Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,580
- 18,227
Huo ni uoga na kutojikubali, mabadiliko hayaletwi kwa kujificha ficha ughaibuni, waje nyumbani wafanye mabadiliko yale wanayoyaona yanahitajika kufanyika, badala ya kuwa vivuli na kufanya mambo nyuma ya migongo ya watu, ma diaspora wote warudi nyumbani, tunahitaji utaalamu wao, na experience zao kujenga nchi yetu, wakija 500 na wakafanya mambo makubwa hapa nyumbani huoni itakua jambo lamaana?? sio lazima wote waajiriwe serikalini au wote wawe viongozi, hapana wanaweza fanya michango yao wakiwa kwenye sekta binafsi ikaeleweka..fimbo ya mbali haiui nyoka, watafanya vizuri zaidi wakiwa hapa kuliko huko..
Unaandika kama illiterate fulani asiyekua na exposure yoyote.
Naomba kwanza ufuatilie Kenya,Israel,India,China na Nigeria unimbie Diaspora wana mchango kiasi gani kwa mwaka ndiyo uje hapa na hizi rants zako.
Waliopo Ughaibuni watafanya kazi kwa ufanisi ikiwa serikali inaandaa mazingira rafiki
Leo nenda pale BRELA uniambie kuhusu Urasimu Mbaya uliopo wa kusajili Makampuni Kulinganisha na Rwanda au Kenya.
Fikiria nje ya Box