hunchback
JF-Expert Member
- Nov 10, 2014
- 658
- 289
Wanajukwaa wote nakuja kwenu kwa ushauri nichukue hatua gani.
Niliomba fundi kufanya decoder installation mwezi wa tano kutoka kitengo cha huduma kwa wateja. Nikaletewa fundi, wakaja wawili bwana.
Wakafunga decoder, wakati wa kufunga miguu ya tv, tv ikavunjika.
Wakiwa pale mafundi wakaniambia Tv za kisasa zina tabia ya kufanya self diagnosis hivyo nisijali tv itakaa sawa (ilikuwa inaonesha, ile pembeni kumepiga mstari kidogo).
Baada ya wao kuondoka nikaona tatizo linazidi ikabidi nipige simu huduma kwa wateja kuelezea.
Nikapewa ushirikiano ikiwemo wao kukiri kosa lilofanyika na kwamba watalifanyia kazi
(Ushahidi ninao wa maongezi yote).
Baada ya siku kadhaa nikaona nazungushwa, nikipiga simu sipati ushirikiano wa kutosha.
Baadaye wamekuja kuniambia kampuni haitahusika na uharibifu badala yake nimpeleke fundi mahakamani ili anilipe (fundi alikuja na mwenzake wakashirikiana kufanya kazi nilikuja kujuabaadaye kuwa siyo muajiriwa ni bodaboda).
Kiukweli hii imeniumiza sana, maana tv ilikuwa ni mpya (Hisense 58') na uzembe umefanyika ila Dstv Tanzania wanaruka kihunzi wakati wao ndio waliniletea mafundi.
Niliomba fundi kufanya decoder installation mwezi wa tano kutoka kitengo cha huduma kwa wateja. Nikaletewa fundi, wakaja wawili bwana.
Wakafunga decoder, wakati wa kufunga miguu ya tv, tv ikavunjika.
Wakiwa pale mafundi wakaniambia Tv za kisasa zina tabia ya kufanya self diagnosis hivyo nisijali tv itakaa sawa (ilikuwa inaonesha, ile pembeni kumepiga mstari kidogo).
Baada ya wao kuondoka nikaona tatizo linazidi ikabidi nipige simu huduma kwa wateja kuelezea.
Nikapewa ushirikiano ikiwemo wao kukiri kosa lilofanyika na kwamba watalifanyia kazi
(Ushahidi ninao wa maongezi yote).
Baada ya siku kadhaa nikaona nazungushwa, nikipiga simu sipati ushirikiano wa kutosha.
Baadaye wamekuja kuniambia kampuni haitahusika na uharibifu badala yake nimpeleke fundi mahakamani ili anilipe (fundi alikuja na mwenzake wakashirikiana kufanya kazi nilikuja kujuabaadaye kuwa siyo muajiriwa ni bodaboda).
Kiukweli hii imeniumiza sana, maana tv ilikuwa ni mpya (Hisense 58') na uzembe umefanyika ila Dstv Tanzania wanaruka kihunzi wakati wao ndio waliniletea mafundi.