Ishu ni kutokana na watu kudhani kuwa akili zetu zaweza kutatua kila kitu bila kufuata kanuni zinazotawala maisha ya binadam!
Tumepewa akili kufikiri ila kwa vitu ambavyo vishawekewa mipaka huna haja ya kutumia akili yako lazma uumie.ingekuwa akili ya binadam yaweza kila kitu ungeweza kutembea, kusema, na kufanya chochote mwenyewe baada tu ya kuzaliwa! Bt hukuweza yote hayo, na kanuni hiyohiyo ndiyo inayotumika kukukuza ambapo huwezi kuuzuia uzee wala hutaweza kutumia akili yako kuzuia kifo!
Kwa hiyo maumbile yako yenyewe yanakiri kufuata kanuni iliyowekwa na MUUMBA, why sasa ktk kipindi unachodhani una akili sana ya kufikiria usifuate kanuni hizo!?
Huu ni ukumbusho tu ndugu zangu, ee MOLA shuhudia nimefikisha japo kwa uchache kile ulichoniwezesha...