Dr Slaa afunga barabara Mwanza

Katika jambo lisilotarajiwa na wengi, Dr Slaa amepita katikati ya maduka hapa jijijini Mwanza huku akiamsha taharuki kwa mamia ya watu wakitaka kumwona. Dr Slaa akiwa ameambatana na mbunge wa Nyamagana mh Wenje alipata wakati mgumu baada ya kila mtu kutaka kumsalimia. Nimeshuhudia magari yakipiga honi na abiria walikuwa wanashuka kwenye daladala wakikimbilia eneo aliopo. Kesho kuna uchaguzi wa meya wa jiji la Mwanza, yawezekana ujio wa Dr ni mahususi kwa shughuli hiyo.

hii hali naifananisha na ndoto niliyoiota majuzi, kwamba nilifika maeneo ya Tabata Aroma nikamkuta amekaa na wadau kadhaa kando kidogo ya barabara kwenye viti wakiwa wanaabadilishana mawazo. Nikampa mkono (ila nilisalimiana nae kwa mkono wake wa kushoto. Kwa mujibu wa ndoto yangu bado una maummivu kiasi ila baadae tukasalimiana kikawaida). Sekunde zilivyokuwa zikisogea watu walionekana kuongezeka pale tulipokuwa na Dk. Watu wakawa wengi sana wakitaka kumpa mkono wa salam. Hali iliyokuwepo ilibidi wapambe wamtoe pale na kumwingiza nyumba iliyokuwa jirani kwa usalama wake. Nao watu bado wakawa wengi pale nje, na barabarani kukawa kumejaa sana na brass band ikawa inapita kwa ajili ya Dk
 
Natabiri vurugu kwenye uchaguzi,huyu babu hana busara anaenda kuchochea mtafaruku.
 
MWZ ni tumaini na mtaji mkubwa kwa chadema, tujipe muda, ccm hawakusoma planning, hawajui kwamba kuna kizazi kijacho, chuki inazidi juu ya serikali ya magamba, wao wanawapeleka watoto wao shule nzuri huku hawa walala hoi wakishindwa kuwasomesha watoto wao. Unamkuta Zomba, na RItz mishipa ya uso imewatoka... eti wanaitetea CCM.
 
Ni dalili njema!!! Nape upo? Ritz, Rejao, Zomba et al mmesikia marafiki zangu. Heri mimi mshabiki sina kadi!!! Ninachoangalia ni mateso ya watanzania walio wengi ambao 67.9% wanaishi chini ya dola 1.25 kwa siku!!! Wengine hata mia hawana na ardhi walishanyang'anywa na wachimba madini.

acheni kugombania madaraka.wananchi walishaanza kuiamini cdm lakini kwa jinsi mambo yanavoenda ndani ya chama watu wanaanza kustuka.hebu angalia na tafakari vurugu za juzi hadi mbunge anaingia chini ya meza.
 
acheni kugombania madaraka.wananchi walishaanza kuiamini cdm lakini kwa jinsi mambo yanavoenda ndani ya chama watu wanaanza kustuka.hebu angalia na tafakari vurugu za juzi hadi mbunge anaingia chini ya meza.

Kutoelewana ni mambo ya kawaida. Hata SSM si ngumi zipo? Si kuna diwani anauguliwa muhimbili kwa sababu ya kichapo toka kwa mgombea wa NEC? Haya masuala ni inevitable na ukizingatia CDM kuna pia mapandikizi maana ni mchezo wanaupenda sana upande ule wa pili. Si wote wanaoleta fujo CDM ni CDM? Wapo waliotumwa wengi ila wanashindwa kwa uwa maji yake ni marefu na mziki wake ni mnene!!
 
Miaka ya nyuma tulikuwa tukisikia kiwete anapindapinda huko barabarani tulikuwa tunatoka na kupiga vigelegele. Siku hizi tukisikia anapinda mjini tunaenda kumzomea.
Maswali yangu ni haya: Je ni kwa nini viongozi hawajifunzi na kuona kuwa kwa sasa watu wanajua ni nani kiongozi wa ukweli? Huyu baba anajipitia ila wenyeji wanafurahishwa na matendo yake na nia yake ya kutukomboa. Kwa nini tusimshangilie?
 
Back
Top Bottom