ZeMarcopolo,
Inawezekana ID imevamiwa na 'zuzu' la mtaani, maana haingii akilini kuwa unaweza kuandika hoja dhaifu kiasi hiki, imajaa contradiction.
Tuanze:Msingi wa hoja yako ni, 'Dr. Slaa kusema kuwa matendo ya serikali ya CCM ni sawa na mfumo wa apartheid wa makaburu wa Afrika ya Kusini.'
Tunajua Apartheid - ni mfumo wa kibaguzi kati ya mwa mwanadamu mmoja na mwingine kutokana na vigezo anavyoweka yeye 'mgabuzi', mfano Makaburi wa Afrika ya Kusini waliwabagua watu wale wote ambao hawakuwa na rangi nyeupe - yaani wazungu. Hapa Wahindi na Weusi (Waafrika) waliwekwa daraja la chini, na hivyo hawakuwa na haki sawa na wazungu kwa sababu tu ya rangi zao. Iwe elimu, matibabu, usafiri, na hata kupiga kura, Makaburu wa Afrika ya Kusini waliwapora haki watu waliowaona ni daraja la chini.
Chama cha Mapinduzi - kama kilivyokuwa TANU - kiliundwa kwa misingi ya kutombagua binadamu mwenzio kwa namna yoyote ile, na ndio zamani (kwa waliokula chumvi) tulikuwa tunaimba binadamu wote ni sawa. Na tukaenda mbele zaidi kwa kuitana NDUGU fulani. Hali ikoje sasa?
Kwanza tuna waheshimiwa! (ubaguzi). Kama mtu si mheshimiwa anakuwa nani? Na ana haki sawa na Mheshimiwa? Jibu- hapana. Kwa sasa tuna mfumo ambao watu fulani wana haki ya kutibiwa India, Afrika ya Kusini na kwingineko ambako wanaona 'kunawafaa' kwa fedha ya umma, lakini wengine wanapiga miayo kwenye Zahati ambao hata Asprin hakuna!. (ubaguzi)
Kwa sasa, kuna mfumo ambao watu fulani wakitaka kufanya medical check-up wanapanda ndege, lakini wakina mama wanajifungulia sakafuni! (Ubaguzi)
Kwa sasa tuna mfumo amabo baadhi ya watoto wanapitiwa na vibasi asubuhi wanapelekwa shule za St. St ... wakati wengine watembea 4km kwenda shule ambayo ni mbavu za mbwa na wanakalia mawe, hapo hujaongelea walimu. (ubaguzi).
Zamani mtoto wa mama ntilie alikuwa anasoma shule moja - darasa moja na mtoto wa rais. (pitia orodha kwenye shule mfano Weruweru, Pugu, Ilboru, Umbwe Secondary, n.k. utakuta majina ya watoto wa viongozi wa juu kabisa enzi hizo!
Zamani kulikuwa na mfumo ambao vyombo vya dola villikuwa vinamlinda kila raia na mali yake - mwenye kipato cha juu au cha chini, lakini sasa vyombo vya dola (i.e. polisi) vimekuwa ni kero kwa walala hoi (Soweto)
Mfumo wa sasa ambao umejaa kasoro unawanyima raia haki ya msingi ya kupiga kura (pitia Hansard za bunge). Kule Zanzibar Sheha anaamua nani ana haki ya kupiga kura na nani hana haki, na kwa kiasi kikubwa maamuzi yake yanaegemea kwenye itikadi za siasa. (ukaburu)
Mtu anapofananisha mfumo wa sasa na Apartheid ni kwa sababu haki za msingi zinatolewa kwa kimatabaka. Mzee Mandela alipinga matabaka, TANU ilipinga matabaka na hata CCM (ya Mwl Nyerere) kiliyapinga matabaka.
Kule Mara kuna watu wako korokoroni kwa sababu tu ya matabaka ya kisiasa. Kimatendo, mfumo wa nchi hii kwa sasa umejaa ubaguzi. Kwanini wagonjwa walale chini sakafuni, wakati wengine wanapelekwa India?