Dr. Slaa: Hakuna huruma kwa wabunge wala rushwa

Bora mmejua kua mwisho wa siku binadamu ni binadamu tu awe kutoka ccm au cdm wote ni wezi na wote ni wala rushwa.. Kuna siku nilisema cdm wakichukua nchi na wao wataiba ka ccm nikashambuliwa hapa haya tumejionea wenyewe.. Kuna msemo unasema 'its better the devil you know'

Hauwezi kutumia issue iliyopo kusema kwamba CHADEMA wataiba kama CCM. CCM inajurikana kama taasisi kwamba inashiriki rasmi kabisa kwenye rushwa, mfano wizi wa fedha za EPA ulibarikiwa na viongozi waandamizi wa CCM kwa ajili ya manufaa yake kisiasa.sitegemi kwa siku za hapa karibuni mpaka kufikia miaka ishirini ijayo kama CHADEMA kinaweza kutumbukia kwenye uchafu wa namna hii. Nitakitetea chama hiki kwa nguvu zangu zote katika hili.

Lakini swala la wanachama wake, kwa hurka zao za kibinaadamu kuweza kushiriki kwenye matendo ya rushwa, sitegemei mtu kushtushwa na hilo, wanaweza na katika hili inawezekana kabisa kabisa kwamba wapo wabunge wa CHADEMA ambao wamekengeuka tayari ni kupokea rushwa.

Ninachokisubiri ni kuona chama kitawachukulia hatua gani. Kwa upande wa CCM najua hakuna hatua zozote zitakazochukuliwa na katika hili niko tayari kupinga. Na ninapinga kama unabisha tegua.
 
Slaa ufisadi ni hulka, hata wewe kuhonga ubunge wa viti maalumu ni ufisadi tu. Ufisadi haukubaliki na chama chochote, sasa toeni boriti kwenye jicho lenu kwanza
 
Nafasi ya cdm kula kama ccm haitakuwepo. Katiba inabadilishwa, mambo yatakuwa magumu sana wala isiwe kula nchi ndio motive ya cdm, hawatajaaliwa hilo. Tutakuwa tuna uwezo wa kumshtaki hata rais wa nchi. Utawala ujao utakuwa mgumu kwa mtu yeyote atakaekuwa madarakani.
 
TL Kipindi kile alimsihi sana ZK Alipo teuliwa na JK kuwa mwanakamati kwenye tume ya madini, Akatae ule uteuzi! ZK hakumuelewa TL!
Sasa nimeamini jinsi magamba walivyo! Yaani wanakupa kamba ndefu ukajinyonge mwenyewe! ukipewa kamba fupi utapata kisingizi kuwa sikujinyonga kamba ilikuwa fupi! TL Unaupeo mkubwa!
 
Dr Slaa amebakia kuwa mtu wa kudandia matukio na kuyatolea kauli za ajabu ili aendelee kusikika kwa wananchi kwamba bado yupo kwenye harakati za kisiasa..

Dr Slaa kila siku unatoa mara kauli unaipa wiki serikali kutoa hukumu kwa mafisadi linapokuja kuhongwa kwa wabunge wa Chadema unaleta siasa eti tunaitaji tupate maelezo ya kina chama chetu hakikurupuki kama akitajwa atawajibishwa kupitia kikao cha CC ya chama.

Dar Slaa anasema anasubiri taarifa kutoka kwa Mbowe sasa sijui unasubiri taarifa gani wakati huwezi kufukuza wala rushwa ndani ya chama chako kwa hiyo kama Mbowe naye yumo utafanyaje.

Huu ushauri Ritz ulipashwa kumpelekea mukama.
Dr. Slaa haitaji kushauriwa na gamba juu ya jambo lolote linalohusu ustawi wa nchi ama ustawi wa Chadema. Hayo mambo tuachie sisi wenyewe ndio tunajua nini cha kumshauri kiongozi wetu.
Na kama kuna mtu yeyote atabainika kula mpunga lazima ang'olewe hata kama ni mzito ama mwepesi kiasi gani. Wasiwasi wetu ni juu ya chama cha mabwepande kama mtathubutu kuwawajibisha wala rushwa wenzenu, kwakuwa hiyo ni jadi yenu kuvuta mpunga.
 
Last edited by a moderator:
Osokoni hatimaye umesema kweli. Aunde chama cha Kigoma Democratic Party na aachane na chama cha CHAGGA DEVELOPMENT MANIFESTO(chadema). Chadema habari yenu kwisha. Tafuteni chaka lingine.
 
kiongozi mkuu wa upinzani nchini ambaye pia ni katibu mkuu wa chadema, dk willibrod slaa alisema:

“nalaani kitendo cha wabunge kuhusishwa na ufisadi hasa ikizingatiwa kwamba chadema tumekuwa tukiupinga vikali. Tumekuwa tukipinga rushwa kwa sababu ndiyo inayoielekeza nchi pabaya… chadema hatufumbii macho rushwa.”

alisema tangu kuanza bunge la 10, chadema kimekuwa kikiona baadhi ya mambo yanayoendelea katika mhimili huo muhimu wa dola yamejaa walakini...

“ndiyo maana sisi chadema tumekuwa tukisema bunge limepoteza mwelekeo.”

alisema akiwa mtendaji mkuu wa chama, anasubiri taarifa kamili kutoka katika kikao cha wabunge wa chama hicho ili kuweka wazi majina ya wahusika na kisha kufuatiwa na kikao cha kamati kuu (cc) ambacho kitakaa na kuchukua hatua kali.

“tunahitaji tupate maelezo ya kina... Chama chetu hakikurupuki… nasubiri taarifa ya kokasi ya chama. Katiba ya chadema inatambua uwapo wa kikao cha wabunge wetu na kwa bahati nzuri, kiongozi wake mkuu ni mwenyekiti wa chadema (freeman mbowe) na katibu (david) silinde ni mbunge wetu. Tunasubiri taarifa yao.”

alisema chadema kina kanuni ya kudhibiti rushwa hivyo, mbunge wake akitajwa miongoni mwa wanaohusishwa na rushwa, atawajibishwa kupitia kikao cha cc ya chama hicho.

source: mwananchi jumatatu
raisi wangu kaongea duu huwa napenda kweli kumsikia huyu mtu!
 
Kila atakaye toa shutma haje na prove mezani sio kelele hambazo hazina mantiki.
 
Zitto asisubiri kufukuzwa ajitoe mwenyewe mwizi mkubwa huyu! aende kujiunga na rafiki yake kafulila waunde chama cha kigoma democratic party asiendelee kutuchafulia chama!!

da...... subirieni ithibitike kama amepewa mlungula. ila na dhani mambo mengine sio lazima kwenda mbali kote hoko kwenye kamati, mwenye akili timamu anajua ZITO ni mtu safi.... Tena kuliko SILAA
 
Nafasi ya cdm kula kama ccm haitakuwepo. Katiba inabadilishwa, mambo yatakuwa magumu sana wala isiwe kula nchi ndio motive ya cdm, hawatajaaliwa hilo. Tutakuwa tuna uwezo wa kumshtaki hata rais wa nchi. Utawala ujao utakuwa mgumu kwa mtu yeyote atakaekuwa madarakani.

pop hicho ndo CDM wanataka. hakuna kuiba iba hovyo mali za nchi. nakushukuru kwa kulijua hilo.
 
Bora mmejua kua mwisho wa siku binadamu ni binadamu tu awe kutoka ccm au cdm wote ni wezi na wote ni wala rushwa.. Kuna siku nilisema cdm wakichukua nchi na wao wataiba ka ccm nikashambuliwa hapa haya tumejionea wenyewe.. Kuna msemo unasema 'its better the devil you know'

Napinga hiyo kauli. Mwisho wa siku kinachotakiwa ni "checks and balance" na si kwamba kuna chama ambacho kitakuwa na viongozi wote "malaika". Suluhisho ni kuwa na upinzani wenye nguvu. Kikitawala CCM basi kuwepo na upinzani wenye nguvu wa kukikosoa (kama CHADEMA inavyofanya kwa sasa); na kama CHADEMA au chama kingine kitatawala, basi CCM au chama kingine kiwe na nguvu ya kukikosoa.

Opportunity makes a thief, ndivyo waingereza wasemavyo. Wanadamu wote tumeumbwa wabinafsi kwa asili.
 
Bora mmejua kua mwisho wa siku binadamu ni binadamu tu awe kutoka ccm au cdm wote ni wezi na wote ni wala rushwa.. Kuna siku nilisema cdm wakichukua nchi na wao wataiba ka ccm nikashambuliwa hapa haya tumejionea wenyewe.. Kuna msemo unasema 'its better the devil you know'

You sound like Zomba or zombie
 
Napinga hiyo kauli. Mwisho wa siku kinachotakiwa ni "checks and balance" na si kwamba kuna chama ambacho kitakuwa na viongozi wote "malaika". Suluhisho ni kuwa na upinzani wenye nguvu. Kikitawala CCM basi kuwepo na upinzani wenye nguvu wa kukikosoa (kama CHADEMA inavyofanya kwa sasa); na kama CHADEMA au chama kingine kitatawala, basi CCM au chama kingine kiwe na nguvu ya kukikosoa.

Opportunity makes a thief, ndivyo waingereza wasemavyo. Wanadamu wote tumeumbwa wabinafsi kwa asili.


Kumbe ndiyo maana mnaitwa NSHOMILEEEEEE! JF inatakiwa kujibu hoja kwa makini ama kuelimisha kama hivi siyo kukurupuka utafikiri tuko ngomani.
Wakora waitu
 
chadema ni chama makini kina uzoefu wa kufukuza wanachama hasa wanaokwenda kinyume na taratibu za chama, watanzania hawakuamini kama CDM wangeweza kuwafukuza madiwani wake arusha.Sasa ni zamu ya zitto, the guy must go.japo ni machungu kumpoteza lakini hakuna jinsi lazima aende zake.CDM wansafisha njia kuelekea kukamata dola chama hakitaweza kukamata dola kikiwa na mafisadi ndani
 
maadili ya chama kama mlezi wa viongozi wa kisiasa yana walakini.
Chadema lazima wawe na sheria za kudhibiti wezi, mafisadi, wala rushwa na wazembe ndani ya chama. Je Chadema ina kumbu kumbu za mali za viongozi wake na wabunge ili kujua kama ni za halali au za mkato???

Bila kuwa na uwezo wa kuwajua viongozi na vyazo vyao vya fedha kuna hatari tukalea mafisadi bila kutambua.

Wabunge wa Chadema ambao tayari wametuhumiwa na bungeni sidhani kama kuna haja ya kusubiri bunge la mafisadi kujadili mafisadi, kuna haja ya kuwaita na kuwahoji huku wakipata uhakika kutoka kwa waziri husika mwenye ushahidi na sehemu mbali mabali.

Kama tuliweza kupata habari za EPA, Buzwagi, nk kwa nini tushindwe kupata habari za hawa ambao wako ndani ya uwezo wetu.

Watuhumiwa wa rushwa wafukuzwe chama kwani hawafai tena na hawatafaa tena ndani ya chama.

Wito sio sahihi kuanza kuhisi mbunge kwa sababu zozote zile. Chama kina wajibu wa kututajia majina kwani Spika, waziri wanaushahidi na majina ya wahusika.
 
Back
Top Bottom