DSTV muda sio mrefu tutawaacha mazima

DSTV muda sio mrefu tutawaacha mazima

Unapokuwa na smart TV vifurushi vya dst TV au Azam hiyo fedha ungetaman ununue bando la internet ili ustream kilakitu Kwa Uhuru Zaid katika TV yako, na bado nyumbani mtatumia ilo bando Kwa mambo mengine sasa apo huwez kutegemea tena ivi vifurushi vya kawaida vya internet ya voda au tigo NI ghali Sana kutumia kwe smart TV, kwahiyo itakubidi tu uhamie kwenye vitu kama fiber ambayo internet inasambazwa majumbani Kwa waya ambapo unalipa bili kama umeme, ambapo kidogo unakuwa huru na TV yako,sasa huduma kama hi serikali haiwezi imwachie mtu binafsi
 
Hiki kitu nilikuwa nawaambia wenzangu leo tu baada ya kugundua hii michuano ya CAFCL haitaoneshwa. Na hapo walianzia kuanzia zile game za kufuzu WC mechi zote 2 za Stars hawakuzionesha.

Yani tulipe pesa kwenye king'amuzi chao bado tulipie mabando kustream live game nyingine ambazo hawazioneshi.
Wameishiwa.
Utopolo na kiremba chako
 
Unlimited internet ni around elfu 70 kwa mwezi mpaka laki na 20 kwa mwezi. Inategemea na ISP anaekuuzia net.

Mimi silipii kingamuzi chochote.

Nalipia unlimited internet zuku 70,000 kwa mwezi
mkuu unafanyaje ukitaka kustream mpira kama unatumia Smart Tv, tupe maujanja.
 
Dstv ukiachana na EPL na Champions league matches hawana cha kuoffer kwa fans wake imagine CAF Champions league hawataonyesha games zao AZAM akipata tender ya kuonesha EPL na Champions league fixtures kesho yake mapema asubuhi nitaliuza dish Lao kwa watu wengine
Azam hapati EPL...HAPATI.
 
Inawezekana ni mambo ya kibali kama ambavyo azam hana cha Epl.Haya mambo yako kibiashara zaidi.
 
Azam huku huku ambako ukivuma tu upepo matangazo yanakata??? Duh sijui ila kwa kweli "burudani kwa wote" ni kichomi kwa sasa, yaani ikinyesha mvua tu ujue jiandae kuweka flash

Sasa hiki ni kitu cha kuzingatiwa, kwanini mtu una dishi lakini upepo wa feni ya asili ukivuma tu mawimbi yanakatika kama zile zama za zungusha antena elekezea mjini???

WABORESHE MITAMBO YAO
Hata dstv mvua ikinyesha sana mitambo yao inakata.

Kuna kipindi mvua ilinyesha kubwa sana mitambo ikakata na kwangu ikawa mazima haionyeshi. Nimepiga huduma kwa wateja taratibu zote nikafuata bado haikuinuonyesha. Jawabu nililopatiwa ni dishi limeyumba.

Nikawasiliana na mafundi wao wakaja kunirekebishia. Fundi akanipa maelezo mazuri tu. Akiniambua dish likifungwa inabidi likazwe sana ili lisiwe rahisi kucheza au kuyumba wakati wa mvua kubwa au upepo mkali. Lisipokazwa sana husababisha mawasiliano kuzima kabisa ikitokea mabadiliko ya hali ya hewa (mvua/upepo).

Endapo mvua kubwa itanyesha au upepo mkali kitakachotokea ni mawasiliano yatapotea kidogo tu kutokana na hali ya hewa ila yatarudi. Na ndiyo maana dstv kuna maelezo mawasiliano yakikata huwa wanakuambia eidha ni kwa sababu ya hali ya hewa au sababu nyengine.
 
Dstv ukiachana na EPL na Champions league matches hawana cha kuoffer kwa fans wake imagine CAF Champions league hawataonyesha games zao AZAM akipata tender ya kuonesha EPL na Champions league fixtures kesho yake mapema asubuhi nitaliuza dish Lao kwa watu wengine
Azam hawezi pata tenda ya kuonesha EPL, maana hapo DStv kajikita kama vile kanjibai alivyojikita kwenye jezi za Simba na ile Mo Extra
 
Hawa Dstv wanazingua.

..........Sasa hivi bora kulipia kifurushi cha 37,000 tu cha 60,000 kwenda juu ni hasara tu.

Wakiendelea kubania hivi tutarudi Azam.
 
Back
Top Bottom