Dr. WSlaa na Mh. F. Mbowe, nimefuatilia kwa karibu mbinu mnazo tumia ili kukipa umaarufu CDM, likiwapo hili mnalofanya kwa wakati huu. Tatizo ninaloona na wale waliosoma theory of games, wanaona udhaifu mkubwa au kutokuwapo ma-strategists wazuri CDM. Sababu za kusema hivyo ni kama zifuatazo:
- Mnataka wananchi wawaunge mkono kuandamana nchi nzima kama walivyofanya Tunisia, Egypt, Libya na nchi nyinginezo za kiarabu ili kumng'oa JK na serikali yake madarakani, kwa ajili ya kupinga hali ngumu maisha kwa wananchi, ufisadi na sababu nyingine nyingi. Ni kweli serikali ina mapungufu hayo, na wananchi woote wanajua. Tatizo ni kwamba, ni kwanini Wewe Dr. Slaa na Mbowe ndio muwaambie si wanayajua matatizo yao wenyewe??
- Kama ni kufuata mfano wa Tunisia, Egypt, Libya, Hivi huko kwao kuna mtu au watu mithili ya Slaa, Mbowe au for that chama kama CDM kilicho waambia watoke mtaani kuandamana??? si wametoka wenyewe hamna wa kuwaambia fanya hiki wala kile wametoka na lao ni moja serikali itoke na wamefanikiwa!!
- Katika mila na desturi zetu za kiafrika huwa tunashirikiana katika shughuli mbali mbali za kijamii ikowemo misiba na sherehe mbali mbali, katika msiba mara nyingi kuna waombolezaji wa aina tatu, wanandugu mara nyingi huwa wanalia kwa huzuni na ni rahisi kuwa gundua, kuna marafiki na majirani, lakini kuna watu wengine tu hulia kwa makelele saana hata kupita ndugu wa marehemu, CDM wanalia kama hilo kundi la tatu!! kwa nini? kwa nini tusilie pamoja kama wana ndugu (CUF,TLP,NCCR,UDP n.k) kwa nini CDM msiba wetu sote Watanzania wanalia kwa makelele? lipo tatizo hapo!
- Kuna vurugu zilitokea Arusha watu wakapoteza maisha, story zikawa nyiiiiingi ila watu wa Arusha pamoja na uongozi wa CDM hasa Slaa wanajua sababu ya hizo vurugu, Police kwa upande wao wametoa utetezi wa video ya matukio yote kwenye vyombo vya habari, CDM (Slaa) ikaahidi kujibu mapigo na kweli amejibu cd ziko sokoni!!! zinauzwa tena kwa Mujibu wa Mh. Regia Mtema, zinauzwa sh. 6000/=, kwa nini CDM iuze kanda mtaani badala ya kupeleka ubalozi wa EU, Wingereza, Marekani, au kwingineko kokote kuonyesha jinsi TZ isivyo kuwa democratic state ili CDM ipata hiyo sifa inayotaka? na pesa ya hiyo filamu inaenda kwa nani?
- Hivi CDM wanafikiri kama serikali ya CCM itapinduliwa kwa maandamano wakati watu watalifananisha hili na yale ya Tunisia, Egypt, Libya!! , this is being naive!!! maana itaonekana ni CDM na Slaa na wamepindua nchi baada ya kushindwa uchaguzi mwaka jana!! hivyo CDM haiata kuwa imeingia madarakani kihalali wala kidemokrasia!! hili mbona liko wazi??.