Dr. Slaa ni mwanasiasa mlaghai.
Siku za hizi karibuni Dr. Slaa amekuwa akisema maneno bila kupima maana na ujumbe unaobebwa na maneno hayo.
Matokeo yake, Dr. Slaa amekuwa sababu ya mitafaruku kutokana na kauli zake.
Hali hiyo tuliishuhudia hata hapa JF ambapo sasa hivi Dr. Slaa anapaogopa kama ukoma kutokana na wadau kuwa wakali kwa kauli zake.
Kiujumla kauli za Dr. Slaa huwa zina madhumuni ya kuwalaghai wale watakaozisikia. Hata hivyo Slaa anapaswa kupima kiasi cha ulaghai anachokitumia kwa sababu sasa ameanza kupitiliza.
Akitoa salam za rambirambi kwa kifo cha aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini na Kiongozi wa ANC Mzee Nelson Mandela, Dr. Slaa ametamka kuwa matendo ya serikali ya CCM ni sawa na mfumo wa apartheid wa makaburu wa Afrika ya Kusini.
Kauli hii iliyolenga kulaghai watu (kwa sababu Slaa anajua kuwa anachosema sio ukweli au more correctly ni uongo) ina madhara makubwa kwa namna mbili.
Kwanza ni kupunguza uzito wa mateso waliyopata watu weusi wa Afrika ya Kusini, ambao hata kupiga kura walikuwa hawaruhusiwi. Slaa anaposema kuwa maisha ya watu wa Afrika ya Kusini kipindi cha ubaguzi wa rangi ni sawa na maisha ya watanzania wa leo chini ya serikali ya CCM anamaanisha kwamba watu weusi walikuwa wanalalamika bure bila kuwa na sababu ya msingi. Hapohapo anasahau kuwa yeye, Slaa, hajafungwa kama Mandela na wanasiasa wengine wa Afrika Kusini. Slaa anapata ulinzi wa polisi, anagombea Urais na kufanya kampeni kwa uhuru, lakini kwa vile tu ameshindwa kupata kura za kumfanya awe Rais, basi anaona hiyo ni kero sawa na apartheid!!!
Katikia hili Slaa, pengine bila kujua, anajiunga na wale wanaomuweka Mandela kwenye kundi la magaidi wasiostahili heshima yoyote. Katika mtandao wa CNN kuna wachangiaji wengi wenye mrengo huu wa Dr. Slaa. Mifano yake ni hii hapa chini.
JimmyBoston • 2 days ago
Mandela is dead. What scares me the most is the people on this board, left leaning liberals, who find the murder of innocent people, going about their daily business, as acceptable to promote a Socialist cause. It sickens me.
Confucius Say • 2 days ago
Whatever Mandela's reasonings, and they are questionable, his methods were criminal. He gave orders to plant I.E.D's and they killed innocent people. Women and children. Over 80% black. How can we be so blind as to forget that? Whatever the cause the means were beyond wrong and to celebrate this man is a shame. To simply gloss over or completely ignore this is atrocious. Church Street Bombings, look it up people. Stop drinking the Kool Aid and do some research.
Kwa mifano zaidi ya comments zinazofanana na hiyo na ya Dr. Slaa soma hapa
http://edition.cnn.com/2013/12/05/world/africa/nelson-mandela-
humor/index.html#disqus_thread
Wenye maoni ya namna hii, yanayofanana na kile alichosema Dr. Slaa, ni watu ambao wanadhani mfumo wa ubaguzi wa rangi (apartheid) unaweza kufananishwa na maisha ya kawaida ya mtanzania wa leo, kama jinsi alivyofananisha Dr. Slaa. Pengine tunaweza kumvumilia hawa wamarekani walioandika hivyo kwenye mtandao wa CNN kwa vile hata ukiwaonyesha ramani ya dunia wanaweza kupata shida kuonyesha Afrika ya Kusini iko wapi kwenye ramani hiyo. Tatizo ni pale mwafrika mtanzania mwanasiasa wa ngazi ya kitaifa anapofananisha ubaguzi wa rangi wa Afrika ya Kusini na maisha ya mtanzania wa leo!!!
Wamarekani hawa wanafananisha mfumo wa apartheid na changamoto wanazokutana nazo kila siku kwenye maisha yao ya Marekani ya leo. Slaa anafananisha mfumo wa apartheid na changamoto za kisiasa anazokutana nazo katika maisha yake ya Tanzania ya leo. Slaa na wachangiaji hawa wote WAMEPOTOKA...
Tatizo la pili katika kauli ya Dr. Slaa ni kwamba inawasafisha makaburu mbele ya macho ya vijana wa leo. Unapomwambia kijana wa kizazi cha sasa kuwa mfumo wa ubaguzi wa rangi, apartheid, ulikuwa ni sawa na jinsi CCM inavyoongoza Tanzania, unampa ujumbe kuwa apartheid was not a problem. Mbaya zaidi ni kwamba unatoa ujumbe, pengine bila kujijua, kuwa apartheid ilikubaliwa na watu wengi.
CCM imekubaliwa na watanzania wengi kwa njia halali ya kidemokrasia ambapo kila aliyekidhi vigezo vya kikatiba kupiga kura aliruhusiwa kupiga kura.Vigezo vya kikatiba vya kupiga kura Tanzania havikutenga walio wengi ili wasishiriki kwenye kuchagua vionngozi. Vilevile, wale wote waliokidhi vigezo vya kugombea, akiwemo Dr. Slaa, waliruhusiwa kugombea. Katika Afrika Kusini ya apartheid, hali haikuwa hivi.
Pamoja na kwamba Slaa amebobea kwenye siasa za kilaghai, lakini sasa amefikia hatua anapaswa kuchagua maneno ya kusema. Slaa asiwe TOO DESPERATE kwenye kutaka kuwafanya watanzania waichukie CCM kiasi cha kutoa kauli za kukejeli harakati muhimu kama alizofanya Mandela za kupiga vita ubaguzi wa rangi.
Dr. Slaa anapaswa kujipima na kuomba radhi kwa kauli hii aliyoitoa. Vilevile anapaswa kuchagua maneno ya kusema katika siku zijazo...
Tafakuri: Katika taarifa yake ya kujiuzuru, aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Lindi, alikiri kushirikiana na Dr. Slaa kufanya mikakati mizuri na mibaya kwa nchi yetu. Je, Slaa amekuwa akihalalisha mikakati hiyo mibaya kwa kufananisha na jinsi ANC ilivyolazimika kutumia mikakati ya namna hiyo kupiga vita apartheid?
Rest in Eternal Peace Nelson Mandela...