Dr. Shein kuelekea 2015...

Dr. Shein kuelekea 2015...

Kamanda ZeM, nina imani watu wengi tunahisi amefika hapo alipo kwa sababu waheshimiwa walitaka mtu asiye na uwezo wa kuwa-challenge, mtu wa 'yes' 'yes' na mtu wasiyemuhofia kwa lolote....

Frankly, sioni huyu Dr. Chein akipewa nafasi ya kugombea urais whether 2010, 2015 au muda wowote ule!

Sasa hivi afya yake haiko ''perfect'' ngoja tuone itakuwaje hapo 2015.
Swala la yes yes, i dont think so. Shein ni challenger kuliko anavyoonekana kwa haraka haraka.
 
SHEIN FOR PRESIDENT 2015.
Ana sifa zote za kuwa kiongozi kwa nchi masikini kama Tanzania.Bongo hatuhitaji kiongozi mwenye mvuto ,tunaitaji kiongozi serious hakuna kuchekacheka ni kazi tuu kwa kwenda mbele.Mambo ya mivuto tuwaachie akina Obama, nchi yao tajiri
Hao waliopita na mivuto yao wamefanya nini zaidi ya ufisadi tuu.
SHEIN FOR PRESIDENT- 2015
 
SHEIN FOR PRESIDENT 2015.
Ana sifa zote za kuwa kiongozi kwa nchi masikini kama Tanzania.

Kamanda mauzauza, naomba tuelimishane kidogo...

- Shein ana sifa gani hasa za kumfanya a-qualify kuwa president wa 'nchi maskini kama Tanzania?'
- Nchi maskini kama Tanzania inahitaji mtu mwenye sifa gani kwa nafasi ya President?
- Unafikiri hata akipewa rungu kamili, atafanya lipi la ziada kupita yale ameyoyafanya (kama yapo) kwa muda wote aliokuwa VP?
 
Tunahitaji kutafakari na kuona nini na wapi kafanya mapinduzi ya kiutendaji na kifikira na kuleta tija ili kwa kile kidogo alichofanya kiweze kuamini anaweza kufanya kitu kikubwa.
otherwise nchi hii ina ombwe kubwa la uchaguzi na hatuna budi kujifunza namna ya kugroome na kuchagua viongozi.
 
Ok mkuu kwa hiyo unaona anayefaa yuko nje ya serikali mkuu? Na kama siyo Shein kwa sasa unaona nani mwenye muelekeo wa kufaa kumpokea JK? Kwa sasa mimi naona upinzani kuchukua ni ndoto labda yatokee mabadiliko ya ghafla na ya uhakika otherwise yoyote tutake ishia kumchagua atakuwa ndani ya serikali au CCM. Hapa tuna badilishana mawazo tu ndiyo niya ya thread.

MWANAFALSAFA,
Hata falsafa za wahenga, haziwezi kuamini kuwa mtu ambaye yuko kwenye nafasi ya juu sana kama makamu wa rais katika serikali ambayo baadhi ya watu wanataka isiendelee kutawala, eti anaweza kuwa ni dawa kwa serikali hiyo hiyo.
Mkuu,
Atakaye fanya kinyume na serikali iliyoko madarakani, lazima awe nje ya serikali hiyo, au awe hana nafasi kubwa kwa sasa.
Mimi sijui ni nani, kwasababu sina shida kubwa na serikali iliyoko madarakani hasa upande wa head of state.
Shida yangu ni kidogo tu, Uozo ulioko kwa wale waliodhaminiwa kumsaidia Rais.
Sioni Rais akisaidiwa mkuu.
 
Inaelekea Shein ni mkimya sana. Makamo wetu wa raisi huyu kwangu mimi ndiye ninayeona anayefaa kuongoza nchi 2015. Hayupo kwenye spotlight sana kama viongozi wengine wakuu. Katika viongozi tulionao mimi naona huyu mzee ni moja kati ya waliyo bora maana haendekezi siasa za jukwaani. Sijui kwa nini yeye hatajwi kati ya moja ya watu wanaoweza kumrithi JK, labda mwenyewe hautaki uraisi. Ukilinganisha na viongozi wengine wanao tajwa tajwa sasa mimi naona so far namsupport Shein for 2015.

Sababu zangu ni zifuatazo.
1.Hajaonyesha tamaa wala uchu wa madaraka.

2.Hana skendo yoyote kubwa anayo tajwa kuhusika.

3.Haelekei kuwa na makundi

4.Ni mpole na hapendi spotlight kitu ambacho kinaweza kuashiria he is all action and no talk.

5.Tetesi niliyo sikiaga ni kwamba 2005 Kikwete alikua na mgombea mwenza wake mwenyewe lakini baada ya majadiliano wakaona kwamba Shein ndiyo anafaa kuwa kwenye tiketi ya chama.

Sijui kama mwenyewe ana ndoto za 2015 lakini kwenye kundi la sasa yeye anaonekana kufaa kuliko wenzie. Wanaweza kutokea wengine wanaofaa kabla ya 2015 ila kwa sasa nimemuona huyu. Haya ni maoni yangu tu wakuu sijui nyie mna semaje.

Ushauri mzuri lakini sifikiri (CCM ZANZIBAR) kama watalikubali hilo sababu watakwambia anatokea pemba,pia sifikiri watu wa makanisa kama watalifurahia hilo kuendelea kuwapo Muslim kiongozi wa nchi ,Maskofu watacharukwa na kulipinga hilo.
sema ukweli ijapokuwa unauma
 
jamani muacheni akapumzike huyu mzee wa watu haiwezi hii nchi iliyojaa fitnaa...na uzandiki wa kila hali...haiwezii jamanii....muacheni akapumzike.period
 
Ninachofahamu mimi(ingawa hakiko kwenye KATIBA ya JMT) ni kuwa Zanzibar ni NCHI na ina RAIS wake. "Tulikosea" tukampa Mzee Mwinyi Urais wa JMT mwaka 1985. Sidhani kama ni sahihi kumpa Mzanzibari Urais wa JMT.
 
Ukilinganisha na viongozi wengine wanao tajwa tajwa sasa mimi naona so far namsupport Shein for 2015.


Mwanafa1 kwanini usiseme 2010 unasema 2015? Bongo nzuri jamani hata uwe kituko vipi utaongoza kwa miaka 10. Hivi kwanini tusiwe na vigezo vya utendaji wa kazi kama kipimo cha kuendelea na urais? So ukishakuwa presidaa hata kama kazi imekushinda unachoweza ni kusafiri tu still utapewa miaka 10? Hii inauma sana kwa kweli hata si kidogo.

Anyway nirudi kwa Shein, sijuwi mimi namwona kama hayuko practical vile. Vitu vingi alivyokuwa anavisema kwenye kampeni mwaka 2005 ilionekana wazi vilikuwa kwa ajili ya kuumba kura tu na si zaidi ya hapo. Lakini pia upole wake inaweza kuwa ni hasara kwa watz kwa maana kwamba ufisadi unaweza kudouble kwa sasa.
 
asante mkuu. Lakini bado sijapata kitu cha kushika hapo. Kama yeye ndiye anayemsaidia rais, anatakiwa anakolegea rais yeye apakazie. Sawa jamaa sio muongeaje, hiyo siyo sifa ya kuwa rais. Ni kipi hasa ambacho mtu anaweza akasema shein alikisimamia kikaa vizuri? Huyu mzee ni kama sumaye, japo yy anaweza akawa sio fisadi lakini hana ile drive na determination ya ku-dare mambo kwa maslahi ya taifa. Huyu alikuwa picked na mzee mkapa kwa maslahi binafsi kama alivyofanya kwa sumaye.
Tatizo anaweza akawa kondoo kabisa mafisadi wakatamalaki...bado nahitaji kuelimishwa tafadhali.

huitaji kuelimishwa wewe unaelimisha hapa kutokea mwanzo wewe ndio unaielewa hii mada ukiacha kuchangia na sign out. Unaona mbali.
 
Usianze balaa lako - Shein ni 2010 kule Zanzibar.
 
Hata mie nadhani Shein ni mpole sana kupambana na mafisadi waliokubuhu ndani ya nchi hii. Akiwa raisi watamtia kizunguzungu!!!!! Na kama ni replacement ya raisi, tunaihitaji mwaka 2010!!!!!
 
Mimi kwa mawazo yangu Rais atakayeleta mapinduzi ya kweli katika system nzima ya nchi hii lazima atoke nje ya hawa walioko serikalini leo,sina maana atoke vyama vya upinzani ila atoke nje ya hawa tunaowaona leo. Ninasema hivi kwa sababu wengi wa hawa ni walewale huyu ni mwenzangu/mwenzetu n.k, kama kuna umuhimu huo wa kuwa na Rais atokaye ndani ya hawa labda awe Magufuli nasema labda.

Lakini ili tuendelee tunahitaji Rais ambaye anaona mbali ya uchama wake, anaona mbali ya urafiki ambaye atasema kwa sauti moja na watz waliowengi, haijalishi kama ni dictator au ni chizi, kwa mana tz ya sasa ilituendelee na tuachane na haya tuyaonayo leo lazima Rais ajaye awe na level fulani ya uchizi ili kuibadilisha system ya nchi hii. waliopo hawawezi kufikia level hiyo, ndo mana nikasema labda Magufuli.

Nawasilisha.
 
SHEIN FOR PRESIDENT 2015.
Ana sifa zote za kuwa kiongozi kwa nchi masikini kama Tanzania.Bongo hatuhitaji kiongozi mwenye mvuto ,tunaitaji kiongozi serious hakuna kuchekacheka ni kazi tuu kwa kwenda mbele.Mambo ya mivuto tuwaachie akina Obama, nchi yao tajiri
Hao waliopita na mivuto yao wamefanya nini zaidi ya ufisadi tuu.
SHEIN FOR PRESIDENT- 2015

Kweli ndugu yangu Mauza uza una mawazo ya kimauzauza. Shein amekuwa serious katika lipi? au u-srious unaousema ni kutokukenua meno? Changamoto tulionayo katika nchi hii kwa sasa ni kuondoa ufisadi.Hata rais aliyepo sasa anaukemea sana ufisadi(japo ni vigumu kujua kama anamaanisha asemayo) lakini umemsikia Shein akikemea hata siku moja? Naamini kabisa Shein ni mwoga, na hawezi kuwa rais wa nchi iliyobanguliwa na mdudu ufisadi kiasi hicho.
 
Lakini............. tunahitaji Rais ambaye ''''''''''''''''''''', haijalishi kama ''''''''''''''''' ni chizi, ,,,,,,,,,, lazima Rais ajaye awe na level fulani ya uchizi.''''''''''''''''''

CreativeThinker

Kama hivi ndo kuwa CreativeThinker mimi naogopa.

Mkuu ni wewe na nani hamtajali kama Rais ajaye atakuwa CHIZI au kuwa na kiwango fulani cha UCHIZI?

Mimi katIka hilo LA UCHIZI, sipo. Sipo kabisa mkuu.

Natarajia tupate RAIS MWENYE AKILI TIMAMU na SOUND MIND.
 
Ndugu zangu naomba kama kuna jina ambalo mnadhani linafaa kujadiliwa liwekwe jamvini, sio la huyu mzee Shein ambaye vingezo vya kuteuliwa na Mkapa ni mysterious mpaka leo.
 
Aingie wapi jamani, amekuwa huko miaka 10, hiyo 10 mingine ndo atafanya nini?? Me sijaona bado
 
Back
Top Bottom