Ruhazwe JR
JF-Expert Member
- Jan 31, 2011
- 3,402
- 927
Kwa hili ninakubaliana nawe JJB, bora anyamaze yaishe. Sisi tunaotaka aseme sio kwa sababu yoyote zaidi ya kutaka kusoma umbea tu. Watanzania sote tumemsaliti Dr.Ulimboka na wanaharakati wote waliowahi kuthubutu kulenga jiwe la kwanza lakini sisi tukaficha mikono yetu. Moja ya maneno na rai aliyoitoa Dr. baada ya kudhulumiwa afya na uhuru wake yalikuwa kuwataka Madaktari wenzake (na Watanzania kwa jumla) kuwa yeye yamemfika yaliyomfika, lakini waliobaki wanendelee na mapambano; matokeo yake, Madaktari walifanya nini na Watanzania tumefanya nini?
Baada ya Mwanahalisi kulezea kile ilichokijua na kuwataja watu na ubini wao na nambari zao za simu, Watanzania tumefanya nini? Tuseme Dr. Ulimboka aje na habari zile zile za Mwanahalisi, Watanzania tutafanya nini? Kama tuwatendaji kweli na sio wambea tu, tuchukue hatua juu ya yale ambayo tayari tunayajua kabla ya kutaka mengine mapya.
Tumwache Dr. apumue na sisi tuendelee na woga na blah blah blah zetu. Uchune Dokta, uchune!
Tena hazina tija hata chembe, lakini kwa vile ndizo wanazotumia wahariri uchwara kuuzia gazeti zitaendela kutawala sana!Tumeshasema habari za Dr. Ulimboka zimetuchosha hapa JF pelekeni Issa Michuzi Blog hizo habari
Godwinnko
Ilishasemwa humu JF kuwa Ulimboka ni mtaalamu na siyo mwanasiasa, hawezi kupelekwa pelekwa na wanasiasa na wanaharkati kwa maslahi yao binafsi. Haya sasa mmeanza kuja na "azimwa" Chanzo chenyewe cha taarifa Tdaima, ndo wale wle Kubenea type. Mwacheni Dr. wa watu apumzike ili aiendeleze taaluma yake, kama waliokuwa wakimtumia hawajaridhikana wabuni mbinu nyingine ya kujipatia umaarufu.
Ninajaribu kueleza kwa points kama nilivyoainisha kwenye nyekundu hapo juu:Bado Madr; 1.Watanzania, na wanaharakati tupo pamoja.
Kweli tumesikia mengi kuhusiana na hili; tumeshuhudia Viongozi wetu wa juu wakikanusha (Kikwete, Pinda na Afande Sele)
Gazeti Mwanahalisi limesema mengi na kwa uwazi.
Lakini yote kwa yote 2a).D. Ulimboka ndiye anayejua siri ya tukio zima na pia anawajua waliohusika. Kwa namna ya pekee Watanzania wanasubiri kauli yake, kisha ndip tutajua mbichi na mbivu (LIWALO NA LIWE)
Wanaharakati bado wanapenda kujua Sababu na matokeo ya tukio lile la kinyama. 3.Tusiongee kisiasa bali turudi katika hali ya kibinadamu.
Huwezi kukurupuka na kuingia mitaani kulaani kitu ambacho huna point ya kukulinda kuhusu ukweli wake. 2b.Lazima ujue ukweli kwanza ndipo uamue.
4.IPO SIKU KITAELEWEKA tu!!!!
View attachment 62579
MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
ni juu yake kuchagua kati ya heahima na utu wake au pesa, asiposema atakuwa amewasaliti wote waliomsapoti, just too bad.
Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100. hata kurudi nchini na kuona hakuna kilichoendelewa tayari ni stress sana kwake. hii nikama mtu laikua napigania haki za watu akauawa then akafufuka akapewa story jinsi watu walivyomsaliti, nafikiri atatamani afe hapohapo na asikumbuke kitu.This is very clear! Huu mgomo ni wa madaktari wote,mshikamano wao wote ndio muhimu.sometimes namuelewa Ulimboka,hakuna jemedari anaweza kusimama imara bila uhakika wa jeshi analoliongoza.
Ulimboka kupigwa tu Madaktari wakasambaratika hadi leo alafu wanataka yeye alianzishe tena!
nafikiri mwenendo wa madaktari umemkatisha tamaa Ulimboka na alitarajia wenzake wangekomaa zaidi baada ya kuumizwa vibaya lakini ikawa kinyume! kumbe hata kama wangemuua kabisa mgomo ungeisha hivi hivi kiuoga!
naelewa nafasi ya Dr Ulimboka!