Dr. Slaa(Balozi): Siendi kutekeleza Sera ya CCM bali Sera ya Taifa. Aongelea sakata zima la Lowassa kuingizwa CHADEMA

Leo tarehe 06/02/2018, Dr. Wilbroad Slaa anaongea na Clous Tv, hakika namwelewa sana huyu mzee.

Kuna kitu kimoja amesema huyu mzee kuwa aliwahi sema kuwa aliamua kuacha siasa za vyama vingi ambazo ni siasa za uvuguvugu. Hivyo yeye hajawahi tangaza kuacha siasa.

Anakili kuwa yeye kwake siasa ni maisha hivyo kumwambia ameacha siasa ni sawa na kusema aachane na maisha. Kimsingi anadai kuwa siasa ni maji, siasa ni elimu, siasa ni chakula, siasa ni biashara na kila kitu unachofanya.

Kwa kauli yake ya kuwa ANAACHANA NA SIASA ZA VYAMA VINGI (opposition parties) kwangu naichukulia hii kauli kama ni kauli ya kuomba CCM, wapime kwa namna yeyote kama anafaa kuwa mtu mhimu kuongoza chama na nchi kwa huko mbeleni.

Kusema kweli upo uwezekano kama yeye binafsi atapenda kujijenga katika CCM, msije shangaa siku moja akawa rais wa jamhuri kupitia CCM.

Hii ndoto yangu ipo wenda ikaja timia na kila mtu atabaki mdomo wazi.

Wenye mtazamo wenu, naomba mawazo yenu.

Kama WATANZANIA wanaohitaji mabadiliko yaendelee, Rais Magufuli Akimaliza Wakati wake, Dr Slaa ashike usukani. Tanzania itaendelea. Sioni mwingine wakuendeleza mufumo wa Rais Magufuli ni Dr Slaa tu. Hapa nakuunga mkono kabisa.
 
Kwani Rais aliepo Sasa Ana mpango wa kuondoka madarakani?

Ok tuamini anaweza kuondoka mda wake ukifika, Leo hii Dr Slaa Ana umri wa miaka takribani 74, wakati anakuja kugombea huo urais atakuwa na umri gani???
 
Ki uhalisia,hawa watu,type ya magufuri,siyo wa kuwapa nchi,maisha yataendelea kuwa magumu,wao wanajikita kwenye economic growth badala ya economic development. mwanzoni niliona category ya watu hawa ni wazuri,ila nimegundua ni hatari kwa maisha ya raia mnyonge,refer mpango wa VAT,,miamala imepanda sana,saiv ili utoe elf 10, unatakiwa uwe na 11500, maana yake ni zaidi ya kodi ya kichwa,,siwatamani type ya viongozi kama hawa
 
Kama WATANZANIA wanaohitaji mabadiliko yaendelee, Rais Magufuli Akimaliza Wakati wake, Dr Slaa ashike usukani. Tanzania itaendelea. Sioni mwingine wakuendeleza mufumo wa Rais Magufuli ni Dr Slaa tu. Hapa nakuunga mkono kabisa.
Slaa amezaliwa 1948, hivi sasa ana miaka 70, baada ya vipindi viwili vya Urais wa Magufuli kwa KATIBA YA SASA, Dr. Slaa kama atakuwa HAI, itakuwa na miaka inayokaribia sana 80. Hatutaki kuipeleka nchi katika level hiyo ya upumbavu ya kumpa nchi mtu Kikongwe
 
Na mke wake anabaki yule yule kichaa? Mbona Tanzania mambo ya msingi ndo tunayafanyia maigizo?
 
nilikua namuheshimu sana ila alipotetea kuhusu lissu kupigwa risasi yaan anaunga mkono kupigwa risasi mh lissu,huyo anachuki na cdm over
 
Siasa ni maisha ni jukumu la kila mtu kuingilia siasa...maaskofu wachungaji na mashekhe wasihusishe na party politics
 
Nimemsikiliza, kwa kiasi kikubwa kaongea vizuri nilipoona kaweka unafiki ni kuhusu kupigwa risasi Lissu.. anyway namuelewa kutoka kuuza supermarket hadi Ubalozi sio kitu kidogo! @Dr Slaa hujamtendea haki Lissu katika mazungumzo yako
 
Back
Top Bottom