwamba kuna tatizo katika uongozi wa cdm..kuna mungumtu pale ambae ana vibaraka wake yeye akiguswa tu silaha yake kubwa ni kumwita "msalati"aliyekosana nae.Baada ya hapo "nyumbu" wote wanapaza sauti ya msalitiiiii
 
Lazima tukubaliane kwamba kuna tatizo katika uongozi wa cdm..kuna mungumtu pale ambae ana vibaraka wake yeye akiguswa tu silaha yake kubwa ni kumwita "msalati"aliyekosana nae.Baada ya hapo "nyumbu" wote wanapaza sauti ya msalitiiiii
Hili ndiyo tatizo KUU....
 
WanaCCM waacheni Chadema Na mambo yao mbona CCM MNA misukosuko mingi ? Mngetumia muda mwingi kusema yenu , wabunge wenu wala Rushwa , majipu ni Wanaccm, ili mradi kila uozo wa nchi ni ccm
CHADEMA ni kama gheto,unaweza kulala na viatu.
 
CDM ya sasa kuna "wazawa" na "wakuja" kila mmoja anamsikiliza "boss" wake ....kila mmoja anakibesi ....wengine wameamua kupiga kimya tu ....
Mkuu hapo ume mnukuu Mh Muhongo "Kuna Wazawa Na wakuja" Au MATAPELI
 
Katika mahojiano yake na Azam TV Babu Duni ambaye juzi amerudi CUF amesema kuwa ndani ya CHADEMA kila mtu ni kambale.

Babu Duni amesema kwamba kuna bureaucracy kubwa sana ndani ya CHADEMA kiasi kwamba agizo linalotoka juu ngazi ya Taifa linaweza kukataliwa na ngazi ya jimbo kwakuwa kila mtu ana sharubu.

My Take: Babu Duni alikuwa akiwachora CHADEMA na ameona ni chama ambacho hakijawa tayari kuongoza nchi kwakuwa mfumo wake wa kiutendaji ndani ya chama ni 'chaos', je hawa watu tukiwapa nchi si haitatawalika kwakuwa kila mtu/kiongozi atakuwa ni kambale?. CHADEMA mrudisheni Dr Slaa aimarishe chama...

Source: Azam news ya saa 2 usiku.
 
Katika mahojiano yake na Azam TV Babu Duni ambaye juzi amerudi CUF amesema kuwa ndani ya CHADEMA kila mtu ni kambale.

Babu Duni amesema kwamba kuna bureaucracy kubwa sana ndani ya CHADEMA kiasi kwamba agizo linalotoka juu ngazi ya Taifa linaweza kukataliwa na ngazi ya jimbo kwakuwa kila mtu ana sharubu.

My Take: Babu Duni alikuwa akiwachora CHADEMA na ameona ni chama ambacho hakijawa tayari kuongoza nchi kwakuwa mfumo wake wa kiutendaji ndani ya chama ni 'chaos', je hawa watu tukiwapa nchi si haitatawalika kwakuwa kila mtu/kiongozi atakuwa ni kambale?. CHADEMA mrudisheni Dr Slaa aimarishe chama...

Source: Azam news ya saa 2 usiku.
Hao hao ndio mlikuwa mnasema Mboye akishasema jambo hakuna wa kumpinga eti chama ni chake, nilitegemea mngetumia nguvu ileile kumpinga Babu Duni kwa hoja zilie zile za kuwa chama ni cha Mboye akitoa agizo hakuna wa kumpinga lkn nashangaa leo mnaunga mkono tena eti chama hakina mdogo wote ni kambare, km ndivyo inapendeza coz hakuna kubruzana hapo kila mmoja ana power.
 
Hii ina dhiirisha CHADEMA haina mwenyewe[emoji106] [emoji106] [emoji1]
 
Back
Top Bottom