Dr.Slaa ajibu hoja mbalimbali na kueleza Sera za CHADEMA hapa JF

Swali/maoni langu (yangu) kwako Dk. Slaa:

CCM na serikali yake hairuhusu mkulima kuuza mazao yake mahala anakotarajia kupata faida kubwa, hasa nje ya mipaka ya nchi yetu. Lakini suala la atalimaje, atavuna vipi hilo wamemwachia mkulima. Akivuna basi hapo ndio wanamuwekea masharti. Mara haruhusiwi kuuza mahindi mabichi, n.k.

Je, Chadema kama chama mbadala nini sera yenu tofauti na hii ya CCM na serikali yake. Mnakubaliana nalo, kama sivyo mbona mko kimya????
Nsololi,

Nakushukuru sana kwa maswali mazuri kuhusu sera mbadala ya kilimo, pamoja na hali halisi ya CCM katika kilimo.

Ni kweli hampati nafasi ya kusikia Sera Mbadala ya Chadema katika Kilimo. Sera ya Chadema toka mwaka 1992, ni Soko huria na Biashara ya Soko. Mtu yeyote anayependa kufanya utafiti ataona sera hiyo ambayo haijabadilika hali leo. Kwa msingi huo nikiisha kusema Soko huria sidhani kama ninahitaji ufafanuzi wa kina.

Tatizo la msingi ni kuwa CCM ambayo hadi 1992 Sera yake ilikuwa ni kufuata siasa ya Ujamaa na kujitegemea, iliacha ghafla baada ya 1992 na kuchukua Sera ya Soko huria bila kuandaa wala mazingira wala kanuni zinazosimamia Soko na Biashara huria. Matokeo yake ni kuwa leo kuna Soko holela badala ya Soko huria. Wanaoishi Marekani, Canada na kwingineko wanafahamu kanuni nyingi zinazotawala soko huria hasa EU, smbako kwa bahati nzuri kwa miaka mitano nimekuwa mbunge wa Kuwakilisha Bunge letu kwenye Bunge la ACP-EU ( Joint Assembly pursuant to Lome Convention and later Cotenou Convention).

Ni dhahiri Sera ya Chadema haisikiki kwa kuwa kipindi kisicho cha uchaguzi Sera siyo priority ya vyombo vya habari na tunalizungumza sana kwenye Operation Sangara na mikutano mbalimbali. Sera za Chadema ziko available na zilikuwepo hadi kwenye web page yetu. Anayehitaji anaweza kutumiwa akiomba japo saa hizi tunafanya maandalizi ya kufanya riview kwa ajili ya uchaguzi.
 
CHADEMA IKIPEWA DHAMANA YA KUIONGOZA TZ, KUANZIA BAADA YA UCHAGUZI MKUU UJAO, imejipanga kuwafanyia nini watanzania?
Exaud J. Makyao,

Swali lako ni zuri sana. Naomba nilijibu tu ifuatavyo:

Tuko kwenye kipindi cha maandalizi ya Manifesto ya vyama mbalimbali kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi mkuu. Mtakuwa hamjatutendea haki, tukianza kuyaeleza kinagaubaga mambo ambayo kimsingi yatakuwa kwenye manifesto yetu.

Naomba mtuvumilie tukamilishe ili tusianze kuwanufaisha wengine kabla ya wakati. Msisahau kuna pia maswalaya Plagiarism na watu wakafaidi kiulaini. Kila kitu kinakuja kwa wakati wake.

Kuna namna ya kueleza kwenye mikutano ya hadhara wananchi tutawafanyia nini na ndiyo tunayowaeleza kwenye operation Sangara lakini huwa haiianzii kwenye Majadiliano scientific kama haya, ambayo ni rahisi kunakiliwa na yeyote kwa manufaa tofauti.
 
Dr. Slaa,

Asante sana kwa kukubali kuja kujibu maswali.

SWALI: kuna watu wengi humu JF na nje ya JF wamekuwa wakikupigia debe la kuwa rais au tuseme ugombee urais kitu amabocho wanaamini hata kama hutapata urais unaweza kusaidia kuinua image ya upinzani na kusaidia kuongeza viti vya upinzani bungeni. Je ni kweli unategemea kugombea urais au ni nini msimamo wako kuhusu hili especially kama chama chako kitakusimamisha ukichukulia pia mwenyekiti wako alishatangaza hatasimama mwaka huu kwenye kiti cha urais.
 
Maswali kwa Slaa
2. Wewe uliwahi kuwa katibu wa kanisa katoliki Tanzania, na inasemekana una matarajio ya kugombea urais. vipi uhusiano wako na kanisa lako mpaka sasa? je chama chako kinapata msaada wa maaskofu wa kikatoliki? ili kuwapa upendeleo? uhusiano wako na jamii ya kiislamu ukoje? kuna tetesi kwamba Zitto ni unwanted product huko chadema kwasababu ya dini yake na mnampango wa kumuweka lwakatare kwenye nafasi yake kwa hila ukweli uko vipi? au bado unaendeleza catholism kwenye national level?

3. Uliwahi kuasi upadre (uhusiano wako na Mungu), ukaasi CCM kwa kuwa walikataa kupitisha jina lako. hii inaweza kuwa tabia yako ya kuasi? tukikupa nchi utashindwa vipi kuwa tatizo badala ya tumaini? kama huogopi kumuasi mungu wako utashindwa kutuasi sisi?


Mkuu tumain nafikiri Dr. Slaa ameshajibu haya maswali na kuyatolea ufafanuzi angalia post No. 19 ya thread hii.
 
Naomba kumuuliza Dr.Slaa swali moja:

Katika CHADEMA nimekuwa nikisikia sekta chache tu mada zake zikijibiwa na wakurugenzi wake kama sekta ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa inayoongozwa na Ndg. John Mnyika, Sekta ya Mambo ya Katiba (Tundu Lissu), Bunge na Halmashauri inayoongozwa na John Mrema.

Kuna sekta zingine muhimu kama vile Elimu, Afya, Kilimo nk wakurugenzi wao ni akina nani kama wapo mbona sisikii wakijibu hoja zao kwenye mikutano mbalimbali.

Samahani wanaJF mimi binafsi kweli siwasikii wala siwajui.
Facts1,

Thanks.

Ni kweli mmekuwa mkisikia Matamko yakitolewa na Wasemaji wachache. Ni swala la mpangilio tu, ukichunguza vizuri, hoja zote zinazojibiwa ni thematic bila kufuata kama fulani ni msemaji wa Wizara fulani. Katiba ya Chadema inatamka wazi nani ni wasemaji katika maswala ya Sera na katika maswala ya Utendaji. Hivyo ni suala la mpangilio wa nani anasema au anatoa Tamko gani.

Lakini haina maana kuwa anayelitoa ndiye amelifanyia utafiti peke yake. Ni njia mmoja ya kutoa matamko ambayo ni coordinated. Lakini Chadema imejipanga vizuri na tungeliweza kila Sekta itolewe Tamko na mtu husika wa Sekta hiyo.

Tatu, ni pia swala la mfumo. Makao Makuu haikugawinyika kisekta bali ki idara. Kwa mfano maswala yote ya Elimu yako chini ya Kurugenzi ya Bunge na Halmashauri na pia Vijana kwa vile wahusika wakuu ni vijana.
 
Mimi si-intatein CCM kuendelea kutawala. Na wala si-intatein ulafi na ubinafsi aka umimi wa viongozi wa upinzani wa kutotaka kuungana na kuweza kuing'oa CCM.

Kama upinzani Kenya wameungana na kusimamisha mgombea mmoja wa uraisi na akashinda why not us? Mwishowe wagombea wetu wa upinzani wa nafasi ya urais wanaishia kugawana kura chache chache tu.

Huyo Dr Slaa na wengine wa upinzani they need to change. We people of Tanzania we need changes as well. We are tired of CCM monopoly.

Hivyo wana JF mi kwa mtazamo wangu kweli sijaona wa kum-supot ktk hivi vyama unless nione muungano wa wapinzani unafanyika.

Asanteni wakuu wote.
Tripo9,

The answer can be as simple as you put.

i) Ikumbukwe licha ya policies kuwa Tofauti, interests za viongozi pia zinatofautina. Kama umefanya utafiti wa kutosha utakumbuka kuwa wakati wake Rais Mobutu wa DRC aliruhusu vyama vya siasa mpaka 2000. Maana yake ni kuwa vingine vimeanzishwa au kuwa facilitated na Serikali kwa lengo la kulinda Serikali. Kuna sura pana ya vyama vya aina hiyo hapa kwetu.

ii) Huwezi kuungana na kiongozi wa chama ambaye mchana anacheka nawe lakini usiku anakupiga kisu. Tunaomfano hai. Kauli ya Chadema na hata Katiba ya Chadema iko wazi kuhusu uwezekano wa kuungana na chama kingine "makini". I think that is the key word siyo mataka tu ya wananchi ambao hawajui details ya mambo tunayokumbana nayo kila siku. Kuna kupenda kitu, na kuna kuangalia kama kitu hicho realisitically kinawezekana. Chadema iliisha kuonyesha njia kwa kuunga vyama vya wenzetu, mara mbili. Nadhani nia na dhamira ya Chadema cannot be challenged practically with evidence.
 
Mh Dr Slaa.

Swali langu ni kuhusu msaidizi wako Zito Kabwe. Ameamua waziwazi kujifungamanisha na wale ambao chama kimewatimua, na tena akaamua kuwaunga mkono katika jitihada zao za kupingana na chama. Ameamua kuwasapoti kina Kafulila wagombee ubunge kwa vyama vingine dhidi ya CHADEMA. Je huu si uasi? Naomba msimamo wako juu ya hili.
 
Facts1,

Thanks.

Ni kweli mmekuwa mkisikia Matamko yakitolewa na Wasemaji wachache. Ni swala la mpangilio tu, ukichunguza vizuri, hoja zote zinazojibiwa ni thematic bila kufuata kama fulani ni msemaji wa Wizara fulani. Katiba ya Chadema inatamka wazi nani ni wasemaji katika maswala ya Sera na katika maswala ya Utendaji. Hivyo ni suala la mpangilio wa nani anasema au anatoa Tamko gani.

Lakini haina maana kuwa anayelitoa ndiye amelifanyia utafiti peke yake. Ni njia mmoja ya kutoa matamko ambayo ni coordinated. Lakini Chadema imejipanga vizuri na tungeliweza kila Sekta itolewe Tamko na mtu husika wa Sekta hiyo.

Tatu, ni pia swala la mfumo. Makao Makuu haikugawinyika kisekta bali ki idara. Kwa mfano maswala yote ya Elimu yako chini ya Kurugenzi ya Bunge na Halmashauri na pia Vijana kwa vile wahusika wakuu ni vijana.
Nashukuru Dr. Slaa kwa majibu yako.
 
Dr. Slaa,

Nitashukuru nikipata jibu lako kuhusu swali langu hili ambalo liko kwenye THREAD #7.

Nakutakia kazi njema na mafanikio zaidi.

AmaniKwetu,

Thanks a lot. Kuhusu kugombea Urais. Nimekwisha kulijibu awali. Lakini naomba niseme ifuatavyo:-

a) Awali kugombea Urais ni haki ya kila raia anayetimiza masharti ya kikatiba. Hivyo, Dr. Slaa, hana sababu yeyote iwapo kwa dhamira yake ataamua kugombea. Hata hivyo nisisitize kuwa sina ambition ya nafasi hiyo, hasa kwa kujua kuwa Urais wa nchi kama Tanzania si jambo la kukimbilia. Mwalimu alikwisha kulieleza hili na baada ya kuzunguka karibu wilaya zote, nimeona sababu ya kauli hiyo ya mwalimu

b) Nadhani pia maswala ya kugombea kimsingi yanahitaji taratibu za kichama. Nadhani ni busara kusubiri kauli ya Chadema. Ninachosisitiza ni kuwa Chadema kwa uhakika itakuwa na mgombea Urais makini, atakayebeba siyo tu bendera ya Chadema, lakini pia hisia za Watanzania. Kipindi tulichonacho siyo kama miaka ya nyuma ambapo unabembeleza wagombea kwa kuhofia ajira zao, mafao yao. Watanzania wamepevuka na kuelewa haki zao mbalimbali.

c) Kimsingi, ninapenda kuwaletea jambo ambalo wengi hawajaligundua bado. Ningependa wana JF wote wasome vizuri na kuutafakari mswada wa Party Financing ambao unategemewa kuwasilishwa Bungeni hivi karibuni. Kwa Tathmini ya awali mswada huu japo kwa nje unaonekana kama kondoo lakini ni mbwa mwitu aliyevikwa ngozi ya kondoo. Kuanzia siku chache zijazo, mtaanza kupata tathmini mbalimbali ya mswada huo.
 
AmaniKwetu,

Thanks a lot. Kuhusu kugombea Urais. Nimekwisha kulijibu awali. Lakini naomba niseme ifuatavyo:-

a) Awali kugombea Urais ni haki ya kila raia anayetimiza masharti ya kikatiba. Hivyo, Dr. Slaa, hana sababu yeyote iwapo kwa dhamira yake ataamua kugombea. Hata hivyo nisisitize kuwa sina ambition ya nafasi hiyo, hasa kwa kujua kuwa Urais wa nchi kama Tanzania si jambo la kukimbilia. Mwalimu alikwisha kulieleza hili na baada ya kuzunguka karibu wilaya zote, nimeona sababu ya kauli hiyo ya mwalimu

b) Nadhani pia maswala ya kugombea kimsingi yanahitaji taratibu za kichama. Nadhani ni busara kusubiri kauli ya Chadema. Ninachosisitiza ni kuwa Chadema kwa uhakika itakuwa na mgombea Urais makini, atakayebeba siyo tu bendera ya Chadema, lakini pia hisia za Watanzania. Kipindi tulichonacho siyo kama miaka ya nyuma ambapo unabembeleza wagombea kwa kuhofia ajira zao, mafao yao. Watanzania wamepevuka na kuelewa haki zao mbalimbali.

c) Kimsingi, ninapenda kuwaletea jambo ambalo wengi hawajaligundua bado. Ningependa wana JF wote wasome vizuri na kuutafakari mswada wa Party Financing ambao unategemewa kuwasilishwa Bungeni hivi karibuni. Kwa Tathmini ya awali mswada huu japo kwa nje unaonekana kama kondoo lakini ni mbwa mwitu aliyevikwa ngozi ya kondoo. Kuanzia siku chache zijazo, mtaanza kupata tathmini mbalimbali ya mswada huo.
Asante.

Naamini ndiye utakuwa mgombea toka CHADEMA ambaye utaungwa mkono na vyama vya upinzani na Watanzania wengi.
 
Dr. Slaa

tunashukuru kwa ufafanuzi wako makini.

SWALI: Katika ufuatiliaji wako wa lile sakata la CCM kuingiza magari na kukwepa kiasi kikubwa cha kodi, je walikwepa kiasi gani? na je, wamelipa kiasi walichokwepa?
 
Mh. Dr. Slaa.
Swali:

1. Kutokana na mahojiano kwenye kituo kimoja cha telivisheni hapa nchini, mmoja wa viongozi tuliowapa dhamana ya kiongoza CHADEMA (NAIBU KATIBU MKUU WAKO) kueleza waziwazi kwamba, yeye atakuwa tayari kusaidia watu walio nje ya CHADEMA kupigania ubunge badala ya kuhakikisha kwamba CHADEMA inapata mgombea anayekubalika na kupata ushindi. Wewe kama kiongozi na mwanachama nini maoni yako kuhusu hili?

2. Kulingana na majibu yaliyokuwa yakitolewa wakati wa mahojiano katika telivisheni siku ile, Mtanzania yeyote yule ameweza kuelewa kwamba Mh. Zitto ni zaidi ya CHADEMA. Endapo tunakuwa na viongozi wa aina hii ndani ya CHADEMA nini mustakabali wa chama kwa siku za baadaye na hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguza mkuu mwakani?

3. Mh. Zitto kwa kauli yake mwenyewe amesema siasa halikuwa chaguo lake la kwanza. Ki maantiki hii ni kauli ambayo wanachama wengi wa CHADEMA hawakutarajia itolewe na mtu kama Mh. Zitto. Je, chama hakioni kwamba Mh. Zitto anajenga hoja za kutaka kufukuzwa CHADEMA ili ionekane siasa za upinzani Tanzania zimeshindwa kutimiza malengo yaliyotarajiwa? Na nini kauli ya Kamati Kuu kuhusu hili?

MAONI YANGU:

HAKUNA MAHALI POPOTE DUNIANI KIONGOZI KUJIONA NI ZAIDI YA CHAMA AU TAASISI. IKISHAFIKIA HAPO AMA KIONGOZI HUYO HATA AWE MSOMI NA MAARUFU KUPITA KIASI "ATAKUWA NI MUFILISI KISIASA" NA NI VYEMA AKATOKA NA WALA ASINGOJE AIBU. HATA KAMA AMEZALIWA NDANI YA CHAMA AU TAASISI HIYO.

ALUTA NA MAPAMBANO YATAENDELEA DAIMA.

Ni wazi upo katika mapambano. Tatizo ni kuwa kwa lugha hii ya kichonganishi na chuki sijui mapambano yako ni kwa faida ya nani. Siamini kama ni kwa faida ya wapenda demokrasia ama hata kwa CHADEMA kama chama chako kama ambavyo unataka wanajamiiforums waamini hivyo.

Na kama ni kweli wewe ni mwana CHADEMA basi ni wazi safari ya mabadiliko makini bado ni ndefu sanaaaaaaaa.



Mh Dr Slaa.

Swali langu ni kuhusu msaidizi wako Zito Kabwe. Ameamua waziwazi kujifungamanisha na wale ambao chama kimewatimua, na tena akaamua kuwaunga mkono katika jitihada zao za kupingana na chama. Ameamua kuwasapoti kina Kafulila wagombee ubunge kwa vyama vingine dhidi ya CHADEMA. Je huu si uasi? Naomba msimamo wako juu ya hili.

Kweli kina MREMA LYATONGA wako wengi na CHADEMA msipokuwa makini kutambua ni hasa ya watu hawa ni wazi maendeleo ya demokrasia nchini yatakuwa yamepigwa kumbo kufikia 2011. By the way, Zitto ni NAIBU Wa DR SLAA na sio msaidizi. Ni wazi huyu siyo "mwenzenu" CHADEMA

Dr Slaa,

Mantiki ya kuingilia hapa sio kujifanya mjuaji ila ni kutoa tahadhari na baadhi ya maswali yanayokuja hapa ambayo nia yake ni kuendelea kuwachanganya CHADEMA na watanzania kwa ujumla.

Nina maswali lakini naamini kwa hali ilivyo sasa ni vizuri nikakuuliza pembeni kwani naamini hilo linawezekana.

Omarilyas
 
Exaud J. Makyao,

Swali lako ni zuri sana. Naomba nilijibu tu ifuatavyo:

Tuko kwenye kipindi cha maandalizi ya Manifesto ya vyama mbalimbali kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi mkuu. Mtakuwa hamjatutendea haki, tukianza kuyaeleza kinagaubaga mambo ambayo kimsingi yatakuwa kwenye manifesto yetu.

Naomba mtuvumilie tukamilishe ili tusianze kuwanufaisha wengine kabla ya wakati. Msisahau kuna pia maswalaya Plagiarism na watu wakafaidi kiulaini. Kila kitu kinakuja kwa wakati wake.

Kuna namna ya kueleza kwenye mikutano ya hadhara wananchi tutawafanyia nini na ndiyo tunayowaeleza kwenye operation Sangara lakini huwa haiianzii kwenye Majadiliano scientific kama haya, ambayo ni rahisi kunakiliwa na yeyote kwa manufaa tofauti.
Asante mheshimiwa.
Jibu lako ni makini.
 
Huwezi kuungana na kiongozi wa chama ambaye mchana anacheka nawe lakini usiku anakupiga kisu. Tunaomfano hai. Kauli ya Chadema na hata Katiba ya Chadema iko wazi kuhusu uwezekano wa kuungana na chama kingine "makini". I think that is the key word siyo mataka tu ya wananchi ambao hawajui details ya mambo tunayokumbana nayo kila siku. Kuna kupenda kitu, na kuna kuangalia kama kitu hicho realisitically kinawezekana. Chadema iliisha kuonyesha njia kwa kuunga vyama vya wenzetu, mara mbili. Nadhani nia na dhamira ya Chadema cannot be challenged practically with evidence.

Nashukuru sana Dr. Slaa kwa maelezo haya.

Kweli hizo ni challenges kubwa ambazo mi mwananchi wa kawaida siwez zitambua.
 
Dr. Slaa,

Chama chochote chenye nguvu zaidi vijijini kuliko mijini, kina nafasi kubwa zaidi ya kushinda uchaguzi mkuu.

CHADEMA imejizatitije kujiimarisha vijijini kuliko mijini?
 
Thanks Dr Slaa

Maswali yangu mafupi mawili:

1. Bado Chadema Mnakubaliana na muundo wa tume ya uchaguzi kama hamkubaliani nao mna mpango gani wa muundo huo kabla ya uchaguzi Mkuu kwani kuna chama kingine kimeenda mahakamani kuukataa muundo huo.

2.Mkiwa wabunge wachache wa upinzani mna mpango gani na muswada sheria mpya ya matumizi ya fedha (part financing) kwenye uchaguzi baada ya kuonekana sheria hiyo inawabana nyie huku ikiwapendelea chama tawala pindi itakapoletwa kwenye bunge lijalo

Asante

Mh. nitafurahi sana nikipata majibu ya maswali yangu
 
Mh Slaa,
Pole na kazi, ningependa fahamu kwani hamuwezi fanya maendeleo yoyote yenye kulenga kuwanufaisha watanzania?kwani ni lazima muingie ikulu ndo mtufanyie hayo maendeleo mnayosema?
 
Back
Top Bottom