Dr Manyau Nyau kumrudisha Kanumba...

Kanumba, rest in peace ''Ong'wise'', watu wanataka kutengeneza jina kwa mgongo wako...
 
ha ha ha ha! umenichekesha sana na wewe ni msaidizi wake nini? maana ulivyokimbia naye da poleni sana

mimi nia yangu ilikua kuona jinsi anavyo kamata misukule. isitoshe nilikuwa sijawahi ona msukule so nilitaka nishuhudie mwenyewe. Nilipofika pale bima kuna bar fulani inaitwa chem chem, ikanibidi nipumzike nianze plan za kuchukua daladala. so mimi niliishia hapo but waliendelea hadi maeneo ya segerea. watu walikua kama buku nne. plani ilikua kumfufua na amina pia.
 
mlikua mnakimbia riadha.

hapana, tulikuwa tunatembea mwendo wa haraka. tulikamata chuma ulete wanne humo njiani wakaunganishwa kwenye msafara. sijui waliishia wapi. hata hiyo ya Kanumba nikisia anapo anzia lazima niunge tela nione anavyo umbuka au umbua watu. hehee...mnitaarifu mkisikia.
 
Enyi Wagalatia ni nani aliyewaloga? Anataka watu wamwamini? Apeleke upuuzi mbali huko,kwanini asionyeshe anachoweza kabla hata kupelekwa Muhimbili au tuseme kifo kilikuwa siri. Wakati mtu amekufa hakuwepo hapa nchini? Tanzania huo ndiyo msiba wa kwanza kutokea mbona anataka kuleta mambo ya kusadikika,huyu mapusi sasa watu watamfanyia kazi.
 
manyaunyau anatisha. pale mwananyamala alifukuza mchawi mchana kutoka pale kwa bi zakalia ndani kwa ndani hadi kwa mtogole watu kibao wanamfuata akanyosha hadi manzese huku ameshikilia paka mdomoni na vijana wake wakipiga ngoma, akanyonya hadi mabibo ndani kwa ndani hiyo mi nikaunga tela, tukaibukia external tukapita makuburi tukatelemka tukapanda tukaibukia kimanga, akadaka paka mwingine kanyonya damu, tukaenda hadi tabata visiwani hadi tabata bima hiyo ishafika saa 12 jioni....

Sasa mkuu hukuchukua hata picha tuone Nyau wa mtaani wanavyopungua statistically. na hilo kundi lote lilikuwa linauga tu, na shugukli walizoacha nazo ni vipi? Maana wabongo ni kama hatujambo kwa hilo. sawasawa na mdundiko ukipita, kila mtoto huyooo.

ONYO: If you like your cat, don't let him near daktari 'catcat'
 
ha ha ha ha.............Dubu uzalendo umenishinda, kwa mara ya kwanza najitumbukiza JF.....umenichekesha mpaka basi......so fuuuuunnnnyyy..................
 
hapana, tulikuwa tunatembea mwendo wa haraka. tulikamata chuma ulete wanne humo njiani wakaunganishwa kwenye msafara. sijui waliishia wapi. hata hiyo ya Kanumba nikisia anapo anzia lazima niunge tela nione anavyo umbuka au umbua watu. hehee...mnitaarifu mkisikia.

Mlijuaje kuwa wale ni chuma ulete?
 
Hata Sokoine alipofariki 1984 tulisikia mengi. Wakadai kageuzwa msukule. Mganga mmoja akadai ana uwezo wa kumrudisha lakini eti aliomba ruhusa kwa Nyerere akakataliwa! Tukasikia uvumi kuwa Sokoine kaonekana Kariakoo wakati alishazikwa Monduli-Juu! Uvumi tu. Na huyu Manyaunyau ni walewale. Lakini ana ujasiri wa ajabu sana, hebu fikiria anavyomkata paka shingo na kunyonya damu yake! Hiyo tu inatosha kuwabadili watu akili maana wanaamini haiwezekani mtu anywe damu ya paka bure tu! Loh, tunayo kazi!
 
jamani mbavu zangu mie kwi kwi kwi
dubu we ni noumer,i wish tungekuwa wote siku hiyo ya kumfufua SK
hapana, tulikuwa tunatembea mwendo wa haraka. tulikamata chuma ulete wanne humo njiani wakaunganishwa kwenye msafara. sijui waliishia wapi. hata hiyo ya Kanumba nikisia anapo anzia lazima niunge tela nione anavyo umbuka au umbua watu. hehee...mnitaarifu mkisikia.
 
Mlijuaje kuwa wale ni chuma ulete?

yeye anawafahamu. yaani akishaanza kazi anapandisha mzuka anakua kama nyama ndo maana anakunywa damu ya paka ili mashetani yapande. kwahiyo akimuona mchawi anamtambua na kutokana nguvu kuzidiana mchawi anakua mpole na kuomba msamaha asidhuliwe. so chuma ulete alikua anasema huyu ni chuma ulete mara wanaanza kukimbizana hadi anamkamata na anasalimisha zana zake kwa manyaunyau. ukibisha anakupaka dawa, kama ni kweli utawashwa hadi uvue nguo
 
Sasa mkuu hukuchukua hata picha tuone Nyau wa mtaani wanavyopungua statistically. na hilo kundi lote lilikuwa linauga tu, na shugukli walizoacha nazo ni vipi? Maana wabongo ni kama hatujambo kwa hilo. sawasawa na mdundiko ukipita, kila mtoto huyooo.

ONYO: If you like your cat, don't let him near daktari 'catcat'

Picha ninazo. ntakuwekea baadae coz sasa hivi sina access. manyaunyau mwenyewe kijana tu kama super nyamwela.
 
Huyu kanyumba alikuwa maarufu enh!naona habari zake nyingi humu kwani ndo yule wa tangazo la haki elimu?kafa lini kwani huyu?
 
Hiyo, noma. Sijawahi ku comment, ila imebidi leo. Nimekaa na watu hapa hadi wamenishangaa nlivocheka. Kweli ulikua committed!
 
Back
Top Bottom