Dr W.P.Slaa ondoa mashaka kuhusu UDSM

Dr W.P.Slaa ondoa mashaka kuhusu UDSM

bato

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
3,960
Reaction score
3,474
Wana JF,kulikuwa na thread hapa JF kuhusu mashaka ya Dr Slaa kwa kiwango cha elimu inayotolewa UDSM.Jana nimepata ujumbe kuwa niangalie ubora wa vyuo vikuu 100 bora Africa."2013 WORLD UNIVERSITY WEB RANKING"
Top 100 Universities and Colleges in Africa.
1.Univers. of S.Africa (S.Africa)
2.'' " " Cape T. (S.Africa)
3." " Stellenbosch. (S.Africa)
4.University of Dar es Salaam (Tanzania)
5....6.....7..8....9....10...
11.Makerere Univ. (Uganda)
12....
20.Nairobi Univ. (Kenya)
21.......
59.Sokoine Univ of Agri. (Tanzania)
60.....
98.Muhimbili University of Health and Alied Science, (Tanzania)
Sijui vigezo,ila nimependa kuwa Mlimani iko juu.Wanaojua zaidi tusaidieni.
 
Mbopna Muhimbili ipo nyuma sana au ni ile migomo isiyokwisha?
 
Wana JF,kulikuwa na thread hapa JF kuhusu mashaka ya Dr Slaa kwa kiwango cha elimu inayotolewa UDSM.Jana nimepata ujumbe kuwa niangalie ubora wa vyuo vikuu 100 bora Africa."2013 WORLD UNIVRSITY WEB RANKING"
Top 100 Universities and Colleges in Africa.
1.Univers. of S.Africa S.Africa
2.'' " " Cape T. S.Africa
3." " Stellenbosch. S.Africa
4.University of Dar es Salaam Tanzania
5....6.....7..8....9....10...
11.Makerere Univ. Uganda
12....
20.Nairobi Univ. Kenya
21.......
59.Sokoine Univ of Agri. Tanzania
60.....
98.Muhimbili University of Health and Alied Science, Tanzania.
Sijui vigezo,ila nimependa kuwa Mlimani iko juu.Wanaojua zaidi tusaidieni.
Mashaka yake yalikuwa kwa Mwigulu kuwa reasoning yake iko chini sana na kama alipata 1st class basi kuna jambo sio la kawaida hapo UDSM. Ila mkuu kuna uzi ulisha dhibitisha kuwa Mwigulu hakuwa na uwezo wa kupata 1st class ila kuna kamchezo kalifanyika. Siendi mbali zaidi ya hapo.
 
Wana JF,kulikuwa na thread hapa JF kuhusu mashaka ya Dr Slaa kwa kiwango cha elimu inayotolewa UDSM.Jana nimepata ujumbe kuwa niangalie ubora wa vyuo vikuu 100 bora Africa."2013 WORLD UNIVRSITY WEB RANKING"
Top 100 Universities and Colleges in Africa.
1.Univers. of S.Africa S.Africa
2.'' " " Cape T. S.Africa
3." " Stellenbosch. S.Africa
4.University of Dar es Salaam Tanzania
5....6.....7..8....9....10...
11.Makerere Univ. Uganda
12....
20.Nairobi Univ. Kenya
21.......
59.Sokoine Univ of Agri. Tanzania
60.....
98.Muhimbili University of Health and Alied Science, Tanzania.
Sijui vigezo,ila nimependa kuwa Mlimani iko juu.Wanaojua zaidi tusaidieni.

Ukweli:
Dr.w.slaa hajawahi kuzungumzia chochote kuhusu shaka ya taaluma itolewayo udsm, hayo unayoyasema wewe labda ni hisia zako katika kujibu kwake issue flani, na bila shaka ni wakati wa kumjibu mh. Mwigulu Nchemba kuhusu logic za red brigade, hata hivyo pale hakuzungumzia chochote kuhusu udsm! usisahau kuwa akina mh. Zitto, Kitila Mkumbo, na wasomi wengi wa udsm wana-support kwa zaidi ya asilimia 100 harakati za chadema kuhusu rasilimali za taifa letu!

Karibu tena kama ukiwa na shaka yoyote! UNDENIABLE
 
Last edited by a moderator:
Kwani dr. Slaa akasoma chuo gani mpaka apate moral authority ya kuhoja kiwango cha elimu cha UD?
 
serikali imejaa phd holders na dr kibao, deliveries zao zikoje? hata mimi std vii naona naweza kuliko wao! Ikumbukwe vyuo vyetu havifundishi u-EPA etc, ni nafsi tu.
 
Mashaka yake yalikuwa kwa Mwigulu kuwa reasoning yake iko chini sana na kama alipata 1st class basi kuna jambo sio la kawaida hapo UDSM. Ila mkuu kuna uzi ulisha dhibitisha kuwa Mwigulu hakuwa na uwezo wa kupata 1st class ila kuna kamchezo kalifanyika. Siendi mbali zaidi ya hapo.

funguka kaka kuhusu mwigulu,ana kelele nyingi, natamani kumjua na nielewe kama ndio sababu ana behave vile alivyo.
 
Mwigulu anaweza kuwa na uwezo ila akajifanya hamnazo! Hilo kwenye siasa linawezekana maana tumeshuhudia wanasiasa wengi wakitumia mihemko zaidi badala ya Logic!
Wana JF,kulikuwa na thread hapa JF kuhusu mashaka ya Dr Slaa kwa kiwango cha elimu inayotolewa UDSM.Jana nimepata ujumbe kuwa niangalie ubora wa vyuo vikuu 100 bora Africa."2013 WORLD UNIVRSITY WEB RANKING"
Top 100 Universities and Colleges in Africa.
1.Univers. of S.Africa S.Africa
2.'' " " Cape T. S.Africa
3." " Stellenbosch. S.Africa
4.University of Dar es Salaam Tanzania
5....6.....7..8....9....10...
11.Makerere Univ. Uganda
12....
20.Nairobi Univ. Kenya
21.......
59.Sokoine Univ of Agri. Tanzania
60.....
98.Muhimbili University of Health and Alied Science, Tanzania.
Sijui vigezo,ila nimependa kuwa Mlimani iko juu.Wanaojua zaidi tusaidieni.
 
Kwani dr. Slaa akasoma chuo gani mpaka apate moral authority ya kuhoja kiwango cha elimu cha UD?

Alihoji wapi? Msizushe mambo, mnajaribu kumjengea maadui lakini hamtashinda! Wasiwasi wa Dr. Ni maarifa na ufahamu wa Mwigulu, kwani haufanani na wahitimu wa UD!
 
Mkuu Dr Slaa hawezi kuleta shaka na Elimu ya UDSM! Labda ana shaka na watu wachache waliosoma pale! Kumbuka, hata kama Chuo ni bora, si kila Mwanafunzi aliyehitimu pale anaweza kuwa bora. Wapo wengi tu vilaza na tulipiga nao pale shule!
 
Sidhani kama Slaa ana haki wa kuhoji kiwango cha elimu cha yeyote yule! Elimu yake ni mbovu afadhali ya MULUGO mara 1000!
 
Wana JF,kulikuwa na thread hapa JF kuhusu mashaka ya Dr Slaa kwa kiwango cha elimu inayotolewa UDSM.Jana nimepata ujumbe kuwa niangalie ubora wa vyuo vikuu 100 bora Africa."2013 WORLD UNIVRSITY WEB RANKING"
Top 100 Universities and Colleges in Africa.
1.Univers. of S.Africa S.Africa
2.'' " " Cape T. S.Africa
3." " Stellenbosch. S.Africa
4.University of Dar es Salaam Tanzania
5....6.....7..8....9....10...
11.Makerere Univ. Uganda
12....
20.Nairobi Univ. Kenya
21.......
59.Sokoine Univ of Agri. Tanzania
60.....
98.Muhimbili University of Health and Alied Science, Tanzania.
Sijui vigezo,ila nimependa kuwa Mlimani iko juu.Wanaojua zaidi tusaidieni.

Mkuu heshima kwako,

Nafikiri alilolisema Dr. Slaa ni kushuka kwa kiasi kikubwa kwa kiwango cha elimu inayotolewa hapo UDSM. Binafsi nilihitimu Chuoni hapo shahada ya kwanza miaka ya mwanzo ya 80, na nimekuwa nikifuatilia sana watu wanaohitimu miaka hii ya sasa. Kwa kiwango kikubwa sana ninashangazwa kila mara ninaposikia watu wanaojiita wahitimu wa UDSM wa miaka hii ya karibuni uwezo wao wa kuchanganua mambo na kufanya tathmini ya masuala mbalimbali. Huwa ninabaki kufikiri sasa kama hawa ndio wahitimu wa UDSM, hao wengine ambao hawakufika hatua hiyo kimasomo wakoje? Wakati tulipokuwa chuoni kuandika 'seminar paper' na kuwasilisha mada kwenye semina ilikuwa ni kitu cha lazima. Na sheria namba moja ilikuwa ni marufuku kusoma, hoja ulizoziandika kwenye karatasi unamkabidhi mwalimu/mhadhiri/mkufunzi halafu wewe unaiwasilisha mada yako bila karatasi na kujibu maswali kuitetea mada yako, unakubali kupewa upinzani na hoja mbadala 'constructive criticism' na unakwenda kuzifanyia kazi. Hakika kimataifa UDSM ilikuwa tishio. Ndipo waliposoma wakina Prof. Shivji, wakina Wadada Nabudere, walikuwepo wakina Walter Rodney, wakina prof. Chachage na wengine wengi, hakuna haja ya kuwataja wote. UDSM palikuwa kitovu cha taaluma, mahali ambapo hata serikali na chama wakati huo kilikuwa kimoja tu CCM, walijua ya kuwa kila changamoto inayotoka pale ilibidi waichukulie kwa makini kwa kuwa walikuwa wanaweza kuwekwa kitimoto na wataalamu na wasomi kutoka Chu Kikuu kuhusu sera mbalimbali zilizokuwa zinaonekana kuwa na mwelekeo usiokubalika kuhusu mustakabali wa maendeleo ya jamii yetu.

Niambie leo hii UDSM imekuwa mahali pa kuipigia kampeni serikali, siyo kitovu cha taaluma huru chenye kutoa changamoto kwa serikali na kujaribu kuipa mwongozo wa kitaaluma kuhusu mustakabali mzima wa maendeleo ya Tanzania. Unakuta mtu anayejisifia na kujiita 'msomi' wengine wanatamba mpaka na kujipa madaraja ya usomi huo, ukimwambia hebu nieleze jambo dogo tu hawezi. 'Msomi' wa UDSM leo hii ukimuuliza kwa nini nchi yetu ni maskini anasema hadharani 'hajui kwa nini nchi yetu ni maskini'. 'Msomi' ambaye hajui maana ya demokrasia hata anadiriki kusema 'ccm itatawala milele' na 'mkichagua upinzani mtakufa'. 'Msomi' ambaye akiambiwa wasilishe mada kwenye kikao anaanza kusoma kuanzia sentensi ya kwanza mpaka ya mwisho, na pengine hata hiyo mada anayoiwasilisha kaandikiwa yote, ukitaka kujua kama kaiandika mwenyewe mtupie swali rahisi tu kuhusu hilo analoliongea uone jinsi atakavyotoka jasho, ama atakavyokenua meno utadhani yuko kwenye mashindano ya urembo. Hiki ndicho kielelezo cha wasomi tulio nao hivi sasa.

UDSM kuwa chuo cha nne haibadilishi ukweli huu. Fahamu ya kwamba hata ukiwapa vichaa mtihani, kutakuwa na atakayeshika namba moja. Haina maana ya kuwa mtu huyo ana akili, ila katika kundi la hao vichaa angalau kwa huyo mmoja dawa zinaelekea kufanya kazi. Ila haina maana ya kuwa amepona!
 
udsm iko juu daima halafu slaa kasoma masomo ya dini tu atajuaje uzuri wa vyuo kama udsm.
 
Mashaka yake yalikuwa kwa
Mwigulu kuwa reasoning yake iko chini sana na kama alipata 1st class
basi kuna jambo sio la kawaida hapo UDSM. Ila mkuu kuna uzi ulisha
dhibitisha kuwa Mwigulu hakuwa na uwezo wa kupata 1st class ila kuna
kamchezo kalifanyika. Siendi mbali zaidi ya hapo.

ni wivu tu unawasumbua. kwa vile mwenyekiti wenu hata elimu ya msingi ina mashaka, katibu mkuu wenu kasomea tu divinity na theology basi mnafikiri mwigulu hawezi kupata first class
 
Mkuu heshima kwako,

Nafikiri alilolisema Dr. Slaa ni kushuka kwa kiasi kikubwa kwa kiwango cha elimu inayotolewa hapo UDSM. Binafsi nilihitimu Chuoni hapo shahada ya kwanza miaka ya mwanzo ya 80, na nimekuwa nikifuatilia sana watu wanaohitimu miaka hii ya sasa. Kwa kiwango kikubwa sana ninashangazwa kila mara ninaposikia watu wanaojiita wahitimu wa UDSM wa miaka hii ya karibuni uwezo wao wa kuchanganua mambo na kufanya tathmini ya masuala mbalimbali. Huwa ninabaki kufikiri sasa kama hawa ndio wahitimu wa UDSM, hao wengine ambao hawakufika hatua hiyo kimasomo wakoje? Wakati tulipokuwa chuoni kuandika 'seminar paper' na kuwasilisha mada kwenye semina ilikuwa ni kitu cha lazima. Na sheria namba moja ilikuwa ni marufuku kusoma, hoja ulizoziandika kwenye karatasi unamkabidhi mwalimu/mhadhiri/mkufunzi halafu wewe unaiwasilisha mada yako bila karatasi na kujibu maswali kuitetea mada yako, unakubali kupewa upinzani na hoja mbadala 'constructive criticism' na unakwenda kuzifanyia kazi. Hakika kimataifa UDSM ilikuwa tishio. Ndipo waliposoma wakina Prof. Shivji, wakina Wadada Nabudere, walikuwepo wakina Walter Rodney, wakina prof. Chachage na wengine wengi, hakuna haja ya kuwataja wote. UDSM palikuwa kitovu cha taaluma, mahali ambapo hata serikali na chama wakati huo kilikuwa kimoja tu CCM, walijua ya kuwa kila changamoto inayotoka pale ilibidi waichukulie kwa makini kwa kuwa walikuwa wanaweza kuwekwa kitimoto na wataalamu na wasomi kutoka Chu Kikuu kuhusu sera mbalimbali zilizokuwa zinaonekana kuwa na mwelekeo usiokubalika kuhusu mustakabali wa maendeleo ya jamii yetu.

Niambie leo hii UDSM imekuwa mahali pa kuipigia kampeni serikali, siyo kitovu cha taaluma huru chenye kutoa changamoto kwa serikali na kujaribu kuipa mwongozo wa kitaaluma kuhusu mustakabali mzima wa maendeleo ya Tanzania. Unakuta mtu anayejisifia na kujiita 'msomi' wengine wanatamba mpaka na kujipa madaraja ya usomi huo, ukimwambia hebu nieleze jambo dogo tu hawezi. 'Msomi' wa UDSM leo hii ukimuuliza kwa nini nchi yetu ni maskini anasema hadharani 'hajui kwa nini nchi yetu ni maskini'. 'Msomi' ambaye hajui maana ya demokrasia hata anadiriki kusema 'ccm itatawala milele' na 'mkichagua upinzani mtakufa'. 'Msomi' ambaye akiambiwa wasilishe mada kwenye kikao anaanza kusoma kuanzia sentensi ya kwanza mpaka ya mwisho, na pengine hata hiyo mada anayoiwasilisha kaandikiwa yote, ukitaka kujua kama kaiandika mwenyewe mtupie swali rahisi tu kuhusu hilo analoliongea uone jinsi atakavyotoka jasho, ama atakavyokenua meno utadhani yuko kwenye mashindano ya urembo. Hiki ndicho kielelezo cha wasomi tulio nao hivi sasa.

UDSM kuwa chuo cha nne haibadilishi ukweli huu. Fahamu ya kwamba hata ukiwapa vichaa mtihani, kutakuwa na atakayeshika namba moja. Haina maana ya kuwa mtu huyo ana akili, ila katika kundi la hao vichaa angalau kwa huyo mmoja dawa zinaelekea kufanya kazi. Ila haina maana ya kuwa amepona!

mkuu lazima hauko sawa aidha kichwani au kwenye mwili wako pengine umegonga viroba mkuu kuwa na heshima na udsm kinaheshima zake.
 
Back
Top Bottom