Dr. Slaa aanza ziara nzito Nyanda za juu Kusini

Dr. Slaa aanza ziara nzito Nyanda za juu Kusini

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa kesho anaanza ziara rasmi ya nyanda za juu kusini itakayomfikisha katika mikoa ya Mbeya,Rukwa na Katavi.

Taarifa iliyothibitishwa na msemaji mkuu wa CHADEMA Tumaini Makene inasema kiongozi huyo maarufu nchini atafanya mambo makubwa matatu katika ziara hiyo ambapo ni kukagua zoezi la uandikishaji wapiga kura kwa njia ya BVR,kukagua shughuli mbalimbali zinazofanywa na chama na kuhutubia mikutano ya hadhara.

Kiongozi huyo atahutubia mikutano ya hadhara katika miji ya Vwawa,Tunduma,Sumbawanga na Mpanda.

Tayari matayarisho yote muhimu ya mapokezi ya kiongozi huyo yamekamilika.
 
Mungu akujali afya kamanda, tunauthamini uwepo wako...

BVR wamulikwe wanafanya hujuma sana...

Dr Slaa amevumbua mambo mazito alipokuwa anakagua zoezi hili kule Kagera.
 
Kila la heri raisi wetu mtarajiwa Mungu akulinde.
 
Daaaah!! Hii waswahili wanasema ugali moto mboga moto. Kule Mbowe huku Slaa pale Lissu hapa Lema mamaaaaaa!!! CCM hawachomoki awamu hii

Na ndiyo maana tunasema Chadema ni Taasisi.Hiki siyo chama cha Oneman show!
 
Mungu aendelee kukupa afya njema akika bila ww mie sipigi kura.
 
Kama walifikiri chadema ni chama cha msimu, sasa ndio kwanza kazi ndio kwanza inaanza IMBA UKOMBOZI OPERATION inamaliza nyanda za juu Rais anaanza magamba ngoma inogile mwaka huu.
 
Back
Top Bottom