Kijakazi
Platinum Member
- Jun 26, 2007
- 9,212
- 14,802
persecution of Christians is real …
Zaidi ya watu 40 wameuawa katika shambulio lililofanywa na kundi tanzu la Dola la Kiislamu (Islamic State) kaskazini-mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa na jeshi la nchi hiyo.
Wengi wa waliouawa walikuwa waumini waliokuwa wakishiriki ibada ya mkesha wa usiku katika kanisa lililoko mjini Komanda walipovamiwa na wapiganaji wa Allied Democratic Forces (ADF). Taarifa ya ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa (Monusco) ilisema kuwa watoto tisa walikuwa miongoni mwa waliouawa.
Maduka na biashara za jirani pia ziliibwa na kuchomwa moto.
ADF ilianzishwa nchini Uganda miaka ya 1990, ikidai kuwa serikali ya nchi hiyo ilikuwa inawabagua Waislamu, lakini kwa sasa kundi hilo linafanya shughuli zake upande wa pili wa mpaka nchini DRC, ambako limekuwa likiwalenga raia wa dini zote pamoja na kufanya mashambulio nchini Uganda.
Tangu wakati huo, ADF imekuwa sehemu ya tawi la Dola la Kiislamu katika Ukanda wa Afrika ya Kati, ambalo pia linajumuisha kundi lingine nchini Msumbiji.
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na BBC Monitoring, karibu asilimia 90 ya operesheni za Dola la Kiislamu kwa sasa zinafanywa na matawi yake yaliyo Afrika.
Shambulio hilo lilikatili maisha ya watu wasiopungua 43, wakiwemo wanawake 19, wanaume 15 na watoto tisa, kwa mujibu wa Monusco.
"Matendo haya ya mashambulizi ya kulenga raia wasio na ulinzi, hasa katika maeneo ya ibada, siyo tu ya kusikitisha bali pia ni ukiukwaji wa viwango vyote vya haki za binadamu na sheria ya kimataifa ya kibinadamu," alisema naibu mkuu wa Monusco, Vivian van de Perre.
Jeshi la DRC limesema "takriban watu 40 walishambuliwa kwa ghafla na kuuawa kwa mapanga, na wengine kadhaa walijeruhiwa vibaya".
Lilisema kuwa "magaidi hawa wameamua kulipiza kisasi dhidi ya wananchi wasio na hatia ili kueneza hofu".
Luteni Jules Ngongo, msemaji wa jeshi la Congo katika jimbo la Ituri ambako shambulio hilo lilitokea, alisema shambulio hilo lililenga kupotosha umakini wa operesheni ya pamoja ya kijeshi inayofanywa na jeshi la Uganda dhidi ya kundi hilo la waasi.
Alisema jeshi litaendelea kulifuatilia kundi la ADF "hadi kwenye ngome yao ya mwisho" na kuwataka wananchi "kuwa waangalifu zaidi na kutoa taarifa kuhusu uwepo wowote wa watu wanaotia shaka kwa vyombo vya ulinzi na usalama".
Mnamo mwaka 2021, DRC iliwaalika wanajeshi wa Uganda kuingia nchini humo kusaidia katika kupambana na ADF. Hata hivyo, mashambulio bado yanaendelea.
Komanda iko katika jimbo la Ituri lenye utajiri wa madini, ambalo limekuwa likigombaniwa na makundi mbalimbali ya waasi kwa miaka mingi.
Wiki iliyopita, Monusco ililaani "kuzuka kwa wimbi jipya la ghasia" mwezi huu, ikitaja mashambulio ya awali ya ADF ya tarehe 8 na 9 Julai ambayo yaliripotiwa kusababisha vifo vya watu 47.
www.bbc.com
Kanisa likiteketezwa kwa moto huko Kongo …
Zaidi ya watu 40 wameuawa katika shambulio lililofanywa na kundi tanzu la Dola la Kiislamu (Islamic State) kaskazini-mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa na jeshi la nchi hiyo.
Wengi wa waliouawa walikuwa waumini waliokuwa wakishiriki ibada ya mkesha wa usiku katika kanisa lililoko mjini Komanda walipovamiwa na wapiganaji wa Allied Democratic Forces (ADF). Taarifa ya ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa (Monusco) ilisema kuwa watoto tisa walikuwa miongoni mwa waliouawa.
Maduka na biashara za jirani pia ziliibwa na kuchomwa moto.
ADF ilianzishwa nchini Uganda miaka ya 1990, ikidai kuwa serikali ya nchi hiyo ilikuwa inawabagua Waislamu, lakini kwa sasa kundi hilo linafanya shughuli zake upande wa pili wa mpaka nchini DRC, ambako limekuwa likiwalenga raia wa dini zote pamoja na kufanya mashambulio nchini Uganda.
Tangu wakati huo, ADF imekuwa sehemu ya tawi la Dola la Kiislamu katika Ukanda wa Afrika ya Kati, ambalo pia linajumuisha kundi lingine nchini Msumbiji.
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na BBC Monitoring, karibu asilimia 90 ya operesheni za Dola la Kiislamu kwa sasa zinafanywa na matawi yake yaliyo Afrika.
Shambulio hilo lilikatili maisha ya watu wasiopungua 43, wakiwemo wanawake 19, wanaume 15 na watoto tisa, kwa mujibu wa Monusco.
"Matendo haya ya mashambulizi ya kulenga raia wasio na ulinzi, hasa katika maeneo ya ibada, siyo tu ya kusikitisha bali pia ni ukiukwaji wa viwango vyote vya haki za binadamu na sheria ya kimataifa ya kibinadamu," alisema naibu mkuu wa Monusco, Vivian van de Perre.
Jeshi la DRC limesema "takriban watu 40 walishambuliwa kwa ghafla na kuuawa kwa mapanga, na wengine kadhaa walijeruhiwa vibaya".
Lilisema kuwa "magaidi hawa wameamua kulipiza kisasi dhidi ya wananchi wasio na hatia ili kueneza hofu".
Luteni Jules Ngongo, msemaji wa jeshi la Congo katika jimbo la Ituri ambako shambulio hilo lilitokea, alisema shambulio hilo lililenga kupotosha umakini wa operesheni ya pamoja ya kijeshi inayofanywa na jeshi la Uganda dhidi ya kundi hilo la waasi.
Alisema jeshi litaendelea kulifuatilia kundi la ADF "hadi kwenye ngome yao ya mwisho" na kuwataka wananchi "kuwa waangalifu zaidi na kutoa taarifa kuhusu uwepo wowote wa watu wanaotia shaka kwa vyombo vya ulinzi na usalama".
Mnamo mwaka 2021, DRC iliwaalika wanajeshi wa Uganda kuingia nchini humo kusaidia katika kupambana na ADF. Hata hivyo, mashambulio bado yanaendelea.
Komanda iko katika jimbo la Ituri lenye utajiri wa madini, ambalo limekuwa likigombaniwa na makundi mbalimbali ya waasi kwa miaka mingi.
Wiki iliyopita, Monusco ililaani "kuzuka kwa wimbi jipya la ghasia" mwezi huu, ikitaja mashambulio ya awali ya ADF ya tarehe 8 na 9 Julai ambayo yaliripotiwa kusababisha vifo vya watu 47.
ADF in DR Congo: IS-linked rebels accused of killing Christian worshippers in Komanda
Most of the dead were worshippers taking part in a night vigil which was stormed by armed men, officials said.
Kanisa likiteketezwa kwa moto huko Kongo …