Wote tunajua kuwa moja ya sababu kubwa ya watanzania wengi hasa wale wenye upeo wa kiasi fulani kuhusu siasa zetu na historia ya harakati za demokrasia ya vyama vingi hadi sasa kushindwa kuamini katika ukombozi wa CHADEMA ni sura ya chama hicho inayowakilishwa na Mwenyekiti wake Freeman Mbowe.
Kwa mtazamoa wa wengi wajuvi wa siasa zetu lakini hata wale wengine wasio na kujua sana, Freeman Mbowe si mwanasiasa bali mjasiria mali ambaye kwake siasa ni mtaji wa biashara zake. Lakini zaidi biashara zake hasa lile danguro la Mbowe na baadae Bilicannas, ni mzigo mkubwa kwa Chadema katika jitihada zake za kujenga imani miongoni mwa watanzania wenye nia ya dhati ya kutaka kuona tunakuwa na MBADALA BORA utakaoweza kuondoa na kutufanya tusahau HISTORIA mbaya ambayo CCM imetupitisha katika miaka ya hivi karibuni.
Hata hivyo moja ya vitu vilivyokuwa vinatupa imani kwa kiasi na CHADEMA ni kuwepo kwa mtu kama Dr Slaa ambaye wengi tulikuwa tunadhani kuwa ni mtu muungwana na muadilifu na pia wa kiasi fulani hasa upande wa vijana ni umahiri wa wabunge wake vijana wakiongozwa na Zitto Kabwe.
Wote hawa walikuwa nguzo muhimu za imani ya watanzania kwa CHADEMA. Nasikitika kusema kuwa tangia uchaguzi uliopita kuanza, nguzo hizi zimeanza ama kuregea ama kubomoka kabisa.
Ukianzia baadhi ya matamshi ya Dr Slaa wakati uchaguzi, Sakata ama kashfa ya hawara ama mke wa mtu, ukaja hoja za kutomtambua rais bila ya kutoa ama kuonyesha ushahidi wa kutosha na sasa haya yanayoaandikwa kuhusu Zitto Kabwe kwa upande mmoja na kauli za Dr Slaa zinazojaribu kukwepa ukweli kuwa msimamo wa Kamati Kuu ya Chadema ni tofauti na ule waliouita msimamo wa chama hapo awali, yote haya yanaelekea kubomoa imani kiasi ambayo watanzania waliweka katika CHADEMA.
Hapa chini ni kile kinahodaiwa kuwa ndio msimamo wa CHADEMA uliotolewa na Dr Slaa kuelezea sakata hili la sasa la Msimamo wa Kamati Kuu Vs Msimamo wao ambao inaonyesha wazi kuwa Dr Slaa anakwepa kukubali kuwa msimamo wa awali ulikuwa tofauti na msimamo wa sasa ambao umetolewa na kamati kuu.
Itakuwa vizuri kama tutajikumbusha kauli hizi hapa chini ambazo zilitolewa hapa Jamiiforum kwa kutumia ID ya Dr Slaa...
Ya kwanza ni hii ambayo ilitolewa siku ya pili baada ya wabunge wa CHADEMA kususia hotuba ya JK yaani tarehe 18/12/2010. Hi ilikuwa kama transcription ya taarifa ya Dr Slaa redioni jioni tu ya siku ile ya kumsusia JK.
Ya pili, ni hii iliyotolewa tena katika ID ya Dr Slaa siku iliyofuata yaani tarehe 19/12/2010.
Jamani. Uungwana nao waweza kuwa mtaji mkubwa kisiasa. Jaribuni hili la kukubalia kuwa tulikosea na sasa tupo tayari kujisahihisha. Hapa sio Kabwe tu atakayekuwa mshindi, Chadema na haswa Dr Slaa atarudisha na kulinda heshima yake lakini sio huu mchezo unaofanyika sasa ambao ni tofauti na fikira zetu kuhusu Dr Slaa.