DSTV muda sio mrefu tutawaacha mazima

DSTV muda sio mrefu tutawaacha mazima

Kwa hili wanatakiwa kujipanga kweli. Maana watapoteza wateja sana wanadhani wa Tanzania waliowateja wao wanapenda Tamthiliya zao basi. DStv wengi hununua kwa ajili ya Super Sports channels.

Sasa Azam anaenda kujichukulia wateja na vile kuna ving'amuzi vinavotumia antena vinapatikana kwa bei ndogo sana basi wajipange..
 
Hiki kitu nilikuwa nawaambia wenzangu leo tu baada ya kugundua hii michuano ya CAFCL haitaoneshwa. Na hapo walianzia kuanzia zile game za kufuzu WC mechi zote 2 za Stars hawakuzionesha.

Yani tulipe pesa kwenye king'amuzi chao bado tulipie mabando kustream live game nyingine ambazo hawazioneshi.
Wameishiwa.
 
Wajitafakari sana muda si mrefu tutawakimbia sijajua kwa nini mzee Bakhresa haleti michuano ya EPL na Champions league kwenye Azam akifanikiwa hili ataimaliza DSTV
DSTV analipa zaidi ya $10M (2015) kwa mwaka na ana exclusivity rights kuonyesha EPL, Champion League na ligi zingine za football kwa east and Central Africa.
 
Ile ilirusha gem zote za ulaya hadi america kusini na Africa!!
Kwa sasa kutokana na streaming,Online TVs ,Hotel IPTV soko la DSTV linashuka Kila kukicha-....na Mapato yake 2020-2023 Yanashuka Kila mwaka.ifikapo 2028 huenda atokuwepo tena..kutokana na fibre optics Networks kusambaza Africa na hivyo kufanya streaming,IPTV,VOD kuwa cheap. Na affordable
 
Back
Top Bottom