TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Nimepita katika group moja katika facebook nikakuta kuna post ambayo inazungumzia tuhuma za ufisadi uliofanywa na watu mbalimbali kutoka vyama vya upinzani akiwemo Dr Slaa..,si vibaya tuhuma hizi nikizileta hapa jamvini kwa kuwa Dr Slaa yupo na naamini wapo pia watu wenye uelewa katika haya yaliyozungumzwa wanaweza kuchangia ama kusaidia katika kukanusha ama kusahihisha ama kukiri tuhuma hizi..,
extracted from TANURI LA FIKRA
Kuchukua tuhuma za mwanachama na kuivesha tuhuma hiyo kwa chama ni makosa na hili linafanywa makusudi na wapinzani ili waendelee kichafua CCM.,haiwezekani ufisadi unasibishwe na CCM hali ya kuwa katika kila chama watu wa AINA hiyo wapo; Nikianza moja kwa moja na katibu mkuu na mgombea URAIS wa chadema Bwana WILBROD SLAA ambaye ni kiongozi mkuu wa taasisi ya CCBRT (katibu wa bodi ya wakurugenzi) ambayo inapatiwa ruzuku ya shilingi za kitanzania; 1,000,000,000/= kutoka kwa serikali kila mwaka kwa kuiendeleza taasisi hiyo kwa manufaa ya watanzania wote na taifa kwa ujumla na pia inapata misaada na harambee mbalimbali kutoka kwa watu binafsi na mashirika makubwa ndani na nje ya TANZANIA kama EUROPEAN UNION,IRISH AID, AUSTRARIAN GVT, AusAID, CBM, JOHNSON&JOHNSON nk, ili kuwaendeleza watanzania katika nyanja ya afya,.tofauti na malengo hayo taasisi hii chini ya Dr Slaa imekuwa ikitoa huduma za jamii kwa ubaguzi mkubwa na kukosekana kwa usawa; nitabainisha kama ifuatavyo;
a) Wagonjwa wanaotibiwa kwa mwaka wanakadiriwa kufika 1,080,000 katika hawa zaidi ya nusu ni kutoka katika mikoa ya kasikazini ikiongozwa na moshi na arusha.(branch ya CCBRT iko moshi)
b) Operesheni zilizofanywa kati ya mwaka 2003-2007 ni kama ifuatavyo.,macho 31,200 napo pia zaidi ya nusu ya wagonjwa walitoka maeneo hayo. Mimi sidhani kuwa moshi kuna watu wenye matatizo ya macho zaidi ya Dodoma, Singida na sehemu nyingine za tanzania ya kati.
c) Operesheni za orthopaedic&plastic surgery kati ya 2003-2007 ni 6,520 bado wagonjwa wengi walitokea kaskazini
d) Na waathirika waliokuwa wakihudumiwa na CCBRT kati ya 2003-2007 zaidi ya 60% ni kutoka mikoa ya Arusha na Kilimanjaro (ripoti ya Tom Varnneste 24 jully 2008)
e) Taasisi hii pia inakadiriwa kuwa na waajiriwa 320 napo hapa ni uchaga, na ukaskazini umetawala, mchakato wa uajiri ukisaidiwa na Jacqueline Kweka(Advocacy Officer) uliona kuwa hakuna watu waliosoma na kustahili kufanya kazi CCBRT ila ni wachaga na watu wa kanda ya kaskazini. Katika utafiti uliosimamiwa na CCBRT, Radar development pamoja na DISABILITY AID ABROAD umeonyesha kuwa ni asilimia 0.7% ya waajiriwa ndio watu wenye ulemavu(CCBRT ikiwemo kwa kutoajiri walemavu ingawa ni taasisi ya kusimamia walemavu nchini)
f) Lakini kama hilo halitoshi gharama za matibabu ni za juu sana katika hospitali zilizo chini ya CCBRT, takwimu zipo; Gharama ya matibabu kwa CCBRT mtu binafsi anatakiwa kulipa kati ya dola 400-714 sawa na 600,000-1,071,000/= gharama hii ni kubwa ajabu kulingana na pato la kawaida la mtanzania na pia ni gharama ya juu hata kuzidi hospitali zingine hapa nchini ambazo hazipati msaada serikali wala mashirika makubwa ya nje na pia hazifanyiwi harambee kama CCBRT.,mfano CATARACT SURGERY HINDU MANDAL 400,000/=, AGA KHAN 315,000/= REGENCY 300,000/= MISSION MIKOCHENI 180,000 WAKATI CCBRT 680,000(Tom Venneste Appendix iii-nov 2008)
Pia CCBRT imekuwa haiko tayari kuwa wawazi juu ya kiasi cha mapato kinachochangiwa kutoka katika taasisi hizi kubwa duniani (dalili kubwa ya kuwepo ufisadi ndani yake)
Ama ukiacha hayo ambayo yanamgusa moja kwa moja Dr Slaa, pia kuna yanayowahusu viongozi wengine wa CHADEMA kama vile DIWANI WA KATA YA SERENGETI,MKOANI MARA KUKAMATWA AKIMILIKI AK47 KINYUME CHA SHERIA kiuhalisia huu pia ni ufisadi na hata yule MBUNGE WA CUF ALIYESHUTUMIWA KUINGIZA NCHINI MAGARI YA WIZI NA KISHA KUKWEPA KODI huu pia ni ufisadi ila inapotokea mambo kama haya yakifanywa na viongozi au wanachama wa CCM yatatangazwa vyombo vyote vya habari na pia suala hilo litabebeshwa kwa chama badala ya mtu binafsi.
extracted from TANURI LA FIKRA
Kuchukua tuhuma za mwanachama na kuivesha tuhuma hiyo kwa chama ni makosa na hili linafanywa makusudi na wapinzani ili waendelee kichafua CCM.,haiwezekani ufisadi unasibishwe na CCM hali ya kuwa katika kila chama watu wa AINA hiyo wapo; Nikianza moja kwa moja na katibu mkuu na mgombea URAIS wa chadema Bwana WILBROD SLAA ambaye ni kiongozi mkuu wa taasisi ya CCBRT (katibu wa bodi ya wakurugenzi) ambayo inapatiwa ruzuku ya shilingi za kitanzania; 1,000,000,000/= kutoka kwa serikali kila mwaka kwa kuiendeleza taasisi hiyo kwa manufaa ya watanzania wote na taifa kwa ujumla na pia inapata misaada na harambee mbalimbali kutoka kwa watu binafsi na mashirika makubwa ndani na nje ya TANZANIA kama EUROPEAN UNION,IRISH AID, AUSTRARIAN GVT, AusAID, CBM, JOHNSON&JOHNSON nk, ili kuwaendeleza watanzania katika nyanja ya afya,.tofauti na malengo hayo taasisi hii chini ya Dr Slaa imekuwa ikitoa huduma za jamii kwa ubaguzi mkubwa na kukosekana kwa usawa; nitabainisha kama ifuatavyo;
a) Wagonjwa wanaotibiwa kwa mwaka wanakadiriwa kufika 1,080,000 katika hawa zaidi ya nusu ni kutoka katika mikoa ya kasikazini ikiongozwa na moshi na arusha.(branch ya CCBRT iko moshi)
b) Operesheni zilizofanywa kati ya mwaka 2003-2007 ni kama ifuatavyo.,macho 31,200 napo pia zaidi ya nusu ya wagonjwa walitoka maeneo hayo. Mimi sidhani kuwa moshi kuna watu wenye matatizo ya macho zaidi ya Dodoma, Singida na sehemu nyingine za tanzania ya kati.
c) Operesheni za orthopaedic&plastic surgery kati ya 2003-2007 ni 6,520 bado wagonjwa wengi walitokea kaskazini
d) Na waathirika waliokuwa wakihudumiwa na CCBRT kati ya 2003-2007 zaidi ya 60% ni kutoka mikoa ya Arusha na Kilimanjaro (ripoti ya Tom Varnneste 24 jully 2008)
e) Taasisi hii pia inakadiriwa kuwa na waajiriwa 320 napo hapa ni uchaga, na ukaskazini umetawala, mchakato wa uajiri ukisaidiwa na Jacqueline Kweka(Advocacy Officer) uliona kuwa hakuna watu waliosoma na kustahili kufanya kazi CCBRT ila ni wachaga na watu wa kanda ya kaskazini. Katika utafiti uliosimamiwa na CCBRT, Radar development pamoja na DISABILITY AID ABROAD umeonyesha kuwa ni asilimia 0.7% ya waajiriwa ndio watu wenye ulemavu(CCBRT ikiwemo kwa kutoajiri walemavu ingawa ni taasisi ya kusimamia walemavu nchini)
f) Lakini kama hilo halitoshi gharama za matibabu ni za juu sana katika hospitali zilizo chini ya CCBRT, takwimu zipo; Gharama ya matibabu kwa CCBRT mtu binafsi anatakiwa kulipa kati ya dola 400-714 sawa na 600,000-1,071,000/= gharama hii ni kubwa ajabu kulingana na pato la kawaida la mtanzania na pia ni gharama ya juu hata kuzidi hospitali zingine hapa nchini ambazo hazipati msaada serikali wala mashirika makubwa ya nje na pia hazifanyiwi harambee kama CCBRT.,mfano CATARACT SURGERY HINDU MANDAL 400,000/=, AGA KHAN 315,000/= REGENCY 300,000/= MISSION MIKOCHENI 180,000 WAKATI CCBRT 680,000(Tom Venneste Appendix iii-nov 2008)
Pia CCBRT imekuwa haiko tayari kuwa wawazi juu ya kiasi cha mapato kinachochangiwa kutoka katika taasisi hizi kubwa duniani (dalili kubwa ya kuwepo ufisadi ndani yake)
Ama ukiacha hayo ambayo yanamgusa moja kwa moja Dr Slaa, pia kuna yanayowahusu viongozi wengine wa CHADEMA kama vile DIWANI WA KATA YA SERENGETI,MKOANI MARA KUKAMATWA AKIMILIKI AK47 KINYUME CHA SHERIA kiuhalisia huu pia ni ufisadi na hata yule MBUNGE WA CUF ALIYESHUTUMIWA KUINGIZA NCHINI MAGARI YA WIZI NA KISHA KUKWEPA KODI huu pia ni ufisadi ila inapotokea mambo kama haya yakifanywa na viongozi au wanachama wa CCM yatatangazwa vyombo vyote vya habari na pia suala hilo litabebeshwa kwa chama badala ya mtu binafsi.