Dr. Mpango, katikati ya simanzi, kuna faraja na tulizo

Dr. Mpango, katikati ya simanzi, kuna faraja na tulizo

Dr. Mpango ona jinsi watz wanavyokupenda
 
Huwa natafakari na kujiwazia na kushangaa pia pindi ninapo kutana na watu wenye hisia za hivyo kama zako juu ya mtu mwingine ambaye hauna unasaba nae pia maisha yake ni bora mara 100 ya kwako, how do you get those feelings? Au mie nipo tofauti? Naona hata huko Instagram au Twitter watu juu ya wasanii.
 
Huyu Mpango huyu, sio yule tuliyemtizamia kweli? Kuna kila harufu ndiye [emoji1787]
 
Dr mango haiba yake ya upole na unyenyekevu itaendelea kumpa mambo mengi , Mimi namkubali huyu mzee
 
Dr. Mpango ni miongoni mwa watu ambao ningekuwa na access naye, ningefarijika sana kuonana naye. Lakini kujua tu kuwa yu mzima, ni zawadi kubwa ya kutosha.
Ni faraja kwa wengi wetu kufahamu Makamu wa Rais ni mzima na buheri.

Lakini hali za nmna hii, hasa nyakati hizi za siasa za hovyo, mtu huwezi kushindwa kujiuliza kama hakuna aina ya njama katika maswala kama haya.

Makamu wa Rais ni kiongozi mkubwa sana katika serikali yetu. Itakuwaje, na ni nani hasa anayeruhusu hali ya sintofahamu namna hii itokee huko huko serikalini?

Hizi siyo njama za kutaka kumlaininisha ili awe sehemu muhimu ya 'chawa'?

Hii ni njia inayotumika atoke mbele zaidi kuunga mkono juhudi?

Mimi ninalisoma hivyo tukio hili.
 
Something is wrong. Hata kama kaonekana, ndani kuna fukuto. Haiwezekani Makamu wa Rais aondoke na kurejea kimyakimya licha ya uvumi. Kuonesha kwamba alikuwa nje kweli, taarifa ya kurejea kwake ingetangazwa kama taarifa rasmi
Ukweli ndo huo.

Hapa Makamu wa Rais katumika na kapewa ujumbe maalum, achangamke, asiwe baridi na juhudi za kuunga mkono 2025.
 
Back
Top Bottom