Duka la kwanza pekee la asali mjini morogoro

Duka la kwanza pekee la asali mjini morogoro

cheseo

Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
80
Reaction score
21
Salam wakuu, napenda kutambulisha kwenu duka la kwanza na pekee la ASALI halisi na bora toka HONEY SPRING. duka lipo katika ghorofa la LOTTOS mkabala na ofisi za bima.
Asali hii inatoka mkoani TABORA na tunauza ASALI YA NYUKI WAKUBWA na ASALI YA NYUKI WADOGO pia katika ujazo tofauti.

bei zetu ni;-
ASALI YA NYUKI WAKUBWA( WAKUBWA CLASSIC)
LITA 1- 12,000
350ml-5000

ASALI YA NYUKI WADOGO
LITA 1-35,000
NUSU LITA-20,000
350ml-15,000

wale mliopo mkoani DAR ES SALAAM na MOROGORO pia unaweza piga simu namba 0683370065 au 0769129351 na ukatoa order yako na utaletewa sehemu utakayoelekeza ulipo.
karibuni sana,

ujumbe;- VIJANA TUINGIE KWENYE UJASRIAMALI KWANI UNALIPA, ANZA KIDOGO NA UTAFANIKIWA.
 

Attachments

  • duka.jpg
    duka.jpg
    60.7 KB · Views: 181
  • duka 2.jpg
    duka 2.jpg
    56.4 KB · Views: 200
Hongera sana kwa kuuza BIDHAA zetu Mkuu. Nina imani hamuwalalii sana Wanyamwezi wangu hapa Sikonge.
 
Doh aisee hapo watakua wameua, watoke kwenye mafuta ya ubuyu hadi kwenye asali? Ntaenda kulia kwa PINDA
 
Asante sana mkuu, hakuna kulalia sku hizi maana wanapata elimu ya jinsi asali ilivyo mali
 
mbona mara nyingi hapo dukani akunaga mtu,japo duka lipo wazi?nimeshakuja zaidi ya mara 3 ninakuta hivyo?
 
mbona mara nyingi hapo dukani akunaga mtu,japo duka lipo wazi?nimeshakuja zaidi ya mara 3 ninakuta hivyo?

Samahani kwa hilo boss, ntalifanyia kazi hilo swala, tatizo muuzaji yupp mmoja ikitokea ametoka ameenda kufata chakula au toilet na mteja akatokea basi tatizo lazma litokee!
Ntalifanyia kazi hilo na samahani kwa hilo
 
Samahani kwa hilo boss, ntalifanyia kazi hilo swala, tatizo muuzaji yupp mmoja ikitokea ametoka ameenda kufata chakula au toilet na mteja akatokea basi tatizo lazma litokee!
Ntalifanyia kazi hilo na samahani kwa hilo

niongeze na mimi tuwe wawili mkuu
 
Ushauri:

Uza: a) Lita moja: TZS 20,000/=

b) Nusu lita: TZS 10,000/=


Utauza sana kwa bei hizi "zilizopoa" kiasi. Kwa 35,000/= per litre utafanya watu waagize huko huko unakochukuwa wewe.
 
Ushauri:

Uza: a) Lita moja: TZS 20,000/=

b) Nusu lita: TZS 10,000/=

Utauza sana kwa bei hizi "zilizopoa" kiasi. Kwa 35,000/= per litre utafanya watu waagize huko huko unakochukuwa wewe.
Samahani boss kwa kucheleqa kujibu nilikua na matatizo ya mtandao!
Upangaji wa bei una mambo mengi boss, je unajua sasa hivi tabora kwenyewe madukani lita 1 ya nyuki wadogo inauzwaje? Kama ulikua huna taarifa ni elfu 20 na iko kwenye package low quality, sasa fanya hesabu kidogo tu ya kuitoa huko, kuisafisha vizuri, kuipack, labelling na kuisambaza kwa wateja,unaweza ukaona utakaposhia!
Ila asante sana kwa ushauri!!
 
Samahani boss kwa kucheleqa kujibu nilikua na matatizo ya mtandao!
Upangaji wa bei una mambo mengi boss, je unajua sasa hivi tabora kwenyewe madukani lita 1 ya nyuki wadogo inauzwaje? Kama ulikua huna taarifa ni elfu 20 na iko kwenye package low quality, sasa fanya hesabu kidogo tu ya kuitoa huko, kuisafisha vizuri, kuipack, labelling na kuisambaza kwa wateja,unaweza ukaona utakaposhia!
Ila asante sana kwa ushauri!!

Nimekupata ndugu yangu..... lakini vipi, inatoka?
 
Salam wakuu, napenda kutambulisha kwenu duka la kwanza na pekee la ASALI halisi na bora toka HONEY SPRING. duka lipo katika ghorofa la LOTTOS mkabala na ofisi za bima. Asali hii inatoka mkoani TABORA na tunauza ASALI YA NYUKI WAKUBWA na ASALI YA NYUKI WADOGO pia katika ujazo tofauti. bei zetu ni;- ASALI YA NYUKI WAKUBWA( WAKUBWA CLASSIC) LITA 1- 12,000 350ml-5000 ASALI YA NYUKI WADOGO LITA 1-35,000 NUSU LITA-20,000 350ml-15,000 wale mliopo mkoani DAR ES SALAAM na MOROGORO pia unaweza piga simu namba 0683370065 au 0769129351 na ukatoa order yako na utaletewa sehemu utakayoelekeza ulipo. karibuni sana, ujumbe;- VIJANA TUINGIE KWENYE UJASRIAMALI KWANI UNALIPA, ANZA KIDOGO NA UTAFANIKIWA.
Hongera Mkuu, biashara hii ni nzuri na haiozi, lakini sio nzuri ikawa pekee dukani au kwenye kiosiki unacholipia kodi na kumlipa muuzaji. labda kama ni home kwako. Tatizo lake ni kwamba utokaji wake sio mzuri, unatakiwa kuwa makini na mvumilivu vinginevyo, kama huna shughuli nyingine unaweza kata mtaji, kwa sababu mtu akishanunua lita moja au nusu lita inamchukua muda kurudi tena, maana mara nyingi inatumika kupaka kwenye mikate na ile ya Wadogo inatumika kama dawa, wakati nikifanya biashara hii nilifanya kautafiti kwa wateja wangu na kubani hivyo. Nillijaribu pamoja na mafuta ya alizeti, mambo yakawa hivyo hivyo. Kwa kuwa nilikuwa nimemweka kijana wa kuuza kutokana na mimi mwenyewe kuwa na majukumu mengine, nilichelea kuweka na vitu vingine, nilihitaji biashara ambayo ni rahisi kuhesabika. Kwa ujumla ni kwamba unatakiwa kuwa makini na biashara ya aina hii.
 
Back
Top Bottom