Duh... Netanyahu kayakanyaga aisee!

Duh... Netanyahu kayakanyaga aisee!

Watakupiga sana lakini huo ndo ukweli wakati Iran yupo kwenye mazungumzo ghafla Israel inaenda kumshambulia Iran ule kulikua ni Zaidi ya Ujinga sasa
Israel imevunjwa vunjwa vibaya na Iran. Siku nyingine Netanyahu hawezi kuanzisha tena vita na iran.
 
Niaje waungwana

Nafikiri mashambulizi ya mwaka jana kati ya Iran na Israel, yalimpofusha sana Netanyahu kwa kuamini kwamba Iran ilikuwa na silaha chache, na dhaifu kwa kuweza kufanya maangamizi katika ardhi ya Israel.

Ikumbukwe kwamba katika mashambulizi yale Iran alitumia makombora ya kawaida na ya masafa mafupi, hivyo hata madhara na uharibifu wake huko Israel haukuwa mkubwa kivile, hali iliyomfanya Netanyahu aamini kwamba Iran haina silaha za maana za kupambana nae, lakini pia aliamini kwamba Iron dome na Thaad zikiongezwa na kurekebishwa vizuri, basi muajemi atachapika vizuri bila kurusha au kuingiza chochote katika ardhi ya Israel.

Masikini, jamaa hakujua kwamba Ayatollah alikuwa anampimia upeo wake wa akili ulipoishia. Akaenda Marekani kuonana na Trump kisha wakapanga namna watakavyoivamia Iran, kutawala anga, na kuzuia kombora kurushwa nchini kwao Israel.

Waswahili wanasema usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Neta akaanza uvamizi kwa mashambulizi ya kushtukiza huku wakiwa wameshajipanga na Marekani, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa na washirika wengine kuzuia mashambulizi ya Iran kwenda Israel. Mpaka hapo walikuwa wanajua Iran haina silaha au makombora ya maana ya kupenya ulinzi wao. Kwa bahati mbaya hali ikawa tofauti na walivyotarajia.

Vinu vikaanza kutumwa Israel katika speed na nguvu ya ajabu kiasi ya kwamba Iro dome na Thaad zao zikabaki kama maonesho tu au mavyuma ya kukamatia kumbi kumbi. Iron dome balada ya kuzuia kombora, inazuia nzi na upepo.

Netanyahu akaona maji yamezidi unga, kinachozuiwa hakionekani, akamwambia baba yake Trump aingilie kati. Baba na yeye kuingilia kati kaishia kupiga hewa, huku mzigo ukiwa umeshahamishwa zamani. Baada ya hapo wakafikiri hilo tukio linamfanya muajemi aogope au kusalimu amri, badala yake ikawa kama vile wamempeleka mzaramo mkoleni. Yani ndo amezidisha mashambulizi na kuigeza Tel Aviv kama Mogadishu.

Baada ya plan kushindwa eti wameamua kuomba poo kwa kutaka vita isimame. Muajemi hataki kusikia hilo, bado anaendeleza kipondo tu huko Israel. Japo wao ni mabingwa wa kuficha taarifa, lakini ukiona Trump anakimbilia kutaka mapigano yasitishwe au vita iishe basi ujue ameona madhara makubwa mno yaliofanywa na Iran huko Israel. Maana ni yeye ndio alikuwa anasema eti waachwe waendelee kuchapana. Sasa imekuaje tena kutaka vita isimame. Za kuambiwa changanya na zako.

Vita sio poa. Nina imani Netanyahu anajuta kuanzisha huu mzozo na vita ikisimama naamini hatokuja tena kuigusa Iran kindezi ndezi vile.

Ukiona mtu mzima analia ujue kuna jambo. Fikiria leo hii Trump anapambana ili vita iishe. Ujue kuna jambo kubwa limetokea huko Israel halitakiwi kusemwa 🤣🤣🤣
Sasa unajua lengo la Israel lifetime?
 
Ningeshangaa sana iran kupigwa na hayo mapapai ya kizayuni😄
Baada ya Marekani kuonesha nia ya kumsaidia Israel mapambano, Russia ikataka kuingia nayo imsaidie Iran. Ayatollah akamwambia Putin we tulia usiwe na shaka, hawa wote wawili nawamudu vizuri sana. Putin akatulia, na kweli Ayatollah kawamudu wote wawili.
 
Sawa, mleta mada hebu niambie Israel ameshaharibu sehemu zote alioona zilikuwa zikichangia kwa asilimia nyingi kumsaidia iran kukamilisha mpango wake wa Nuclear, na watu muhimu kawaondoa.

Sasa nakuuliza ulitaka apige makazi ya watu maana hicho ndicho kilichobakia! Mimi sioni kingine...

Na Labda hapa ungesema wameshindwa kumuondoa Ayatollah.

Na labda pia waIran hawakuwa na utayari kufanya mapinduzi.

Hayo mawili nafkiri yangeeleweka zaidi, yani Israel kucheza kwenye Anga la Irani akipiga kila anachotaka, na sijaskia kuna ndege ya Israel imedondoshwa, na huku Iran akimpiga Israel na kupiga anachopata nafasi ya kupiga, na unasema Iran mshindi?

Unafikiri Israel ingeenda kwa mfumo wa kubutua chochote anachokutana nacho huko Iran pangebaki salama?
 
Sawa, mleta mada hebu niambie Israel ameshaharibu sehemu zote alioona zilikuwa zikichangia kwa asilimia nyingi kumsaidia iran kukamilisha mpango wake wa Nuclear, na watu muhimu kawaondoa.

Sasa nakuuliza ulitaka apige makazi ya watu maana hicho ndicho kilichobakia! Mimi sioni kingine...

Na Labda hapa ungesema wameshindwa kumuondoa Ayatollah.

Na labda pia waIran hawakuwa na utayari kufanya mapinduzi.

Hayo mawili nafkiri yangeeleweka zaidi, yani Israel kucheza kwenye Anga la Irani akipiga kila anachotaka, na sijaskia kuna ndege ya Israel imedondoshwa, na huku Iran akimpiga Israel na kupiga anachopata nafasi ya kupiga, na unasema Iran mshindi?

Unafikiri Israel ingeenda kwa mfumo wa kubutua chochote anachokutana nacho huko Iran pangebaki salama?
Iran sio Palestina tuliwaambia nyie hamkusikia, Kilichompata Netanyau anajutia ujinga wake, hana hata lengo moja alilofanikisha, Ila Iran amekamilisha malengo yote, ndio maana Trump anataka hii vita isimame maana Israeli inaenda kuangamizwa na Iran.
 
Iran sio Palestina tuliwaambia nyie hamkusikia, Kilichompata Netanyau anajutia ujinga wake, hana hata lengo moja alilofanikisha, Ila Iran amekamilisha malengo yote, ndio maana Trump anataka hii vita isimame maana Israeli inaenda kuangamizwa na Iran.
Kwanza mimi sishabikii hii vita, ila nachoongelea hapa ni kuwa mfano mimi nilitaka kuingia ndani kwako kukunyang'anya silaha ambayo umekuwa ukiitengeneza kwa muda mrefu na unaelekea kuikamilisha, na umekuwa ukiniahidi kuwa ukishaikamilisha basi utanimaliza nayo, mimi nikafanikiwa kuingia ndani kwako nikaharibu kila mfumo wako wa kuitengeza hiyo silaha.

Je, wewe unaona kuna kitu kingine umebaki nacho cha kunitisha mimi?

Hebu assume katika makombora yote yaliyotua Israel ingekuwa ni bomu moja tu la Nuke, hapo Israel pangekuwa na maafa kiasi gani?
 
Kwanza mimi sishabikii hii vita, ila nachoongelea hapa ni kuwa mfano mimi nilitaka kuingia ndani kwako kukunyang'anya silaha ambayo umekuwa ukiitengeneza kwa muda mrefu na unaelekea kuikamilisha, na umekuwa ukiniahidi kuwa ukishaikamilisha basi utanimaliza nayo, mimi nikafanikiwa kuingia ndani kwako nikaharibu kila mfumo wako wa kuitengeza hiyo silaha.

Je, wewe unaona kuna kitu kingine umebaki nacho cha kunitisha mimi?

Hebu assume katika makombora yote yaliyotua Israel ingekuwa ni bomu moja tu la Nuke, hapo Israel pangekuwa na maafa kiasi gani?
Ushahidi uliotolewa na shirika la nguzu za atomic mitambo ya Iran ya nyuklia ipo sama, hakuna dalili yoyote kua mitambo hiyo imeathirika, America mwenyewe ameshindwa kuleta madhara yoyote katika shambuluo lake, achana na huyo Israeli uwezo wake kwa Iran umedhihirika ni mdogo sana, hata Iran mwenyewe haihofii tena Israeli na ndio sababu Trump anataka hii vita isimame, maana Israeli hana uwezo tena wa kabiliana na Iran kwa hali yoyote. Msilolijua Iran hii vita amejiandaa nayo kwa muda mrefu, kitu ambacho Israeli hawezi kwenda nayo hata mwezi mmoja atakua amesha tepepeta vibaya sana
 
Ushahidi uliotolewa na shirika la nguzu za atomic mitambo ya Iran ya nyuklia ipo sama, hakuna dalili yoyote kua mitambo hiyo imeathirika, America mwenyewe ameshindwa kuleta madhara yoyote katika shambuluo lake, achana na huyo Israeli uwezo wake kwa Iran umedhihirika ni mdogo sana, hata Iran mwenyewe haihofii tena Israeli na ndio sababu Trump anataka hii vita isimame, maana Israeli hana uwezo tena wa kabiliana na Iran kwa hali yoyote. Msilolijua Iran hii vita amejiandaa nayo kwa muda mrefu, kitu ambacho Israeli hawezi kwenda nayo hata mwezi mmoja atakua amesha tepepeta vibaya sana
Unaongea kitu gani hapa?
Umeelewa post yangu nilokujibu?

Nimekuambia vile Israel ilikuwa inalenga, sasa Yeye anaona amekamilisha, wewe unasema vita ya mwezi, kwani alikuambia anataka kupigana au anataka kukomesha mambo ya Nuclear?

Elewa tofauti hapo...!!!
 
Ushahidi uliotolewa na shirika la nguzu za atomic mitambo ya Iran ya nyuklia ipo sama, hakuna dalili yoyote kua mitambo hiyo imeathirika, America mwenyewe ameshindwa kuleta madhara yoyote katika shambuluo lake, achana na huyo Israeli uwezo wake kwa Iran umedhihirika ni mdogo sana, hata Iran mwenyewe haihofii tena Israeli na ndio sababu Trump anataka hii vita isimame, maana Israeli hana uwezo tena wa kabiliana na Iran kwa hali yoyote. Msilolijua Iran hii vita amejiandaa nayo kwa muda mrefu, kitu ambacho Israeli hawezi kwenda nayo hata mwezi mmoja atakua amesha tepepeta vibaya sana
Mimi nakumbuka walisema hivyo baada Israeli kushambulia na hawajasema hivyo baada ya US kushambulia.
 
Unaongea kitu gani hapa?
Umeelewa post yangu nilokujibu?

Nimekuambia vile Israel ilikuwa inalenga, sasa Yeye anaona amekamilisha, wewe unasema vita ya mwezi, kwani alikuambia anataka kupigana au anataka kukomesha mambo ya Nuclear?

Elewa tofauti hapo...!!!
Hilo la kukomesha nyuklia ameshindwa, pamoja na US kumsaidia lakini pia nae kashindwa.
 
M
Thread ingekuwa nzuri lakini umeiharibu kwa kuandika kiushabiki tena ushabiki wa kijinga.
1. Iron dome na Alloy 3 zime intercept karibia 95% ya makombora ya Irani, kumbuka kuwa hakuna mfumo au mashine ambayo inaufanisi wa 100%.
2. Lengo la Israel ilikuwa kuvuruga program ya nyuklia ya Irani. Wao wameona wamefanikiwa.
3. Wananchi wengi wa Israel wako kwenye Bomb shelters na kufanya kazi za kujenga uchumi zisimame, wanataka vita iishe ili wawndelee na shughuli za kiuchumi.
4. Irani imepata harasa ya vita hii kuliko Israel ambayo imepoteza raia wa kawaida wachache.
Mkuu usituumbue sisi Wairan wa Maneromango.
 
Hilo la kukomesha nyuklia ameshindwa, pamoja na US kumsaidia lakini pia nae kashindwa.
Unaongea nini wewe? Wenzio waajemi wanalia kilio cha mbwa mdomo juu, halafu wewe unaongea hivyo hovyo.
 
Kwanza mimi sishabikii hii vita, ila nachoongelea hapa ni kuwa mfano mimi nilitaka kuingia ndani kwako kukunyang'anya silaha ambayo umekuwa ukiitengeneza kwa muda mrefu na unaelekea kuikamilisha, na umekuwa ukiniahidi kuwa ukishaikamilisha basi utanimaliza nayo, mimi nikafanikiwa kuingia ndani kwako nikaharibu kila mfumo wako wa kuitengeza hiyo silaha.

Je, wewe unaona kuna kitu kingine umebaki nacho cha kunitisha mimi?

Hebu assume katika makombora yote yaliyotua Israel ingekuwa ni bomu moja tu la Nuke, hapo Israel pangekuwa na maafa kiasi gani?
Hivi Kwa akili Zako Iran ni mijnga kiasi Gani kupiga bomu la nyuklia Israel ambayo ni Palestine? Wewe unafikiri ni kwanini Iran hajapiga kinu Cha nyuklia Cha Israel wakati yeye amepigwa kinu chake? Lakini alipga TU research center? Tumia ubongo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom