Message sent and delivered
Jamii forum ni mtandao wa kijamii wenye muktadha wa kuweka hoja zinazojadilika kwa kuzingatia masharti vigezo na taratibu zake
Ni katika muktadha huo kuna watu wana hobbie na vipawa tofauti
. Kuna ambao hupendelea kuweka mada kwa jukwaa moja tu ndani ya majukwaa mengi ya forum
. Kuna wengine hupendelea kusoma tu bila kuchangia chochote
. Kuna wengine hupendelea kulike tu
. Kuna wengine hupendelea kuchangia mada mbalimbali
. Kuna wengine hupendelea kufanya vyote kwa pamoja
Hatulingani, hatufanani.... Inashangaza sana kama mtu atakuwa anaumia kuona kuna mtu anakuwa na uwezo na muda wa kuweka mada mpya kila wakati.... Inakuwa ni husuda ama ni wivu au ninini?
Mtu ambaye wala hamfamiani kabisa mmekutana mtandaoni kwenye mijadala na hoja mbalimbali, hufahamu hata maisha na vipaumbele vyake... Hajawahi kukuomba hata mia... Unaumizwa kumuona kila wakati ana post mpya kwa jambo fulani.... Hivi hapa mwenye shida ninani?
Forum iko wazi kwa yeyote kuandika chochote kulingana na jukwaa husika... Almradi tu havunji taratibu na kanuni zilizowekwa... Haina restrictions
Tatizo la wengi katika uchache wenu mnataka kuwapangia watu cha kufanya katika maisha yao ama kufanya nyie mtakavyo kwa mitazamo yenu... Huu unaitwa utapiamlo wa ufahamu....
The Book iko hivi nitaendelea kuweka mada hapa jukwaani kadiri nitakavyoona inafaa na kadiri nitavyopata mada za kuweka.... Habari za kusema najifanya najua kila kitu huo ni mtazamo wa washindwa wengi waliokosa uthubutu wa kujaribu kufanya kitu kwa kuhofia maoni ya wengine.... Sana sana watu kama nyie ndio huwa na kimuhemuhe cha kuchungulia kwenye new post kuona Mshana kaandika nini....
Hata hivyo kwa kutamatisha napenda kukushukuru kwakuwa follower mzuri wa mada zangu la sivyo usingefahamu kamwe kuwa kila wakati niko na kitu jipya ambacho hata hivyo kinakuvutia kuchangia...
JF ni sehemu ya wote wenye title za great thinkers... Si vema kupangiana cha kufanya.... Hakuna mtoto hapa...