Hapa Ghana, nilimwonesha mmoja tu mwanzoni, mfanyakazi mwenzangu, baada ya kama dakika 10, wafanyakazi karibu wote 33, kila mmoja alikuwa na kopi ya hotuba hiyo, na kila mmoja akiomba digital copy ili aweze kuwatumia wenzake, na wengine wamesema wanawatumia viongozi wao wa serikali na wabunge. Kila mmoja ameifurahia, na kusema ndivyo viongozi wa Afrika wanavyotakiwa kufikiri na kutenda. Hotuba hiyo imekuwa ni gumzo.
Kuna yale maneno ya kwenye Biblia, 'Nabii hasifiki nyumbani', nimeamini. Wakati Watanzania walio wengi wameichukulia ni hotuba ya kawaida na baadhi kuibeza, wenzetu nchi nyingine wameipa uzito unaostahili. Ghana ipo juu sana kiuchumi na kidemokrasia ukilinganisha na Tanzania lakini kila aliyeisoma hotuba hiyo amestajabia uzito wa maneno yaliyopo ndani yake, na wengi wanasema kuwa huo ndiyo ulitakiwa kuwa msimamo na mwongozo wa utawala wa Africa.