Dr Slaa kuzindua miradi ya maji Kyela

Dr Slaa kuzindua miradi ya maji Kyela

hongera dr slaa nakumbuka enzi zile karatu ccm walisema maji karatu hakuna.uliposhda ubunge ukatuletea maji.hongera sna
Ni bahati kubwa sana kwa wana Kyela kutembelewa na mkombozi huyu , huyu mtu anatakiwa kila mahali kwenye nchi hii , Mungu amlinde sana .
 
Hiyo inaitwa onjeni muone chadema ilivyo nzuri. CCM imeshika nchi hii miaka 35 maji bado tatizo ubungo...achana na vijiji pembezoni! Nayalivyo makorofi yanawatesa wanaubungo kwa sababu za ovyo kabisa.

Hivi mnafitini Mnyika ili mweke nani nafasi hiyo.....hata hamwezi kuona umuhimu wa Mnyika Bungeni?...Tusipokuwa macho ccm watajaza mazezeta bungeni!
Hiyo onjeni muone chadema imenifurahisha sana ! Asante kamanda kwa kibwagizo kikali .
 
hii maana yake serikali imeshindwa kazi
Imeshindwa kitambo sana , serikali mpya ya UKAWA inayotawala mji mdogo wa kyela haitaki kabisa ujinga huu .
 

Attachments

  • attachment-14.jpeg
    attachment-14.jpeg
    10.4 KB · Views: 511
Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa anatarajiwa kuzindua visima sita vya maji katika jimbo la Kyela.

Akizungumza na wanahabari kiongozi wa Chadema Kyela na Mjumbe wa mkutano mkuu Taifa Abraham Mwamanyaki amesema visima hivyo vimefufuliwa na Chadema mara tu baada ya kupata ushindi mkubwa kwenye uchaguzi wa Vijiji na kufanikiwa kuongoza halmashauri ya mji wa Kyela.

Mbunge wa Kyela Harrison Mwakyembe na CCM yenye madiwani wengi walishindwa kufufua visima hivyo kwa madai hamna hela kutokana na ufisadi mkubwa uliopo ndani ya Halmashauri hiyo.

Dr Slaa amealikwa kuzindua visima hivyo kutokana na maombi ya wananchi wa Kyela ambao wana imani kubwa Dr Slaa ndiye atakayekuwa Rais wa awamu ya tano.

Chadema wanavyohangaika kama vile kuku anataka kutaga.visima hivi vimejengwa na serikali sasa iweje mwanasiasa akazindua?
 
Ni bahati kubwa sana kwa wana Kyela kutembelewa na mkombozi huyu , huyu mtu anatakiwa kila mahali kwenye nchi hii , Mungu amlinde sana .

Aisee, ni kweli Slaa anatakiwa kila mahali, hasa anatafutwa na wale aliowaibia wake zao, hiyo ni kweli anatakiwa sana.
 
Mkuu molemo Mungu akubariki sana kwa habari hii njema sana kwa sisi wanakyela , japokuwa sijapata lunch bado lakini kwa uzi huu nahisi kushiba mno ! Asante Dr Slaa kwa kuwarudishia wana kyela japo muda wako tu , ikumbukwe kwamba Dr slaa ni rais wa kyela , ALISHINDA KWA KISHINDO 2010 .
Mkuu samahani naomba kuuliza.
Hivi hizi sifa mnazommwagia Slaa huwa ni jokes au mko Serious?
 
Mkuu samahani naomba kuuliza.
Hivi hizi sifa mnazommwagia Slaa huwa ni jokes au mko Serious?
Dr Slaa alishinda kwa kishindo
kyela mwaka 2010 alimuacha jk kwa mbali sana , tafuta matokeo ujiridhishe mwenyewe au muulize jk mwenyewe au hata mwakyembe , hakuna wasichokijua , sisi wana kyela tunajua kwamba tulimchagua Dr slaa .
 
Ni bahati kubwa sana kwa wana Kyela kutembelewa na mkombozi huyu , huyu mtu anatakiwa kila mahali kwenye nchi hii , Mungu amlinde sana .

Amina Kamanda.Mungu atasikiliza sala yako hii..
 
Chadema wanavyohangaika kama vile kuku anataka kutaga.visima hivi vimejengwa na serikali sasa iweje mwanasiasa akazindua?

Wanaohangaika ni wananchi wa Kyela wanaohitaji Ukombozi
 
Visima 6 ndio miradi ya maji? acheni utani hii nchi kubwa hata Sabodo aliwapa mtonyo wa visima 100. Watu wa Kyela kweli siku hizi ndio wamekuwa wepesi hivi, siamini kule wako vizuri na kukarabati visima sita ndio mudhalilishe hivi mkiwajengea barabara ya lami si ndio mtawavua na nguo kabisa.

Ukirudia mara 2 kusoma ulichoandika utagundua uwezo wa ubongo wako ni sawa na wa kondoo.
 
Mm ni mmoja kati ya familia nyingi zilizo kuwa zimeathirika kwa kukosa maji hapa Kyela Mbugani nyumbani kwangu!Tulikuwa tunaamka saa 8 usiku kwenda kutafuta maji!

CHADEMA ndani ya week maji kila sehemu yapo,naamka saa 1 asubuhi maji yapo na hakuna tena kuamka usiku na giza totoro

Kwa hili walilofanya CHADEMA ndani ya week wanastahili mno pongezi maana CCM liliwashinda kwa miaka

At least sasa tunafaidi ndoa zetu maana "Mama" hatuamki tena usiku wa mnene kutafuta maji tukiwaacha wake zetu vitandani

Asante sana kwa ushuhuda huu Kamanda.
 
hongera dr slaa nakumbuka enzi zile karatu ccm walisema maji karatu hakuna.uliposhda ubunge ukatuletea maji.hongera sna

Karatu ndiyo Jimbo pekee Tanzania ambalo shida ya maji ni historia.Kazi iliyofanywa na Dr Slaa.
 
Back
Top Bottom